MADAI! Mwanaume mmoja aliyejitambulisha kwa jina la
Severin Daniel Ndauka amejitokeza katika Ofisi za Global Publishers na
kudai kwamba, staa wa sinema za Bongo, Rose Donatus Ndauka ni mtoto wa
kaka yake ambaye alichukuliwa kutoka Tanga na kupelekwa jijini Dar.
Mzee Severin Daniel Ndauka anaedai kuwa Rose Ndauaka ni mwanaye.
Mzee huyo aliyekuwa akizungumza kwa kujiamini mbele ya waandishi
wetu, alisema mwaka 1979, shemeji yake, Nyazimbili au mama Godwin
(anayedaiwa ni mama wa Rose) alijifungua mtoto wa kike katika Kijiji cha
Sakura wilayani Pangani, Tanga ambapo kwa bahati mbaya mama huyo
alifariki dunia hivyo mtoto kuchukuliwa na kanisa ambalo lipo Msimbazi
Dar hakutaka kulitaja jina lililomlea mtoto huyo kwa kuwa familia
haikuwa na uwezo.
“Baada ya hapo, hatupata taarifa tena lakini mimi niliamua kuja Dar
kwa ajili ya kumtafuta Rose. Nilikwenda Msimbazi, nilipofika nikaambiwa
Rose alichukuliwa na kituo cha kulea watoto kilichopo Kurasini. Ilibidi
niende Kurasini, kufika nikaambiwa alichukuliwa na msamaria mwema kwa
ajili ya kumlea kama mtoto wake.
Staa wa sinema za Bongo, Rose Donatus Ndauka.
“Tangu hapo hatukupata taarifa nyingine lakini baadaye dada yangu
anaitwa Maria Ndauka akanipigia simu, akasema amemuona Rose kwenye
televisheni akiigiza na marehemu Steven Kanumba ndiyo nimekuja hapa
mnisaidie kumpata,” alisema mzee huyo.