EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA
Showing posts with label Diamond. Show all posts
Showing posts with label Diamond. Show all posts

Wednesday, August 5, 2015

Diamond apagawa Aunt, Iyobo kuoneshana mahaba live

IYOBO (1)Moses Iyobo akiwa  na mzazi mwenzake, Aunt Ezekiel usiku wa kuamkia Agosti 3, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Hoteli ya Regency iliyopo Mikocheni jijini Dar.
Musa Mateja
Aah! Rais wa Wasafi Classic Baby (WCB), Nasibu Abdul ‘Diamond’, juzikati alijikuta akipigwa butwaa kufuatia kitendo cha mcheza shoo wake, Moses Iyobo ëMozeí na mzazi mwenzake, Aunt Ezekiel kuoneshana ‘mahaba nipeleke kuzimu’ hadharani, Risasi Mchanganyiko lilikuwepo kushuhudia.
IYOBO (7)
Tukio hilo la Diamond kupagawishwa na mahaba ya wawili hao lilijiri usiku wa kuamkia Agosti 3, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Hoteli ya Regency iliyopo Mikocheni jijini Dar ambapo kulikuwa na sherehe ya kuzaliwa ‘bethidei’ ya Iyobo. Lakini kabla ya kufika kwenye tukio hilo, twende hatua kwa hatua.
MWONEKANO WA DIAMOND UKUMBINI
Akiwa kwenye sherehe hiyo iliyojazwa pia na mastaa, muda mwingi Diamond alionekana mwenye furaha ya hali ya juu kufuatia mishemishe za bethidei hiyo iliyoandaliwa na Aunt kama moja ya kumshtukiza ‘sapraizi’ mpenzi wake huyo.
Habari zinasema mpaka Iyobo anaingia ukumbini hapo alikuwa hafahamu kama kuna sherehe ya kuzaliwa kwake.
IYOBO (2)
Rais wa Wasafi Classic Baby (WCB), Nasibu Abdul ‘Diamond’ akiwa kabeba keki.
MUDA WA MSHTUKO
Iyobo alizama ukumbini hapo saa 7 usiku kwa kuitwa na Aunt. Aunt pia ni staa wa sinema za Kibongo.
Baada ya Iyobo kuingia ukumbini alipata mshtuko kufuatia Diamond na nyota wa filamu za Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ kumkaribisha kwa kummwagia maji na vinywaji mbalimbali ambapo waalikwa wengine nao waliungana kumuogesha huku wakimwimbia ‘hepi bethidei tu yu.’
IYOBO (3)
DIAMOND AFUNGUA SHAMPENI
Baada ya zoezi la kumkaribisha Iyobo aliyekuwa amelala zake nyumbani kwa Aunt kumalizika, Diamond alipewa chupa ya kinywaji aina ya shampeni kwa ajili ya kufungulia sherehe hiyo ambayo ilianza hapo.
IYOBO (5)
Moses Iyobo akiwa kamkumbatia mpenzi wake Aunt Ezekiel.
DIAMOND ACHEZA HUKU NA KULE
Katika hatua nyingine, waalikwa walitumbua macho kumwangalia Diamond ambaye muda mwingi alikuwa akicheza tena kwa vituko mbalimbali.
IYOBO (4)
ABEBA KEKI
Pengine ni kwa sababu ilikuwa bethidei ya mcheza shoo wake, kwani ulipofika wakati wa kupeleka keki mezani, Diamond aliibeba yeye hadi eneo husika kwa ajili ya ‘kulishania’.
IYOBO (6)
MAHABA NIPELEKE KUZIMU SASA!
Sasa wakati Aunt na Iyobo wakiwa katika tukio la kulishana keki kwa mtindo wa mahaba nipeleke kuzimu (mdomo kwa mdomo), Diamond alionekana kushtuka na kuwatumbulia macho (angalia picha ukurasa wa mbele).

Saturday, July 25, 2015

Utata mpya mtoto wa Diamond!

Diamond-Platnumz-na-Zari
Staa wa Bongo Fleva,  Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’,  akiwa katika pozi na mpenzi wake Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.
MUSA MATEJA
Utata mpya umeibuka wakati mama kijacho wa staa wa Bongo Fleva,  Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’,  akitarajiwa kujifungua muda wowote kutoka sasa, ishu ni juu ya uraia wa mtoto atakayezaliwa.
TUJIUNGE NA MTU WA NDANI
Habari kutoka kwa mtu wa ndani wa familia hiyo zilidai kwamba, utata umezidi kuigubika familia hiyo kwa kile kinachodaiwa kuwa ndugu wa pande zote kuendelea kuvutana juu ya Zari ajifungulie nchi gani kati ya Tanzania, Uganda na Afrika Kusini ‘Sauz’.
DIAMONDZARI.jpg
Utata huo umevuja wakati paparazi wetu akiwa katika mishemishe za kutaka kujua Zari alipo kwa sasa na atajifungulia katika hospitali ipi ndipo alipopenyezewa ‘ubuyu’ kwamba hadi sasa kuna utata mkubwa katika familia hiyo.
MABISHANO YA URAIA
Chanzo kilimweleza mwanahabari wetu kuwa, kikubwa ni mabishano ya uraia na sehemu sahihi ya kujifungulia mtoto huyo.
Kilidai kwamba, suala hilo limekuja kufuatia ndugu wa Zari kutaka ajifungulie Sauz jambo ambalo Diamond na familia yake wamekuwa wakilipinga vikali.
ZARINADIAMOND4.jpg
ZARI NJIA PANDA
Ilisemekana kwamba, kwa upande wake Zari amekuwa njia panda kutokana na shinikizo hilo huku mama Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ naye akisisitiza kuwa lazima Zari ajifungulie Bongo ili amuhudumie mkwe wake huyo.
“Yaani ndugu wa Zari wanampa Diamond wakati mgumu sana kutokana na kuendelea kung’ang’ania Zari akajifungulie kwao (Sauz ambako kuna ndugu wengi) wakati furaha ya Diamond ni kuona mtoto akizaliwa Bongo.

Thursday, July 9, 2015

DIAMOND, ZARI KIMENUKA

OHOOO! Wakati penzi lao likitarajia matunda ya kupata kijacho miezi kadhaa ijayo, uhusiano wa Nasibu Abdul ‘Diamond na staa wa Uganda, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ umedaiwa kutibuka baada ya Diamond kufunguka kuwa anampenda mwigizaji wa Nigeria, Omotola Jalade Ekeinde, Amani linakupa mchapo.Mkali wa Bongo fleva Nasibu Abdul ‘Diamond.
Diamond aliitoa kauli hiyo hivi karibuni jijini Lagos alipokuwa akihojiwa redioni ambapo alipoulizwa ni wasanii gani maarufu anavutiwa nao kimapenzi, bila hiyana, mkali huyo kutoka Tandale-Dar, alisema ni Omotola, Tonto Dikeh na Genevieve Nnaji.
WAMBEA WASHIKIA BANGO
Mara baada ya Diamond kutamka kauli hiyo na kusambaa kwenye mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo vya habari, ‘wambea’ walilivalia njuga suala hilo na kumfikishia maneno Zari, ambaye naye anadaiwa kuyaamini na kumcharukia Diamond.
TUJIUNGE NA CHANZO
Chanzo makini kilicho karibu na Diamond kilipenyeza habari  kuwa, kauli hiyo aliyoitoa nchini Naigeria imezua mtafaruku mzito kwani Zari hakufurahishwa nayo kwa kile kichoelezwa kuwa ni kuonesha dhahiri kwamba staa huyo anayesumbua na wimbo wa Nana anaweza kuhamishia ‘majeshi’ kwa Omotola, Genivieve kama si Tonto.
“Ndugu yangu nakwambia upande wa pili kimesanuka ile mbaya baada ya Diamond kusikika akisema anawazimikia Omotola na wenzake wa Nigeria, mama la mama (Zari) huko aliko (Sauz) kafura ileile.

Saturday, June 20, 2015

KUMUONA MTOTO WA ZARI, MIL.20

AMA kweli Mbongo-Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Mama Kijacho, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, sasa ni wa kimataifa zaidi ambapo wakati mwanamama huyo akijiandaa kujifungua, tayari mtoto ajaye ameandaliwa chumba maalum cha kulala na gharama za kumuona kwa atakayehitaji picha hasa za kwenye vyombo vya habari, itakuwa si chini ya Sh. milioni 20.
Mbongo-Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Mama Kijacho, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.
CHANZO KUTOKA WCB
Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho kipo ndani ya Wasafi Classic Baby (WBC), Diamond na Zari wameamua kutenga chumba maalum cha mtoto wao atakapozaliwa.
Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ akiwa katika pozi na lafiki yake.
MASHARTI YA KUMWAGA
Ilidaiwa kwamba, chumba hicho kitakuwa mahususi kwa mtoto tu na wala hakuna mtu mwingine atakaye ruhusiwa kuingia kumuona bila malipo zaidi ya mama, baba na familia yao ambao nao wataingia kwa sharti la kutopiga picha.
“Naona Zari anampeleka Diamond kimataifa kila kukicha maana nimeshuhudia chumba kina ‘full’ mazagazaga ya mtoto na nilipouliza nikaambiwa hicho ni chumba cha mtoto wa Zari mara tu atakapozaliwa.

Wednesday, May 27, 2015

DIAMOND ATELEKEZA WATOTO SHULE!

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS KABANG! Staa anayevuna fedha nyingi kupitia kipaji chake cha muziki, Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amewatelekeza watoto katika Shule ya East Africa International jijini Dar ambao aliahidi kuwalipia ada, Risasi Mchanganyiko linakuwa la kwanza kukudondoshea.
 
Wanafunzi wanaodaiwa kutelekezwa na Staa anayevuna fedha nyingi kupitia kipaji chake cha muziki, Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Chanzo makini kililiambia gazeti hili juzi kwamba, baada ya Diamond kuwashindanisha watoto hao, Hillary na Hamis (katika picha no. 1 na 2 zilizoko ukurasa wa mbele walipelekwa shule na Diamond) katika shindano la Ngololo lililonyika Januari, mwaka jana katika Viwanja vya Leaders Club, Dar na kushinda aliamua kuwapeleka katika shule hiyo na kuahidi kuwalipia ada kila mwaka lakini kuanzia hapo aliwatelekeza.
“Jamani Diamond kila kukicha anafanya shoo za mamilioni lakini ameshindwa kuwalipia ada wale watoto ambao aliahidi kuwasomesha. Wamesoma mwaka mmoja tu,  mwezi uliopita walitimuliwa na sasa wako nyumbani. Inauma sana kwani hawa watoto walitolewa kwenye shule za kawaida na yeye ndiyo akawapeleka kule,” kilisema chanzo hicho.
WAZAZI WANASEMAJE?
Akizungumza na gazeti hili, mmoja wa wazazi wa wanafunzi hao, Fadhili alisema watoto wao walitimuliwa shuleni tangu April mwaka huu kwa kuwa, Diamond hakuwahi kuwalipia ada tangu alipowaingiza pale.“Inauma sana, kwani tangu watoto wetu watimuliwe tumekuwa tukifuatilia kwa mtu tuliyeambiwa ni msimamizi wa Diamond (jina lake linahifadhiwa kwa sasa) lakini hatupi jibu la kueleweka.

 
Nasibu Abdul ‘Diamond akiwa na wanafunzi hao pamoja na mwalimu wao.

Tuesday, May 19, 2015

Diamond Platnumz ameanza kununua vitu vya mtoto wake

Msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz anayetegemea kupata mtoto na mpenzi wake Zari ambaye ni mtu maarufu Uganda na Afrika mashariki ameanza kununua vitu vya mtoto wake kabla hajazaliwa. Diamond ambaye alikuwa Uingereza kwenye show ameonekana akifanya shoping kwenye maduka ya vitu vya watoto.
 zari baby 2 zari baby 3 zari baby 4

Monday, April 27, 2015

DIAMOND PLATINUMS AKIBUSU MIMBA YA ZARI


Diamond Platinums akibusu Tumbo la Mpenzi wake Zari the big Boss Lady jana zanzibar walipokuwa Mapumzikoni mara baada ya Diamond Jana usiku kuangusha Bonge la Show bab kubwa Katika viwanja vya Ngome Konge Zanzubar.
Zari ambaye ni Mjamzito wamwkuwa wakitenda Vyombo vya habari Pamoja na Mitandao ya Kijamii kutokana na Uhusiano wao,Katika Mitandao ya Kijamii kwa sasa Ni Nadra sana Kupita siku mbili bila uhusiano

Friday, April 3, 2015

ZARI AZUA KIZAAZAA MSIBANI


Dustan Shekidele, Morogoro
Kazi ipo! Mwandani wa staa mkubwa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari’ juzikati alizua kizaazaa kisa ujauzito alipohudhuria kwenye msiba wa aliyekuwa bosi wa Tip Top Connection, Abdul Taletale ‘Abdul Bonge’ aliyefariki dunia ghafla wikiendi iliyopita.
Mwandani wa staa mkubwa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari akifichwa na bodigadi wake.
Tukio hilo la Zari lilichukua nafasi katika Kijiji cha Mkuyuni, Tarafa ya Matombo mkoani hapa ambapo mastaa kibao walisafiri kutoka Dar kwa ajili ya mazishi ya kiongozi huyo.
ILIKUWAJE?
Awali, katika tukio hilo lililoshuhudiwa na Ijumaa mapema Jumanne wiki hii, Zari na Diamond, wakiwa wameongozana na wapambe wao walifika eneo la msiba ambapo kwa taratibu za Kiislam, wanawake hawachanganyiki na wanaume hivyo Zari akachukuliwa kwenda upande mwingine huku Diamond akielekea upande wa wanaume.
HALI YA HEWA YABADILIKA
Mara baada ya mastaa hao kutinga eneo hilo, umati mkubwa uliokuwa msibani hapo ulianza kuwazingira huku kila mmoja akitaka kuwaona.Akiingizwa garini.
ZARI AIBUA KIZAAZAA
Akiwa upande wa wanawake wenzake, Zari alijikuta akizungukwa na baadhi ya watu walionekana wazi kumchunguza kuanzia miguuni hadi kichwani ikidaiwa kuwa, walikuwa wakicheki kama kweli ana mimba ya Diamond.

Thursday, March 19, 2015

DIAMOND, PENNY MZOZO UPYA

IMEVUJA! Ile mimba ya aliyekuwa Mtangazaji wa Efm Radio, Penieli Mungilwa ‘Penny’ ambayo ilijulikana alipachikwa na staa wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ imezua mzozo upya baada ya kuvuja kwa madai mengine.
Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Chanzo makini kimeliambia Amani kwamba, tofauti na madai ya Diamond kwamba Penny alitoa mimba yake, lakini kumbe Diamond hakumpa mimba ila ilikuwa ni magumashi ya Penny.
SIKIA HII
“Hali ilikuwa hivi! Kutokana na Diamond kutafuta mtoto kwa muda mrefu, hasa kwa mpenzi wake wa nyuma Wema Sepetu kushindikana, ikabidi Penny atumie mbinu yake ili kufaidika na pesa za Diamond.
“Penny aliahidiwa na Diamond kwamba, kama atakubali kuzaa naye atamnunulia gari zuri, kwa hiyo kazi ikawa kwa Penny sasa, afanyaje?
“Siku moja Penny alimwambia Diamond kwamba amenasa, Diamond akafurahi sana, lakini kumbe Penny alishaenda kwenye hospitali moja kubwa iliyopo Kinondoni (jina tunalo), akaongea na nesi mmoja kwamba kama atakwenda na Diamond kupima mimba akubali kwamba anayo, lengo lake ni kupata gari,” kilisema chanzo hicho.
Mtangazaji wa Efm Radio, Penieli Mungilwa ‘Penny’ akiwa na aliyekuwa mpenzi wake Nasibu Abdul ‘Diamond’.

Monday, March 16, 2015

ILIBAKI HIVI TU DIAMOND AKATWE MGUU!


Musa Mateja
Msanii nguli wa muziki wa kizazi kipya na nyota wa Wimbo wa Nitampata wapi aliyewahi kuwa mchumba wa Wema Sepetu, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amenusurika kukatwa mguu katika Hospitali ya TMJ, Mikocheni jijini Dar es Salaam kufuatia ugonjwa wa Foot Corn (maarufu kwa jina la kisahani) kumtesa kwa kipindi kirefu.
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, Diamond ambaye kwa sasa anaminya kimalavidavi na mwanamama Zarina Hassan ‘Zari’, alianza kusumbuliwa na ugonjwa huo takribani siku 730 zilizopita (miaka miwili), huku mwenyewe akipuuzia matibabu yake na kuelekeza nguvu kwenye shoo za ndani na nje ya nchi.

Wednesday, March 11, 2015

DIAMOND APATA MSHTUKO DENI LA MIL.800

Musa Mateja/mchanganyiko MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amepatwa na mshtuko mkubwa baada ya kuwepo madai ya kudaiwa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 800 na serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Risasi Mchanganyiko linakupa mchapo kamili.
Msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
ILIKUWAJE?
Mwishoni mwa wiki iliyopita, barua inayodaiwa kuandikwa na mamlaka hiyo halali ya serikali, ilisambazwa mitandaoni, ikielezwa kuwa ilikuwa imetumwa kwa meneja wa msanii huyo ambaye kwa sasa ndiye yupo juu, ikimtaka kupeleka nakala za mikataba yote ya muziki aliyoingia kwa ajili ya kufanya shoo, kuanzia mwaka 2010 hadi sasa.

GUMZO MITANDAONI
Baada ya kuwekwa kwa barua hiyo mitandaoni, watu mbalimbali walitoa maoni yao walionyesha hisia tofauti, baadhi wakipinga kwa madai kuwa wanamuonea huku wengine wakisema siyo Diamond tu, bali wasanii wote wanastahili kulipa kodi kutokana na mapato wanayopata kupitia kazi zao.

KODI ZIPOJE KIBONGOBONGO?
Mtaalam mmoja wa mambo ya kodi aliyezungumza na Risasi Mchanganyiko, alisema kwa mujibu wa taratibu zao, msanii huyo anastahili kulipa kodi kiasi cha asilimia kumi ya fedha anazopata katika kila mkataba anaoingia.

“Kuna walipa kodi wengine kama wafanyabiashara, hawa wanalipa kile ambacho kitaalamu kinajulikana kama Capital Gain, yaani kulipa kadiri unavyopata. Mtu anakwenda TRA mwenyewe na kueleza mapato yake na mamlaka itampangia kiasi cha kulipa. Ila watu kama wasanii na wengine wanaolipwa, wanatakiwa kutoa asilimia kumi ya malipo,” alisema mtaalam huyo aliyekataa kutajwa jina gazetini.
DIAMOND ANADAIWA SH. NGAPI?
Kama suala hilo litafanyika kwa mujibu wa mtaalam huyo, Diamond ambaye malipo yake kwa shoo moja yanatajwa kuwa ni shilingi milioni 20 kwa sasa, atatakiwa kulipa kiasi kinachozidi milioni 800 kutokana na hesabu zilizofanywa na watu wanaofuatilia muziki wake.

Thursday, February 19, 2015

MASTAA WAMCHANA DIAMOND

IMEKULA kwake! Wasanii wa sinema na Bongo Fleva wamemchana vibaya staa wa muziki wa kizazi kipya, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwamba si mtokaji kwenye misiba ya wenzake.
Staa wa muziki wa kizazi kipya, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Wakizungumza na Amani kwenye maziko ya baba mzazi wa Mbongo Fleva, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’, Ebby Sykes, Jumatatu iliyopita, wasanii hao walioomba majina yao yalindwe walisema kumbukumbu za vichwani mwao zinaonesha kuwa, Diamond amekuwa akichagua misiba ya kujitokeza hasa ile ambayo itampa  ‘kavareji’ kwenye vyombo vya habari.

Tuesday, February 17, 2015

JULIANA KANYOMOZI AZUNGUMZIA MUZIKI WA DIAMOND NA ANGEFANYA NAE COLLABO ITAKUWAJE

diamond on sammisagocom
Kupitia ‘Bill Da African wa Uganda All Star‘  Muimbaji kutoka Uganda ‘Juliana Kanyomozi’ amesema yeye ” binafsi ni shabiki wa nyimbo za msanii kutoka Tanzania Diamond Platnumz,nina furaha sana kwa mafanikio aliyopata, anakipaji kikubwa ,anawakilisha Afrika Mashariki kwa ukubwa zaidi huko nje” .
juliana
Akaaulizwa kama atafanya wimbo na Diamond utakuaje na utaitwaje, Juliana anasema “Ukiwa studio mambo mengi yanatokea, sababu ni msanii anayefanya nyimbo za mapenzi nadhani utakuwa wimbo wa mapenzi, na mkubali na amebarikiwa katika kazi zake ” .

Monday, February 16, 2015

MAMA DIAMOND MUNGU MKUBWA!

Thank you God! Neno pekee unaloweza kusema ni Mungu mkubwa baada ya kusikia taarifa kwamba mama mzazi wa Supastaa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kassim ‘Sandra’, amerejeshwa Bongo kutoka India ambapo afya yake imetengemaa, Ijumaa Wikienda lina kitu kamili.
Mama mzazi wa Supastaa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kassim ‘Sandra’ akirejea kutoka India.
Habari kutoka chanzo cha kuaminika ndani ya familia ya jamaa huyo, kililieleza gazeti hili kwamba, tayari  Sandra amesharejea katika hali yake ya kawaida na ndiyo maana akarudi Bongo baada ya kulazwa hospitalini nchini India kwa kusumbuliwa na ugonjwa wa kupooza.
Mwanafamilia huyo alisema kwamba, Diamond na mama yake walirejea nchini wikiendi iliyopita baada ya kufanyiwa matibabu ya kina na madaktari kujiridhisha kwa hali ya juu dhidi ya afya yake ambapo waligundua hali aliyonayo kwa sasa imetengemaa hivyo wakamruhusu kurejea kuungana na familia yake.
Habari zilieleza kuwa kwa sasa bimkubwa huyo yupo fiti na anaendelea na mazoezi ya kawaida huku akimalizia dawa alizopewa na wataalam hao wa afya.
Mama na mwana wakiwa ni wenye furaha baada ya kukutana tena.
“Mama amerejea juzikati kutoka kwenye matibabu nchini India alikokuwa amepelekwa, hivyo tunamshukuru Mungu sasa anaendelea vizuri na afya yake kwa jumla inaridhisha ingawa ana programu ya kufanya mazoezi mepesi ili aweze kuimarika zaidi ya vile alivyokuwa awali.

Thursday, February 5, 2015

KITUMBO CHA ZARI KIMEMFURAHISHA MAMA WEMA!

Stori: Imelda Mtema/Amani
SIKU chache baada ya Nasibu Abdul ‘Diamond’ kuweka picha zinazomuonesha mpenzi wake wa sasa Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ akiwa na kitumbo kinachoashiria kukua kwa ujauzito, mama mzazi wa zilipendwa wa Diamond, Wema Sepetu ‘Madam’, Mariam Sepetu amefunguka kuwa amefurahia tukio hilo.
Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’ akiwa na mpenzi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Mzazi huyo ambaye ni fundi wa kuzungumza, alisema tukio hilo limemfurahisha kwani anaamini ndoto za Diamond kurudiana na binti yake zitakuwa zimeyeyuka rasmi kama alivyokuwa akimuomba Mungu siku zote.
Kuonesha kwamba amefurahishwa na kitendo hicho, alimtaka Zari aendelee kumpenda Diamond, amgande kila idara ili isije kutokea akarudi kwa binti yake ambaye walimwagana mwishoni mwa mwaka jana.
“Yaani kama inawezekana naomba sana huyo Zari azidi kumganda Diamond, asimpe muda wa kugeuka nyuma kabisa ili mambo mengine yaendelee kwa sababu uhusiano wa Diamond na mwanangu haukuwa na baraka zangu,” alisema mama Wema.
Mama Sepetu aliongeza kuwa, hana maana ya kumchagulia mchumba mwanaye bali anahitaji mwanaume yeyote mwenye heshima na anayejiheshimu kwa sababu mwanaume asiyejitambua hawezi kuwa baba bora wa familia.

Thursday, January 22, 2015

WEMA HAJAMPELEKA DIAMOND MAHAKAMANI – MARTIN KADINDA

Meneja wa Wema Sepetu, Martin Kadinda amekanusha taarifa zilizoandikwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari nchini likiwemo gazeti la Mtanzania kuwa amempeleka Diamond polisi kwa kile kinachosemwa ni kumtapeli shilingi milioni 10.


Martin ameiambia Mtandao wa Bongo5 kuwa Wema na Diamond hawadaiani chochote na kwamba habari hizo ni za uongo.

“Unajua tatizo ni kwamba hatujajua source ni nani,” amesema Martin. “Kwa sababu taarifa ikishaingia kwenye social network everybody posts, kwahiyo sisi tunamtafuta nani ameianzisha hiyo stori. “We don’t have any issue with Diamond. Diamond hana issue yoyote na Wema,” amesisitiza.

“Kwahiyo tunashangaa ni kama ambavyo wanazusha sijui kafumwa na nani ni uongo mtupu. Lakini nashangaa media ambazo zinaaminika zinaamua kuandika story bila kumpigia simu mhusika au meneja na kuuliza ukweli wa hiyo story.”

BONYEZA HAPA KUSOMA ===>WEMA AMPELEKA DIAMOND POLISI, KISA NI DENI

Diamond akimtaja Zari kwenye wimbo wa Mr Blue 'Pesa'

Monday, January 19, 2015

MUME: ZARI HAWEZI KUZAA NA DIAMOND

Stori: Kampala, Uganda
Oohoo! Wakati staa mkubwa wa muziki wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akichekelea kitendo cha mpenzi wake wa sasa, Zarinah Hassan ‘Zari’ au ‘The Boss Lady’ kunasa mimba yake, habari ya mjini huko Kampala, Uganda ni juu ya aliyekuwa mume wa mwanamama huyo, Ivan Ssemwanga kufunguka na kusema: “Naapa Zari hawezi kuzaa na Diamond.”
Staa mkubwa wa muziki wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na Zarinah Hassan,  'Zari'.
HABARI YA MJINI
Wikiendi iliyopita, vyombo vya habari na mitandao nchini Uganda ambako kuna makazi mengine ya Zari mbali na Afrika Kusini, kulipambwa na habari hizo baada ya mwanaume huyo aliyezaa na mwanamama huyo watoto watatu kuanika siri nzito juu ya ishu hiyo.
‘Ubuyu’ huo ulidadavua kwamba, kwanza jamaa huyo mwenye utajiri wa kutupwa alianza kwa kuelezea namna alivyoshtuka aliposikia Zari ni mjamzito.

Saturday, January 17, 2015

SHABIKI ZARI KUWA NA UJAUZITO, INA MAANA DIAMOND NA ZARI WALIFANYA NGONO BILA KINGA,WALIPIMA NA WALIJUANA KWA MUDA GANI ?

zari 56

Kupitia info za mashabiki wa sammisago.com, Shabiki wa Diamond ametuma mtazamo wake kuhusu issue ya Diamond na Zari kutegemea mtoto na kusema.
 
Sijawahi kuona mastaa hawa wakiwa hospitalini au kwenye kituo chochote wakipima afya zao, ukizingatia ni watu wakuweka hadharani mambo yao yote basi hata kupima wangeweka instagram au huko twitter

Ni vizuri staa kuzaa na staa mwenzake ila Diamond ana muda wa kuwa baba? mahusiano yake mengi ni kiki au drama a,bazo hata Kwa Zari tuliyedhani itakuwa tofauti kumbe ni yale yale, mimi ni shabiki tu ila nawatakia kila la heri kwenye familia yao wanayoanzisha
Shabiki alimaliza hivyo.Upi mtazamo wa juu comment za huyu shabiki ?

Friday, January 9, 2015

KISA ZARI DIAMOND AITWA SHOGA

HII ni ‘bad news’ kwa staa namba moja wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’. Mfanyabiashara maarufu nchini Uganda anayefahamika kwa jina la King Lawrence, ameibuka na kumuita nyota huyo shoga.
Staa namba moja wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na Zarinah Hassan ‘Zari’.
ISHU ILIPOIBUKIA
King ambaye ana makazi yake pia nchini Afrika Kusini, amedaiwa kutoa kauli hiyo juzi, Jumatano kupitia mtandao wa Facebook akionesha kukerwa na kitendo cha staa wa muziki Uganda, Zarinah Hassan ‘Zari’ kuangukia katika penzi la Diamond.
ATUMIA GIA YA WATOTO
Awali, King ambaye imeelezwa alikuwa na urafiki na dereva wa aliyekuwa mume wa Zari, Ivan Semwanga, alianza kwa kumchokonoa Diamond kwa gia ya kujifanya anawatetea watoto wa Zari ambapo alitupia picha ya Zari akiwa na Diamond mtandaoni ikiwa na ujumbe wenye kejeli na jeuri ya fedha.
UJUMBE ULIVYOSOMEKA
“As a concerned uncle, Im offering Zari’s tomboy Diamond Dola 40,000 so as to leave the old mom of three to take care of her kids. The young boys miss their mom. Please Diamond do it for the kids.”
(Nikiwa kama mjomba, ninampa jikedume wa Zari, Diamond, Dola 40, 000 (Sh. Mil 66) ili amuache mama wa watoto watatu (Zari) awalee vizuri watoto wake. Watoto wanammisi mama yao.”
Diamond Platnumz na Zari wakidendeka.
ABADILISHA GIA
Kuonesha ana mpango mchafu wa kumchafua Diamond ambaye anaipeperusha vyema bendera ya Afrika kimuziki, badala ya ishu ya watoto, alibadili upepo na kujinadi eti yeye ndiye wa kwanza kutembea na Zari.
Pasipo kueleweka kusudi lake, alimpiga dongo Diamond ambaye usiku wa kuamkia leo alipewa heshima ya kipekee kutumbuiza kwenye Tuzo za Wanamichezo Bora zilizoandaliwa na Shirikisho la Afrika (Caf) nchini Nigeria.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate