EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 13, 2015

Yanga wamtwisha zigo Magufuli

Mgombea wa urais kupitia chama kikongwe nchini cha CCM, Dk John Pombe Magufuli.
Sweetbert Lukonge na Nicodemus Jonas
SIKU moja tu baada ya kuibuka na ushindi wa kishindo na kupata nafasi ya mgombea wa urais kupitia chama kikongwe nchini cha CCM, Dk John Pombe Magufuli, tayari ameshauriwa mambo kadhaa kama moja ya mizigo anayotakiwa kuipatia ufumbuzi akishinda kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Magufuli alipata kura 2,104 ambazo ni 87% ya kura 2,422 zilizopigwa na kuwa ni dalili nzuri kwamba hata kwenye uchaguzi mkuu Oktoba atafanya vema.
Kitendo hicho cha urais kunukia kwake, kumeifanya klabu kongwe ya soka nchini, Yanga, kuwa ya kwanza kupitia Katibu Mkuu wake, Dk Jonas Tiboroha, kumpa Magufuli, mzigo wa kuufanyia kazi.
Lakini Simba na baadaye Azam FC ambazo ndizo klabu kubwa zinazochuana sasa katika kipindi hiki, nazo zikatoa yao kwa Magufuli.
Yanga:
Akizungumza na Championi Jumatatu, Dk Tiboroha alisema furaha yake ni kusikia kupitishwa kwa mtu mpenda michezo tangu akiwa masomoni.
“Uzuri ninamfahamu vizuri, Magufuli ni mwanamichezo mwenzetu. Nilimfahamu tangu nikiwa masomoni pale chuoni (Chuo Kikuu Dar es Salaam-UDSM), kila siku alikuwa akifanya mazoezi ya kukimbia. Hivyo ni furaha kwetu kwa watu wa soka na anatakiwa kuanzia pale alipoishia Rais Kikwete,” alisema Dk Tiboroha.

“Akishinda, tunaomba serikali yake itambue kuwa changamoto kubwa kwenye soka letu ni suala la udhamini. Hivyo iwe tayari kushawishi makampuni makubwa ili yawekeze kwenye soka letu.
“Ligi kubwa zote zimeendelea kutokana na kuwa na udhamini mkubwa na wa kutosha, hivyo ili na sisi tuweze kufanya vizuri lazima tupate udhamini.
“Lakini pia ni lazima atambue kuwa soka kwa sasa ni ajira hususan kwa vijana, hivyo ni lazima sekta hii ipewe kipaumbele kama moja ya sekta ya kutoa ajira kwa vijana,” aliongeza Dk Tiboroha.
Simba:
Kwa upande wa Simba, Makamu wa Rais, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ amesema kuwa uteuzi huo wa Magufuli una faida kubwa katika medani ya soka.
“Mimi ni CCM damu, lakini nawapongeza sana CCM kwa hatua hiyo ya kumteua Magufuli kuwa mgombea wa nafasi ya urais wa nchi yetu, hakika hawajakosea kumpatia nafasi hiyo.
“Akifanikiwa kushinda aangalie mambo yafuatayo kwa ajili maendeleo ya michezo hapa nchini, hususan soka kwani tumechoka kuwa wasindikizaji kila wakati.
“Kwa kushirikiana na TFF, serikali yake iwe na mipango madhubuti ya kutengeneza wachezaji kuanzia ngazi ya chini kabisa kama yafanyavyo mataifa mengine.
“Lakini pia anatakiwa kuhakikisha kunakuwa na uwekezaji wa hali ya juu kwa kuwa na miundo mbinu mizuri ya mchezo, ukiangalia kwa asilimia kubwa viwanja vingi hapa nchini siyo vizuri, ni vibovu, hivyo ni matumaini yangu kuwa hilo ataliangalia.
“Mbali na hayo, pia timu za taifa anatakiwa kuziangalia kwa jicho la pekee, vizuri atenge bajeti kwa timu hizo, pia klabu zinazowakilisha Tanzania kimataifa.”
Azam FC:
Naye, Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba, amesema: “Vipo vingi vya kuboresha lakini aanze na suala la viwanja vya soka, vipo vingi ambavyo vinamilikiwa na CCM na serikali lakini havitumiki ipasavyo au vimesahaulika kwa hiyo ni vema kwanza vikaanza kuboreshwa hasa sehemu za kuchezea ‘pitch’.
“Anatakiwa pia kuhimiza na kuangalia makampuni makubwa yanayoweza kuwekeza kwenye soka kwa ajili ya kufika mbali kupitia kwa watu hao wenye uwezo mkubwa wa udhamini.
“Kingine ni kuhusu kuthaminika kwa wachezaji wetu, kwanza ieleweke kuwa soka ni ajira na iwekewe mkazo ikiwemo hata kima cha chini cha mshahara wa mchezaji kiwe wazi na itambulike ni ajira kama nyingine.”

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate