BAADA ya klabu ya Simba kulaani kitendo cha Azam FC kumuuza
mchezaji Mrisho Ngassa kwa El Mereikh ya Sudan, klabu hiyo sasa umeamua
kushtaki suala hilo kwa Shirikisho la soka Tanzania (TFF).
Juzi, Azam FC ilitangaza kumuuza Ngassa kwa dola 75,000 huku ikipanga
kumpatia dola 50,000 kama dau la kusaini mkataba wa miaka miwili.Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, Azam wamefanya
uhuni katika mazingira ya kumuuza Ngassa kwani nyota huyo ana mkataba na
Simba utakaokwisha Mei 31, 2013.
Alisema kwa mujibu wa makubaliano yaliyopo kwenye mkataba wa Ngassa, Simba na Azam zote zina mamlaka na mchezaji huyo, hivyo hakuna mmojawapo kufanya maamuzi bila kumshirikisha mwingine.
“Mkumbuke mbali ya dola 25,000 tulizotoa kwa Azam FC, tuliingia
gharama nyingine za kumshawishi zaidi kama gari, donge nono, pia tulimpa
kazi ya ziada kocha wetu kuhakikisha anapandisha kiwango cha Ngassa,”
alisema.
Kamwaga alisema Azam wanajichanganya juu ya suala hilo kwani awali
waliandika barua kuwa Ngassa amepata timu, hivyo anataka kuondoka Simba
kabla ya kuandika barua nyingine kuwa wameamua kumuuza kwa sababu Simba
imemsainisha mkataba mwingine.