EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, April 22, 2015

HIVI WASANII MTAKUWA NA UCHUMBA‭, ‬NDOA ZA MAIGIZO MPAKA LINI‭?‬


Kwenu mastaa wa tasnia mbalimbali Bongo‭, ‬habari zenu bwana‭. ‬Poleni na majukumu ya kila siku ya kulijenga taifa‭.‬
Mkitaka kujua afya yangu‭, ‬mimi ni mzima‭, ‬namshukuru Mungu naendelea kutimiza majukumu yangu‭, ‬likiwemo hili la kuwaandikia barua‭.‬
Nimewakumbuka leo kupitia barua‭, ‬nataka kuwaambia kwamba mimi pamoja na mashabiki wengine wa sanaa yenu tumewachoka‭. ‬Tumechoka kuona na kusikia kila siku mkifanya maigizo kwenye maisha yenu halisi‭.‬
Hivi ni kwa nini kila kukicha tunasikia mnaachana‭? ‬Kwa nini hamdumu kwenye uhusiano wa mapenzi‭? ‬Kwa nini hamdumu kwenye ndoa kama mashabiki wenu wanavyowategemea‭?‬
Penzi linapoanza kushamiri‭, ‬mnalinadi kwenye mitandao na vyombo vya habari‭. ‬Mnawaaminisha mashabiki wenu kuwa mnapendana kwa kauli zenu motomoto lakini ndani ya miezi miwili mitatu penzi chali‭.‬Wengine mnaonesha kwamba mmedhamiria na kuamua kufunga ndoa kabisa‭, ‬lakini kumbe moyoni bado mnakuwa mna lenu jambo‭. ‬Mashabiki wenu wanafurahia kuona mmeoana lakini ndoa nayo haidumu‭, ‬mnaachana‭.‬
Mbaya zaidi mnapoachana mnapeana maneno ya kashfa‭, ‬mnaumbuana kiasi ambacho kinadhihirisha kabisa mlikuwa hamna mapenzi ya dhati‭ ‬au hamkudhamiria kabisa kuingia kwenye ndoa‭.‬Hivi kama kweli mlipendana‭, ‬nini kinawafanya muanze kuumbuana‭? ‬Badilikeni‭, ‬mashabiki wenu wamechoka kusikia kila kukicha ndoa ya‭ ‬staa fulani imevunjika‭, ‬wachumba fulani wameachana‭, ‬ni aibu‭.‬
Watu hawapendi kuona Nay wa Mitego na Siwema mkiwa mmeachana‭. ‬Tena mnaachana kwa kupeana maneno yanayoonesha kwamba mlikuwa hamna nia ya dhati ya kuwa wapenzi‭.‬Shamsa Ford na Dick‭, ‬kapo yenu ilikuwa nzuri‭. ‬Mlipamba vyombo vya habari‭, ‬uhusiano wenu ukazaa matunda ya mtoto mmoja lakini ndoto ya kuishi kama mume na mke imeyeyuka‭.‬
Nasibu Abdul‭ ‬‮!‬٪Diamond‮!&‬‭ ‬na Wema Sepetu penzi lenu lilikuwa likipendwa‭  ‬na wengi‭, ‬likaishia njiani‭. ‬Rose Ndauka na Malick Bandawe mlioishi na kubahatika kupata mtoto mmoja‭, ‬nini kiliwakuta‭? ‬Inasikitisha‭.‬Wolper na Dallas nao walipamba sana vyombo vya habari lakini mwisho wa siku chali‭. ‬Ndugu zangu‭, ‬mnapaswa kubadilika‭. ‬Msiigize maisha yenu‭. ‬Igizeni kwenye filamu‭, ‬mkirudi nyumbani mjitambue kwamba heshima‭, ‬upendo‭, ‬busara vinahitajika ili kuishi na mwenzako‭.‬
Mbona wapo wasanii wengi tu maarufu duniani na wamedumu kwenye uhusiano‭? ‬Kwa nini msiige mfano kwa mastaa kama Marlaw na mkewe‭, ‬Jay Z na Beyonce ambao wanaheshimu penzi lao hadi sasa‭?‬Jamani‭, ‬cha msingi mnapaswa kuheshimu suala la uhusiano‭, ‬msifanye masihara katika maisha ya ukweli‭.  ‬Vitu vingine vinapaswa kufanyika kwenye filamu pekee na siyo kuvihamishia katika maisha halisi‭.‬
Bila shaka mtakuwa mmenielewa na mtabadilika‭, ‬kila la kheri‭.‬

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate