Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, akiwa katika pozi na mpenzi wake Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.
MUSA MATEJA
Utata mpya umeibuka wakati mama kijacho wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, akitarajiwa kujifungua muda wowote kutoka sasa, ishu ni juu ya uraia wa mtoto atakayezaliwa.
TUJIUNGE NA MTU WA NDANI
Habari kutoka kwa mtu wa ndani wa familia hiyo zilidai kwamba, utata umezidi kuigubika familia hiyo kwa kile kinachodaiwa kuwa ndugu wa pande zote kuendelea kuvutana juu ya Zari ajifungulie nchi gani kati ya Tanzania, Uganda na Afrika Kusini ‘Sauz’.
Utata huo umevuja wakati paparazi wetu akiwa katika mishemishe za kutaka kujua Zari alipo kwa sasa na atajifungulia katika hospitali ipi ndipo alipopenyezewa ‘ubuyu’ kwamba hadi sasa kuna utata mkubwa katika familia hiyo.
MABISHANO YA URAIA
Chanzo kilimweleza mwanahabari wetu kuwa, kikubwa ni mabishano ya uraia na sehemu sahihi ya kujifungulia mtoto huyo.
Kilidai kwamba, suala hilo limekuja kufuatia ndugu wa Zari kutaka ajifungulie Sauz jambo ambalo Diamond na familia yake wamekuwa wakilipinga vikali.
ZARI NJIA PANDA
Ilisemekana kwamba, kwa upande wake Zari amekuwa njia panda kutokana na shinikizo hilo huku mama Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ naye akisisitiza kuwa lazima Zari ajifungulie Bongo ili amuhudumie mkwe wake huyo.
“Yaani ndugu wa Zari wanampa Diamond wakati mgumu sana kutokana na kuendelea kung’ang’ania Zari akajifungulie kwao (Sauz ambako kuna ndugu wengi) wakati furaha ya Diamond ni kuona mtoto akizaliwa Bongo.