EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA
Showing posts with label Zari. Show all posts
Showing posts with label Zari. Show all posts

Saturday, July 25, 2015

Utata mpya mtoto wa Diamond!

Diamond-Platnumz-na-Zari
Staa wa Bongo Fleva,  Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’,  akiwa katika pozi na mpenzi wake Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.
MUSA MATEJA
Utata mpya umeibuka wakati mama kijacho wa staa wa Bongo Fleva,  Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’,  akitarajiwa kujifungua muda wowote kutoka sasa, ishu ni juu ya uraia wa mtoto atakayezaliwa.
TUJIUNGE NA MTU WA NDANI
Habari kutoka kwa mtu wa ndani wa familia hiyo zilidai kwamba, utata umezidi kuigubika familia hiyo kwa kile kinachodaiwa kuwa ndugu wa pande zote kuendelea kuvutana juu ya Zari ajifungulie nchi gani kati ya Tanzania, Uganda na Afrika Kusini ‘Sauz’.
DIAMONDZARI.jpg
Utata huo umevuja wakati paparazi wetu akiwa katika mishemishe za kutaka kujua Zari alipo kwa sasa na atajifungulia katika hospitali ipi ndipo alipopenyezewa ‘ubuyu’ kwamba hadi sasa kuna utata mkubwa katika familia hiyo.
MABISHANO YA URAIA
Chanzo kilimweleza mwanahabari wetu kuwa, kikubwa ni mabishano ya uraia na sehemu sahihi ya kujifungulia mtoto huyo.
Kilidai kwamba, suala hilo limekuja kufuatia ndugu wa Zari kutaka ajifungulie Sauz jambo ambalo Diamond na familia yake wamekuwa wakilipinga vikali.
ZARINADIAMOND4.jpg
ZARI NJIA PANDA
Ilisemekana kwamba, kwa upande wake Zari amekuwa njia panda kutokana na shinikizo hilo huku mama Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ naye akisisitiza kuwa lazima Zari ajifungulie Bongo ili amuhudumie mkwe wake huyo.
“Yaani ndugu wa Zari wanampa Diamond wakati mgumu sana kutokana na kuendelea kung’ang’ania Zari akajifungulie kwao (Sauz ambako kuna ndugu wengi) wakati furaha ya Diamond ni kuona mtoto akizaliwa Bongo.

Wednesday, June 24, 2015

DOKTA FADHILI AMPA ZAWADI ZARI


DOKTA FADHILI AMZAWADIA ZARI BAISKELI (2) Mpenzi wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.
Mwandishi wetu
DAKTARI wa Kitengo cha Sayansi na Tiba Asili kilichopo Mbezi-Afrikana, Dokta Fadhili Emily, amemnunulia baiskeli ya kubebea mtoto, mpenzi wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kama zawadi pindi atakapojifungua.
DOKTA FADHILI AMZAWADIA ZARI BAISKELI (2)Mfano wa baiskeli aliyitoa Dkt. Fadhili kwa Zari.
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko akiwa nchini Sweden alikoenda kwa ziara binafsi, Dokta Fadhili alisema kwa kutambua yeye ni mtu wa Kigoma anakotokea Diamond, ameona amnunulie shemeji yake huyo baiskeli hiyo ambayo kwa mujibu wake, ina thamani ya shilingi milioni 5 za Kitanzania.
DOKTA FADHILI AMZAWADIA ZARI BAISKELIDkt. Fadhili Emily.
“Mimi ni mwenyeji wa Kigoma, Zari ni shemeji yangu hivyo nikiwa huku Sweden nimeona niwawakilishe vijana wote wa kule kwa kumnunulia baiskeli hii ya kisasa shemeji yetu, wanatumia wanawake wengi Ulaya kubebea watoto wao,” alisema.
Zari anatarajiwa kujifungua kati ya Agosti au Septemba, mwaka huu ambapo ujio wa mtoto huyo umekuwa ukitengeneza vichwa vya habari kila kukicha.

Wednesday, March 11, 2015

DIAMOND APATA MSHTUKO DENI LA MIL.800

Musa Mateja/mchanganyiko MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amepatwa na mshtuko mkubwa baada ya kuwepo madai ya kudaiwa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 800 na serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Risasi Mchanganyiko linakupa mchapo kamili.
Msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
ILIKUWAJE?
Mwishoni mwa wiki iliyopita, barua inayodaiwa kuandikwa na mamlaka hiyo halali ya serikali, ilisambazwa mitandaoni, ikielezwa kuwa ilikuwa imetumwa kwa meneja wa msanii huyo ambaye kwa sasa ndiye yupo juu, ikimtaka kupeleka nakala za mikataba yote ya muziki aliyoingia kwa ajili ya kufanya shoo, kuanzia mwaka 2010 hadi sasa.

GUMZO MITANDAONI
Baada ya kuwekwa kwa barua hiyo mitandaoni, watu mbalimbali walitoa maoni yao walionyesha hisia tofauti, baadhi wakipinga kwa madai kuwa wanamuonea huku wengine wakisema siyo Diamond tu, bali wasanii wote wanastahili kulipa kodi kutokana na mapato wanayopata kupitia kazi zao.

KODI ZIPOJE KIBONGOBONGO?
Mtaalam mmoja wa mambo ya kodi aliyezungumza na Risasi Mchanganyiko, alisema kwa mujibu wa taratibu zao, msanii huyo anastahili kulipa kodi kiasi cha asilimia kumi ya fedha anazopata katika kila mkataba anaoingia.

“Kuna walipa kodi wengine kama wafanyabiashara, hawa wanalipa kile ambacho kitaalamu kinajulikana kama Capital Gain, yaani kulipa kadiri unavyopata. Mtu anakwenda TRA mwenyewe na kueleza mapato yake na mamlaka itampangia kiasi cha kulipa. Ila watu kama wasanii na wengine wanaolipwa, wanatakiwa kutoa asilimia kumi ya malipo,” alisema mtaalam huyo aliyekataa kutajwa jina gazetini.
DIAMOND ANADAIWA SH. NGAPI?
Kama suala hilo litafanyika kwa mujibu wa mtaalam huyo, Diamond ambaye malipo yake kwa shoo moja yanatajwa kuwa ni shilingi milioni 20 kwa sasa, atatakiwa kulipa kiasi kinachozidi milioni 800 kutokana na hesabu zilizofanywa na watu wanaofuatilia muziki wake.

Thursday, February 5, 2015

KITUMBO CHA ZARI KIMEMFURAHISHA MAMA WEMA!

Stori: Imelda Mtema/Amani
SIKU chache baada ya Nasibu Abdul ‘Diamond’ kuweka picha zinazomuonesha mpenzi wake wa sasa Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ akiwa na kitumbo kinachoashiria kukua kwa ujauzito, mama mzazi wa zilipendwa wa Diamond, Wema Sepetu ‘Madam’, Mariam Sepetu amefunguka kuwa amefurahia tukio hilo.
Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’ akiwa na mpenzi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Mzazi huyo ambaye ni fundi wa kuzungumza, alisema tukio hilo limemfurahisha kwani anaamini ndoto za Diamond kurudiana na binti yake zitakuwa zimeyeyuka rasmi kama alivyokuwa akimuomba Mungu siku zote.
Kuonesha kwamba amefurahishwa na kitendo hicho, alimtaka Zari aendelee kumpenda Diamond, amgande kila idara ili isije kutokea akarudi kwa binti yake ambaye walimwagana mwishoni mwa mwaka jana.
“Yaani kama inawezekana naomba sana huyo Zari azidi kumganda Diamond, asimpe muda wa kugeuka nyuma kabisa ili mambo mengine yaendelee kwa sababu uhusiano wa Diamond na mwanangu haukuwa na baraka zangu,” alisema mama Wema.
Mama Sepetu aliongeza kuwa, hana maana ya kumchagulia mchumba mwanaye bali anahitaji mwanaume yeyote mwenye heshima na anayejiheshimu kwa sababu mwanaume asiyejitambua hawezi kuwa baba bora wa familia.

Monday, January 19, 2015

MUME: ZARI HAWEZI KUZAA NA DIAMOND

Stori: Kampala, Uganda
Oohoo! Wakati staa mkubwa wa muziki wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akichekelea kitendo cha mpenzi wake wa sasa, Zarinah Hassan ‘Zari’ au ‘The Boss Lady’ kunasa mimba yake, habari ya mjini huko Kampala, Uganda ni juu ya aliyekuwa mume wa mwanamama huyo, Ivan Ssemwanga kufunguka na kusema: “Naapa Zari hawezi kuzaa na Diamond.”
Staa mkubwa wa muziki wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na Zarinah Hassan,  'Zari'.
HABARI YA MJINI
Wikiendi iliyopita, vyombo vya habari na mitandao nchini Uganda ambako kuna makazi mengine ya Zari mbali na Afrika Kusini, kulipambwa na habari hizo baada ya mwanaume huyo aliyezaa na mwanamama huyo watoto watatu kuanika siri nzito juu ya ishu hiyo.
‘Ubuyu’ huo ulidadavua kwamba, kwanza jamaa huyo mwenye utajiri wa kutupwa alianza kwa kuelezea namna alivyoshtuka aliposikia Zari ni mjamzito.

Saturday, January 17, 2015

SHABIKI ZARI KUWA NA UJAUZITO, INA MAANA DIAMOND NA ZARI WALIFANYA NGONO BILA KINGA,WALIPIMA NA WALIJUANA KWA MUDA GANI ?

zari 56

Kupitia info za mashabiki wa sammisago.com, Shabiki wa Diamond ametuma mtazamo wake kuhusu issue ya Diamond na Zari kutegemea mtoto na kusema.
 
Sijawahi kuona mastaa hawa wakiwa hospitalini au kwenye kituo chochote wakipima afya zao, ukizingatia ni watu wakuweka hadharani mambo yao yote basi hata kupima wangeweka instagram au huko twitter

Ni vizuri staa kuzaa na staa mwenzake ila Diamond ana muda wa kuwa baba? mahusiano yake mengi ni kiki au drama a,bazo hata Kwa Zari tuliyedhani itakuwa tofauti kumbe ni yale yale, mimi ni shabiki tu ila nawatakia kila la heri kwenye familia yao wanayoanzisha
Shabiki alimaliza hivyo.Upi mtazamo wa juu comment za huyu shabiki ?

Friday, January 9, 2015

KISA ZARI DIAMOND AITWA SHOGA

HII ni ‘bad news’ kwa staa namba moja wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’. Mfanyabiashara maarufu nchini Uganda anayefahamika kwa jina la King Lawrence, ameibuka na kumuita nyota huyo shoga.
Staa namba moja wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na Zarinah Hassan ‘Zari’.
ISHU ILIPOIBUKIA
King ambaye ana makazi yake pia nchini Afrika Kusini, amedaiwa kutoa kauli hiyo juzi, Jumatano kupitia mtandao wa Facebook akionesha kukerwa na kitendo cha staa wa muziki Uganda, Zarinah Hassan ‘Zari’ kuangukia katika penzi la Diamond.
ATUMIA GIA YA WATOTO
Awali, King ambaye imeelezwa alikuwa na urafiki na dereva wa aliyekuwa mume wa Zari, Ivan Semwanga, alianza kwa kumchokonoa Diamond kwa gia ya kujifanya anawatetea watoto wa Zari ambapo alitupia picha ya Zari akiwa na Diamond mtandaoni ikiwa na ujumbe wenye kejeli na jeuri ya fedha.
UJUMBE ULIVYOSOMEKA
“As a concerned uncle, Im offering Zari’s tomboy Diamond Dola 40,000 so as to leave the old mom of three to take care of her kids. The young boys miss their mom. Please Diamond do it for the kids.”
(Nikiwa kama mjomba, ninampa jikedume wa Zari, Diamond, Dola 40, 000 (Sh. Mil 66) ili amuache mama wa watoto watatu (Zari) awalee vizuri watoto wake. Watoto wanammisi mama yao.”
Diamond Platnumz na Zari wakidendeka.
ABADILISHA GIA
Kuonesha ana mpango mchafu wa kumchafua Diamond ambaye anaipeperusha vyema bendera ya Afrika kimuziki, badala ya ishu ya watoto, alibadili upepo na kujinadi eti yeye ndiye wa kwanza kutembea na Zari.
Pasipo kueleweka kusudi lake, alimpiga dongo Diamond ambaye usiku wa kuamkia leo alipewa heshima ya kipekee kutumbuiza kwenye Tuzo za Wanamichezo Bora zilizoandaliwa na Shirikisho la Afrika (Caf) nchini Nigeria.

Monday, December 22, 2014

DIAMOND, ZARI PROJEKTI YANOGA!

Acha muvi iendelee! Ile projekti ya mastaa wakubwa Afrika Mashariki, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Zarinah Hassan ‘Zari’ sasa imenoga.
Mastaa wakubwa Afrika Mashariki, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Zarinah Hassan ‘Zari’wakila ujana.
Habari zinaeleza kwamba katika pati ya mwaka ya Zari wiki iliyopita iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Guvnor uliopo Kampala, Uganda mwanadada huyo hakuishia kwenye pati tu bali alitumia nafasi hiyo kumtambulisha Diamond aliyekuwa mgeni rasmi kuwa kwa sasa wao ni wapenzi.
‘Diamond Platnumz’ na Zarinah Hassan ‘Zari’ wakifanya yao.
Mbali na mahaba niue waliyooneshana mbele za watu, wawili hao walitumia chansi hiyo ‘kudendeka’ mbele ya kamera hivyo kudhihirisha kwamba mambo yao yapo juu ya mstari.

Saturday, December 20, 2014

ZARI, DIAMOND MAHABA KWEUPE UGANDA

STAA anayetamba na ngoma mpya ya Nitampata Wapi, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na mtoto mzuri kutoka Uganda, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’ wameoneshana malovee hadharani na kuwaacha watu midomo wazi.
Nasibu Abdul ‘Diamond’akiwa kwenye pozi na mtoto mzuri kutoka Uganda, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’.
Tukio hilo lililoacha historia ya aina yake kwa kutokana na umaarufu wa wawili hao, lilitokea Jumatano iliyopita, nchini Uganda wakati Zari alipokwenda kumpokea Diamond katika Uwanja wa Ndege wa Kampala nchini humo.‘Zari The Boss Lady ‘Diamond wakipata ukodaki.
Kwa mujibu wa chanzo kilichoambatana na Diamond, Zari alimpokea mgeni wake kwa mabusu motomoto na msafara wa kwenda hotelini ulipoanza, walipewa ulinzi mzito hadi hotelini ambako kila wakati wawili hao walipeana mabusu ya kiaina kuonesha ‘wamemisiana’.

Friday, December 19, 2014

DIAMOND, ZARI WAFUNIKA ALLWHITE CIROCPARTY ILIYOFANYIKA KAMPALA UGANDA


Mfanyabiashara mrembo na muimbaji wa Uganda, Zarinah Hassan 'Zari'  au 'The Boss Lady' akiwekwa sawa kabla ya shoo yake ya All White Ciroc party iliyofanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa Guvnor nchini Uganda.
 
Staa wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul 'Diamond Platnumz' (kulia) akiwa na Zari au 'The Boss Lady' kabla ya kuelekea katika shoo.
 
The Boss Lady akiwa katika pozi.

Thursday, December 18, 2014

ZARI AMPOKEA DIAMOND KWA SHANGWE UGANDA JANA

STAA wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul 'Diamond Platnumz' akiwa na mfanyabiashara mrembo na muimbaji wa Uganda,Zarinah Hassan 'Zari'  au 'The Boss Lady' baada ya kuwasili Uganda jana.
Diamond Platnumz akiwa na Zari the Boss Lady wakiondoka Uwanja wa Ndege wa Uganda.

Wednesday, December 3, 2014

MTUNGO WA ZARI BALAA! DIAMOND NI WA 13!

Ingawa mwenyewe amekuwa akikanusha kila kukicha, mrembo tajiri mwenye maskani yake nchi jirani ya Uganda na Afrika Kusini, Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady, anadaiwa kuwa na mtungo mrefu wa wanaume ambapo kama ni kweli anatoka na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ basi jamaa huyo atakuwa anashika nambari 13.
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na  Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady.
Kwa mujibu wa jarida la linalodili na habari za showbiz (biashara ya shoo) la E-Vibe la nchini Uganda la hivi karibuni, Zari ambaye wikiendi iliyopita alimng’arisha Diamond katika zulia jekundu kwenye Tuzo za Channel O (Choamva) zilizofanyika Johannesburg nchini Afrika Kusini ‘Sauz’, anadaiwa kuwa ‘klozi’ na idadi hiyo ndefu ya wanaume.

Zari akiwa amebeba tuzo za Diamond nchini Afrika Kusini.
Jarida hilo lilieleza kwamba ndani ya kipindi cha miaka 14 baada ya kutimiza umri wa mtu mzima wa miaka 18, Zari mwenye umri wa miaka 32 sasa, ameshajiachia na wanaume wa kada mbalimbali wakiwemo vigogo serikalini, wafanyabiashara, mastaa wa tasnia mbalimbali na hata vijana wadogo.
MABUSU
Kabla ya Diamond, picha za Zari zilivuja akiwa anabusiana kwa hisia na mwanaume, Farouk Sempala anayesifika kwa dili za mjini. Mara nyingi, Zari amekuwa akishangaza watu na kuacha maswali kuwa nini huwa kinamsukuma kumzoea mwanaume haraka na kuingia naye kwenye urafiki?
Zari au The Boss Lady akiwa na aliyekuwa mumewe Ivan Semwanga.
Kwa mujibu wa jarida hilo, kuna mtandao maalum wa kundi la watu uliundwa kwa ajili ya kufuatilia nyenendo za Zari katika sekta ya mapenzi ndipo data zikamwagwa.

Monday, December 1, 2014

DIAMOND, MAMA’KE, ZARI WALA BATA SAUZ

GOOD time! Katika hali ya kushangaza, mkali wao ndani ya Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, mama’ke (Sanura Kassim ‘Sandra’) na mama la mama, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’ wamekutana pande za Sauz na kuponda raha.
 
Mkali wao ndani ya Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akila bata na mtoto mzuri, ‘Zari The Boss Lady’.
Chanzo makini kilicho karibu na Diamond, kimeeleza kuwa msanii huyo na mama’ke, katikati ya wiki iliyopita, walikwea ‘pipa’ kwenda nchini humo kwa ajili ya mapumziko mafupi kabla ya kuhudhuria ‘event’ ya utoaji Tuzo za Channel O (Choamva) ambazo msanii huyo ameshiriki.
 
Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Zari wkiwa kwenye picha ya pamoja na Kampani waliyokuwa nayo Sauzi.

Friday, November 28, 2014

DIAMOND, ZARI WAUMBUKA!

Licha ya madai wanayoyatoa mastaa wawili hot kwa sasa, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady kuwa si wapenzi bali kuna project wanaifanya, wawili hao wameumbuka.
Kuumbuka huko kumekuja kufuatia kuvuja kwa picha inayowaonesha mastaa hao wakidendeka huku wakiwa kwenye hisia kali.



Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Zarinah Hassan wakibusiana kimahaba.
Katika picha hizo ambazo kwa sasa zinapatikana mtandaoni, Zari anaonekana akiwa amevaa kofia ya Diamond wakionekana wenye furaha na baadaye wakahamia kwenye kupeana mahaba.
Aidha, picha ambayo inawaumbua ni ile ya kudendeka ambapo baadhi ya wadau walioiona walisema, inavyoonekana projecti wanayoifanya imevuka mipaka.

 
Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Zarinah Hassan wakiwa kwenye pozi.
“Wasitutanie bwana, hivi kweli kwa picha hii watasema ni projekti? Hawa ni wapenzi ila hawataki tu watu wajue,” alisema mdau mmoja aliyejitambulisha kwa jina la John baada ya kuona moja ya picha hizo.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate