MSANII Judith Wambura ‘Lady Jaydee,’ juzi usiku aliubeba
uzinduzi wa filamu ya ‘Foolish Age,’ iliyochezwa na Elizabeth Michael
Lulu uliofanyika Ijumaa usiku katika ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar
es Salaam.

Jaydee aliyepanda jukwaani baada ya tukio la uzinduzi wa filamu hiyo
akikaribishwa
na Lulu aliyetamka wazi kuwa amekuwa akimpenda Jaydee ‘Anakonda’ tangu
utotoni mwake, aliufanya ukumbi urindime kwa mayowe ya shangwe na
nderemo.
“Napenda kuwashukuru watu wote mliofika hapa Mlimani City katika
uzinduzi wa filamu hii ambayo naamini italishika soko ipasavyo kwa
sababu imechezwa kwa umahiri mkubwa,” alisema Lulu na kuamsha shangwe za
aina yake.
Lulu hakuishia hapo, ndipo akasema atakuwa mchoyo kama asingemtaja
Lady Jaydee aliyekuwa miongoni mwa watu mashuhuri waliofika katika tukio
hilo la historia maishani mwake.
“Lady Jaydee nakupenda sana, njoo dadangu, nilikuwa nakupenda sana
tangu nilipokuwa mdogo hadi sasa bado nakupenda,” sauti ya Lulu
ilisikika ukumbini kupitia kipaza sauti.
Kilichofuata ni Jaydee kwenda jukwaani na moja kwa moja akaanza kuimba
wimbo
wa






