EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA
Showing posts with label FLORA MBASHA. Show all posts
Showing posts with label FLORA MBASHA. Show all posts

Wednesday, February 18, 2015

MTOTO WA FLORA JIPU PWAA!

Stori: Richard Bukos na Issa Mnally/Risasi Mchanganyiko
BAADA ya utata wa uhalali wa baba wa mtoto wa Mwimba Injili maarufu Bongo, Flora Mbasha kutawala kwenye magazeti mbalimbali na mitandao ya kijamii, hatimaye jipu limepasuka baada ya baba mdogo wa Flora, aliyejitambulisha kwa jina moja la Kisekwa kufunguka kwamba mtoto huyo ni damu halali ya Mbasha, Risasi Mchanganyiko lina kauli yake kuthibitisha hilo. 
Mwimba Injili maarufu Bongo, Flora Mbasha.
NI MAHAKAMA YA ILALA
Kisekwa alifunguka hayo juzikati katika Mahakama ya Ilala jijini Dar alipokuwa amekwenda kusikiliza kesi ya aliyekuwa mume wa Flora, Emmanuel Mbasha kudaiwa kumbaka shemeji yake ambapo alisema anamshangaa Mbasha kushindwa kukiri ukweli ulio wazi kwamba mtoto ni damu yake wakati moyoni anautambua.
TUJIUNGE NA KISEKWA
“Inakuwaje Mbasha anashindwa kukubali ukweli kwamba mtoto ni wake wakati anatambua fika kwamba ujauzito ni mali yake kabla hata ya mgogoro wao? Ndugu wote tulikuwa tunajua hilo, upande wetu na hata kwao. Mbona hakuikataa tangu kipindi hicho?
Aliyekuwa mume wa Flora Mbasha, Emmanuel Mbasha.
Mgogoro wao ulikuwa wa mambo ya kawaida ya kifamilia, haukuhusiana hata kidogo na Flora kuchepuka wala nini, tangu mwanzoni mwa mgogoro wao wakiwa wanaishi pamoja wameshaitwa mara tatu katika ofisi za Ustawi wa Jamii na alielezwa kuwa mkewe ni mjamzito, akifahamu ni mali yake na akaonywa kuwa kitendo cha kuendekeza migogoro ya mara kwa mara kinaweza kumletea matatizo mkewe na kichanga kilichokuwa tumboni, mbona hakubisha? Tulikuwa tukijadili matatizo yao na kila mmoja kuweka hoja zake mezani, hakuna kati yao aliyehusisha mgogoro huo na suala la kuchepuka,” alisema Kisekwa.

Monday, February 9, 2015

FAMILIA YA MBASHA KIKAO KIZITO DAR

Stori: Waandishi Wetu/Ijumaa Wikienda
SIKU chache baada ya kuibuka utata mkubwa juu ya kichanga cha kike cha mwimba Injili maarufu Bongo, Flora Mbasha huku mitandao ya kijamii ikieleza kwamba baba wa mtoto huyo si aliyekuwa mume wa mwanamuziki huyo, Emmanuel Mbasha ‘Ima’, familia ya mwanaume huyo inadaiwa kufanya kikao kizito jijini Dar ili kupata ufumbuzi, Ijumaa Wikienda linakujuza.
Mwimba Injili maarufu Bongo, Flora Mbasha akiwa amejifungua kitoto kichanga Hospitalini.
Kwa mujibu wa chanzo makini kilicho karibu na familia ya Mbasha, familia hiyo ilikutana Jumamosi iliyopita nyumbani kwa Ima, Tabata-Kimanga, Dar ili kulizungumza suala hilo na kuona kama wanaweza kukubaliana kukilea kichanga hicho endapo ni damu yao.
“Ndugu walitofautiana, kila mtu alikuwa na mtazamo wake hivyo wakaona bora wakutane na kutafuta jibu la pamoja kama wanalea au hawalei,” kilisema chanzo hicho.
KIKAO CHAVUNJIKA
Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kuwa, kikao hicho hakikufikia muafaka kutokana ndugu hao kutofautiana kimisimamo kwani kila mmoja alitoa mawazo yake.
Mwimba Injili huyo, Flora Mbasha anayedaiwa kuzaa kitoto kichanga nje ya ndoa.
MBASHA ANASEMAJE?
Alipotafutwa Mbasha ambaye sasa anatamba na Wimbo wa Haribu Mipango ya Shetani ambao inadaiwa amekuwa akiutumia kama kijembe kwa Flora, alisema aachwe kwanza kwani suala hilo linamuumiza kichwa na ni la  kifamilia zaidi.

Thursday, July 3, 2014

MBASHA AMSHITAKI GWAJIMA

stori: Waandishi Wetu
Mambo juu ya mambo! mvumo mkali wenye kuogofya unaendelea kutamalaki katika ndoa ya wanamuziki zao la upako wa Injili Bongo, Emmanuel na Flora Mbasha, safari hii ‘topiki’ siyo zile tuhuma za ubakaji zilizopo mahakamani.
Wanamuziki zao la upako wa Injili Bongo, Emmanuel na Flora Mbasha,
Mbeba ‘niuzi’ wa awamu hii ni Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, baada ya Mbasha kuona isiwe tabu, hivyo kuamua kupambana na mtumishi huyo wa Mungu kwa njia ya kiroho zaidi.

Thursday, June 26, 2014

FLORA AKOMBA KILA KITU


Stori: Waandishi Wetu
MACHOZI upya! Habari halali kwa ubongo wako zinaeleza kwamba wakati mumewe, Emmanuel Mbasha (32) alipokuwa mahabusu, Dar kati ya Juni 15 hadi 17, mwaka huu, staa wa Gospo Bongo, Flora Mbasha (31) anadaiwa kwenda nyumbani na kukomba vitu vya ndani kuvipeleka kusikojulikana.
Sehemu ya chumba cha kupumzikia kilichobakiwa na kochi na zulia.
Ilisemekana kwamba wakati hayo yakiendelea, Mbasha alikuwa nyuma ya nondo za Mahabusu ya Keko jijini Dar es Salaam ambako alishikiliwa.
Kwa mujibu wa mtu aliyeambatana na Mbasha alipopata dhamana dhidi ya kesi yake inayomkabili ya ubakaji wa shemejiye mwenye umri wa miaka 17, alipofika nyumbani kwake Tabata-Kimanga, Dar alipigwa butwaa kukuta hakuna vitu ndani!
Chumba kingine kilichosafishwa kabisa bila ya samani yoyote.
Habari zilidai kwamba alipowauliza majirani kama walimuona mtu akiingia ndani walimwambia mkewe (Flora) ndiye alikuwa akiingia na kutoka mara kwa mara.
Ilielezwa kuwa vitu hivyo vilihamishwa Juni 16 ambapo Mbasha alitoka mahabusu Juni 17, yaani siku moja tu.

Monday, June 23, 2014

EMMANUEL MBASHA ALIZWA HATI ZA NYUMBA, VIWANJA


MAJANGA! Siku chache baada ya kuachiwa kwa dhamana katika kesi ya kudaiwa kumbaka shemejiye, mwimbaji wa Injili na mfanyabiashara Bongo, Emmanuel Mbasha amedaiwa kuibiwa hati za nyumba na viwanja.
Mfanyabiashara Bongo, Emmanuel Mbasha mume wa Flora Mbasha.
Chanzo makini kilichomo ndani ya familia, kimedai kuwa mara baada ya Mbasha kujitokeza na kuwekwa mahabusu Juni 17, mwaka huu, mtu asiyejulikana alikwenda nyumbani kwa mfanyabiashara huyo, Tabata-Kimanga, Dar na kukwapua hati za nyumba na viwanja mbalimbali anavyovimiliki.

Saturday, June 21, 2014

WAKATI MBASHA AKIWA HURU KWA DHAMANA, GWAJIMA APASUA JIPU!

Stori: Haruni Sanchawa na Richard Bukos
WAKATI mume wa mwimba Injili Bongo,  Flora Mbasha, Emmanuel Mbasha akiachiwa huru kwa dhamana kufuatia kesi ya kudaiwa kumbaka shemejiye, Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima la jijini Dar es Salaam, Josephat Gwajima ameibuka na kunena mazito kuhusiana na sakata hilo, Risasi Jumamosi limesheheni mkobani.
Mbasha akiwa na Pingu.
Mbasha aliachiwa kwa dhamana juzi akitokea Gereza la Keko, Dar baada ya kupandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Juni 17, mwaka huu na kusomewa mashitaka mawili ya ubakaji ambayo hata hivyo, aliyakana.
Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima la jijini Dar es Salaam, Josephat Gwajima.
ILIVYOKUWA KORTINI
Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, mheshimiwa Wilbeforce Luago siku hiyo ya Juni 17, alitoa hoja kwamba upande wa jamhuri hauna pingamizi hivyo dhamana ipo wazi.

Monday, June 24, 2013

FLORA MBASHA; SALUTI MIAKA 11 YA NDOA BILA 'KIKOHOZI'.


Makala: Sifael Paul na Mitandao
FLORA Mbasha ni mwimba Injili Bongo mwenye ‘profaili’ kubwa ndani na nje ya Tanzania. Kama ulikuwa hujui, ni mmoja wa mastaa wengi wakubwa wa ‘gospo’ watakaoshusha upako kwenye Tamasha la Matumaini litakalofanyika katika Uwanja wa Taifa, Dar, Julai 7, mwaka huu.
Flora alizaliwa jijini Mwanza mwaka 1983 katika familia ya Dini ya Kikristo. Ni mtoto wa pili kwenye familia ya Henry Mayallah na Caroline Moses Kulola.
Alimpoteza baba yake mwaka 1998. Kwa wakati huo walikuwa wakiishi jijini Arusha, akamwacha Flora na nduguze Benjamin na Dorcus.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate