EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, December 2, 2014

SHEHE AFIA KABURINI AKIZIKA

 
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
Aliyekuwa Shehe Mkuu wa Bakwata Wilaya ya Mbeya, Abubakar Mketo amefariki dunia mwishoni mwa wiki iliyopita  kufuatia kuanguka ghafla makaburini wakati akitoa mawaidha ya Kiislam ya jinsi waumini wanavyotakiwa kuishi katika ulimwengu wa dhambi! Inauma sana!
Shehe aliyefariki akizika.
Tukio hilo lililowaacha watu na machozi lilijiri katika Makaburi ya Nonde jijini hapa wakati wa mazishi ya marehemu aliyejulikana kwa jina la Mayasa Salmini au  Bibi Majuto aliyefariki dunia katikati ya wiki iliyopita.

ILIVYOKUWA
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, baada ya kumaliza kuusitiri mwili wa marehemu Bibi Majuto ndani ya nyumba yake ya milele, Shehe Mketo alisimama na kuanza kutoa mawaidha kwa waombolezaji waliohudhuria mazishi hayo akiwaelekeza namna ya kuishi kwa kutii amri za Mungu na kufuata njia zake kwa vile hakuna anayejua atakufa lini kama ilivyokuwa kwa marehemu Bibi Majuto.
HEBU MSIKIE
Vyanzo vinadai kuwa, dakika chache kabla ya shehe huyo hajapatwa na mauti alionekana ni mwenye afya njema huku akitoa Neno la Mungu ambalo kila mtu aliyekuwa eneo hilo la makaburi lilimgusa na kujitafakari upya njia zake, alisema:

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abasi Kandolo akiwa kwenye mazishi.
“Kila nafsi lazima itaonja mauti na si ajabu hata mimi  ninayeongea wakati huu naweza kufa wakati wowote ule baada ya kumaliza mazungumzo haya mbele ya macho yenu sasa hivi.”
KUANGUKA
Mashuhuda wanasema kweli kifo kiko mwilini mwa mtu kwani mara baada ya kumaliza kusema maneno hayo, Shehe Mketo aliyesifika kwa uadilifu  alianguka chini ghafla na hapo hekaheka zikaanza, watu wakiulizana ‘jamani nini kimetokea, jamani nini kimetokea?’
AKIMBIZWA HOSPITALI KUMBE TAYARI
Baadhi ya watu walimbeba shehe huyo huku wakimpepea na kumwingiza kwenye gari kisha kumkumbiza Hospitali ya Rufaa ya Mbeya ambako madaktari baada ya kumpokea walisema shehe huyo tayari alikuwa ni marehemu.
MSIBA WAKE
Shehe aliyekuwa akitoa mawaidha wakati wa mazishi sasa ukawekwa msiba wake, watu wakaanza kuomboleza nyumbani kwake Soko Matola jijini hapa ambako pia msiba wa Bibi Majuto ulikuwepo huku kila mmoja akiuliza nini kilimpata mtumishi huyo wa Mungu mpaka akapoteza maisha baada ya kauli yenye mwashirio wa tukio hilo?
Shehe mwenzake akilia kwa uchungu.
MAZISHI YAKE PALEPALE
Kesho yake, mchana shehe huyo ambaye saa ishirini na nne nyuma alikuwa hai, alizikwa kwenye makaburi yaleyale aliyotolea mawaidha ya Bibi Majuto ambapo kaburi lake limepakana na la bibi huyo.
KAULI ZA MASHEHE
Mashehe mbalimbali waliohudhuria mazishi hayo walisema kifo cha mwenzao kinafundisha waumini kujiandaa na safari ya kifo ambacho kinaweza kutokea wakati  wowote bila kutarajia.
Shehe wa Msikiti wa Isanga, Ibrahim Bombo yeye alisema: “Tukio hili ni dalili pekee ambazo zinapaswa kuwafundisha waumini wa Kiislam kujiandaa kwa kufanya matendo mema kwa kuwa kifo kinaweza kumkuta binadamu mahala popote.
Waombolezaji wakizika.
“Tujiwekee maandalizi ya safari ya akhera, hakuna anayejua saa wala tarehe ya kuondoka kwake duniani, kifo cha shehe wetu kitupe mafundisho.”CHA AJABU SASA
Cha ajabu sasa, wakati shehe huyo anasema hayo, baadhi ya waombolezaji walimtolea macho pima, huenda waliamini kitampata kilichompata marehemu!

KAULI YA MKUU WA MKOA
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro aliwataka ndugu, jamaa, marafiki na waumini kutohusisha kifo hicho na imani zozote za kishirikina bali waamini kuwa kimetokana na mipango ya Mungu kwa vile kila mtu ataondoka duniani kwa njia zake.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate