EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA
Showing posts with label Ray. Show all posts
Showing posts with label Ray. Show all posts

Saturday, April 4, 2015

RAY AMSALITI CHUCHU KWA HUSNA, WANASWA USIKU

Musa mateja
MUIGIZAJI nyota wa filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’, amedaiwa kumsaliti mpenzi wake wa siku nyingi, Chuchu Hans baada ya kukutwa akiwa amepozi kimahaba na mshiriki wa Miss Tanzania mwaka 2011, Husna Maulid katika Ukumbi wa Escape One, Mikocheni jijini Dar, hivi karibuni.Muigizaji nyota wa filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ akipozi kimahaba na Husna Maulid.
Wawili hao waliokuwa wamepakatana, walikutwa katika ukumbi huo wakati bendi mbili kubwa za muziki wa dansi nchini, FM Academia na The African Stars ‘Twanga Pepeta’ zilipokuwa zikiangusha burudani kabambe ya kushindana.
Uwepo wa Ray na Husna ulitafsiriwa kuwa ni usaliti kwani muda wote waliokuwa ndani ya ukumbi huo wawili hao walikuwa wamegandana kimahaba huku wataalamu wa ubuyu wakikazia madai kwa kusema wawili hao ni wapenzi.
Husna Maulid akisisitiza jambo kwa Ray.
“Sasa wewe kusoma hujui hata picha huoni? Hawa watakuwa ni wapenzi tu, haiwezekani mtu mpakatane, mpeane kampani kiasi hiki na mtu ambaye siyo mtu wako,” alisikika shuhuda mmoja.
Ray ambaye kabla ya kuwa na Chuchu aliwahi kutoka kimapenzi na mwigizaji Blandina Changula ‘Johari’ na Ruth Suka ‘Mainda’, alionekana kufurahia kumpakata Husna huku wakipeana kampani ya kuzungumza, lakini alipatwa na mshtuko mkubwa baada ya kugundua kuwa alikuwa akifuatiliwa na kamera ya paparazi wetu.
Kutokana na mazingira ya wawili hao ukumbini hapo, paparazi wetu alishindwa kuzungumza nao juu ya ishu hiyo na hata alipowatafuta kwa simu siku iliyofuata, simu zao ziliita bila kupokelewa (huenda walijua wataulizwa nini).Lakini Chuchu, ambaye ndiye ‘mmiliki’ wa Ray hivi sasa, alipoulizwa kama anajua lolote juu ya ukaribu wa watu hao, alishtuka na kudai haamini kama Ray anaweza kumsaliti au amewahi kupiga picha na Husna za kimahaba.
Muigizaji nyota wa filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray.
“Khaa! Unasemaje? Mimi siamini labda kama kuna picha zao za pamoja naomba unitumie Whatsapp nizione maana nashindwa niongee nini, sikujua kama walienda popote Ray na Husna.”
Mwanahabari wetu alimtumia picha hizo Chuchu lakini hadi tunakwenda mitamboni, mrembo huyo hakuwa amejibu kitu chochote.

Saturday, January 10, 2015

CHUCHU HANS AFUNGUKIA KUACHANA NA RAY

Stori: Musa Mateja na Gladness Mallya
STAA wa Filamu Bongo, Chuchu Hans juzikati alifungukia madai ya kwamba ameachana na mchumba wake Vicent Kigosi ‘Ray’, akaeleza kuwa, hakuna ukweli wowote juu ya hilo.Chuchu alifikia uamuzi wa kufafanua juu ya madai hayo juzi kufuatia tetesi zilizokuwa zimeenea kwamba yeye na kipenzi chake huyo wametibuana na sasa kila mtu kimpango wake.
Staa wa Filamu Bongo, Chuchu Hans akiwa na mpenzi wake 'Ray''.
Akifungukia juu ya uvumi huo Chuchu alisema: “Kutakuwa na watu wanaosambaza uongo huo, huwezi kuamini muda si mrefu nilikuwa na baby wangu Ray, tukawa tunashangaa tu juu ya umbeya huo.

Wednesday, December 17, 2014

CHUCHU HANS ACHARUKA MADAI YA USALITI

KIMENUKA! Msanii wa filamu, Chuchu Hans ambaye ni mpenzi wa wa nguli wa filamu Bongo, Vicent Kigosi ‘Ray’, amecharuka ishu ya kumsaliti mpenzi wake huyo na jamaa anayedaiwa kuwa ni mfanyabiashara anayeishi maeneo ya Mbezi Beach Dar.
Msanii wa filamu, Chuchu Hans.
Chanzo kinasema pamoja na Chuchu kuwa na Ray kwa muda wote, lakini inadaiwa kuwa muda fulani amekuwa akitoka na kwenda Mbezi anapoishi kijana huyo.
Hata hivyo paparazi wetu aliamua kumvutia waya Chuchu na kuzungumza naye ishu hiyo ambapo alidai stori hizo zinasambazwa na watu ambao lengo ni kutaka kumchafua kwa mpenzi wake Ray.
“Watu hawapendi kuniona natoka na Ray na ni hao ndiyo wanaotumia muda mwingi kutaka kutuvuruga. Siwezi kufanya hivi na huyo jamaa sijui wa Mbezi kwanza simfahamu na pili jamii haitanielewa nikifanya hivi,” alisema Chuchu.

Saturday, November 22, 2014

RAY: CHUCHU SASA NDO’ KILA KITU KWANGU

LEGENDARY kwenye anga la sanaa Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ kwa mara ya kwanza amefunguka kuwa mpenzi wake wa sasa, Chuchu Hans ndiye kila kitu na kilichobaki ni ndoa tu.
Legendary kwenye anga la sanaa Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ akiwa na mpenzi wake Chuchu Hans.
Akizungumza na paparazi wetu, Ray alisema licha ya kupitia katika changamoto nyingi za mapenzi lakini kwa Chuchu amefika na haoni tabu kujinadi kwa mtu yeyote juu ya penzi lake hilo.
“Chuchu ndiye kila kitu kwangu, tunaendana kwa kila kitu hivyo nitakaowaudhi kwa kumpenda yeye, wanisamehe,” alisema Ray.Ray kabla ya kuwa na Chuchu, kwa nyakati tofauti alikuwa akitajwa kushea penzi la mwigizaji Ruth Suka ‘Mainda’ na Blandina Chagula ‘Johari’.

Saturday, September 27, 2014

RAY, JB WAMPIGIA SALUTI KAJALA

Waigizaji wakongwe kwenye tasnia ya filamu Bongo, Jacob Steven ’JB’ na Vincent Kigosi ‘Ray’ wamempigia saluti muigizaji mwenzao,  Kajala Masanja kutokana na filamu fupi aliyotengeneza ya Mbwa Mwitu.
Staa wa Filamu Bongo, Kajala Masanja akihojiwa na waandishi wakati wa uzinduzi wa filamu yake ya Mbwa Mwitu.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye uzinduzi wa filamu hiyo uliofanyika Mlimani City juzi, JB alisema kuwa  Kajala amebuni kitu cha tofauti kabisa ambacho jamii nzima mpaka watoto wanafahamu kuhusu Mbwa Mwitu.

Wednesday, July 23, 2014

RAY, CHIKI NUSURA WAZICHAPE!

ILIBAKI kidogo mastaa wa sinema za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray’, na Salum Mchoma ‘Chiki’, wazichape baada ya kutokea mzozo kati yao uliodumu kwa dakika tatu wakirushiana maneno.
Staa wa sinema za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray’.
Tifu hilo lilitokea wikiendi iliyopita, Lamada Hotel – Ilala, Dar ambapo Chiki alimshukia Ray akidai kuwa (Ray) haungi mkono uongozi wa Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Nyerere’ ndiyo maana alikacha sherehe yake hivi karibuni.

Saturday, June 21, 2014

MASHABIKI WALILIA PENZI LA RAY, JOHARI

MASHABIKI wa sinema za Kibongo wamefunguka kuwa wanapenda uhusiano waliouita wa kimapenzi kati ya Wakurugenzi wa RJ Company, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Blandina Chagula ‘Johari’.

Thursday, May 15, 2014

‘UCHAWI’ WATAJWA PENZI LA RAY, CHUCHU

Stori: SHAKOOR JONGO NA MUSA MATEJA
‘UCHAWI’ umetajwa kwenye mapenzi ya staa wa filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ na ubavu wake wa sasa, Chuchu Hans.
Staa wa filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ akiwa na mpenzi wake Chuchu Hans.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu, mapenzi ya Ray kwa Chuchu ni makubwa sana kiasi kwamba hayawezi kuwa ya hivihivi tu kwani msichana huyo ni mtoto wa Kitanga anayejua jinsi ya kumshika mwanaume kama Ray.

Saturday, March 15, 2014

HATIMAYE JOHARI KUOLEWA!

KILA jambo na wakati wake! Hatimaye staa wa filamu za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’ yuko kwenye mwanga wa maisha ya ndoa kufuatia Kiongozi wa Kundi la Mtanashati, Ostaz Juma Namusoma kuweka wazi uhusiano wao wa kimapenzi huku akisema ana mpango wa kumuoa kabisa, Risasi Jumamosi linakupa zaidi.

Staa wa filamu za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’.
YAMEKUJAJE?
Hivi karibuni katika mtandao wa kijamii wa Instagram, Ostaz alitumbukiza picha inayomwonesha yeye akiwa katika ‘pozi nono’ na Johari huku akimsifu mwandani wake huyo. Hali hiyo ilisababisha maswali kwa baadhi ya mashabiki wa Johari.
Risasi Jumamosi lilianzia hapo kuchimba hatua kwa hatua na kubaini kuwa, wawili hao wako ‘klozidi’ tangu kitambo hasa baada ya penzi bubu la Johari na staa mwenzake wa sinema za Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ kuparaganyika.
Kwa sasa Ray anadaiwa kutoka kimapenzi na mcheza filamu mwenzake, Chuchu Hans ambapo nao inadaiwa wako katika mikakati ya kufunga ndoa kama si pingu za maisha.

Johari na Ostaz Juma katika picha ya pamoja.
Chanzo chetu kimoja kilisema kuwa, Ostaz amekufa kimapenzi kwa Johari, ‘hakohoi, hanywi maji, halali usingizi’ na yuko tayari kwa ndoa itakayokuwa ya kifahari.
“Ukitazama hapo Johari hana kipingamizi, ingekuwa zamani angesema yuko na Ray kuna kikwazo cha yeye kuolewa na Ostaz, lakini kwa sasa kipi kitamzuia?” chanzo hicho kilipayuka.

Saturday, March 8, 2014

MASTAA WENYE NYOTA ZA NGONO!

Stori: Hamida Hassan na Gladness Mallya
Makubwa! Mtabiri maarufu Bongo, Maalim Hussein Yahya ameanika nyota za baadhi ya mastaa wa Bongo katika kipengele cha mapenzi au ngono, Risasi Jumamosi limesheheni.
Mtabiri maarufu Bongo, Maalim Hussein Yahya.
Akizungumza na mapaparazi wetu katikati ya wiki hii ofisini kwake Magomeni-Mwembechai jijini Dar, Maalim alitumia saa kadhaa kuangalia nyota ya mmoja baada ya mwingine na kueleza sifa zao katika sekta ya uhusiano na tendo la ndoa.
Wema Sepetu.
Baadhi ya mastaa alioweza kuwasoma nyota zao kirahisi ni pamoja na ‘kichaa’ wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, waigizaji Wema Sepetu, Vincent Kigosi ‘Ray’, Aunt Ezekiel, Steven Jacob ‘JB’, Jacqueline Wolper, Blandina Chagula ‘Johari’ na wengine.
ALIANZA NA WEMA
Akimzungumzia Wema aliyezaliwa Septemba 28, Maalim alisema nyota yake ni Mizani hivyo ana tabia zifuatazo katika masuala ya mapenzi:
“Kwanza yeye (Wema) na Diamond nyota yao ni moja hivyo mambo yao mengi yanafanana.
“Wanapenda kuwa kwenye ulimwengu wa mapenzi na mahaba wakati wote. Wanathamini sana masuala ya ngono kuliko maisha mengine.”
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Wema Sepetu katika pozi la kimahaba.
NDOA NA DIAMOND
“Hawa watakuwa watu wa kuachana na kurudiana mpaka watakapofunga ndoa ya kifahari hapo baadaye.
“Kuhusu mambo mengine kinyota ni kwamba wana sifa ya uongozi, wanapenda kuwa huru na kujitegemea. Wanapenda kuheshimika kwenye jamii na ni wacheshi, wana hekima na diplomasia.”
Vincent Kigosi ‘Ray’.
KUHUSU RAY
Kwa upande wake Ray ambaye amezaliwa Mei 28, Maalim alisema nyota yake ni Mapacha.
Akimchambua kinyota kuhusu masuala ya mapenzi, alisema:
“Akimpenda mwanamke ana uwezo wa kumpa chochote, kimawazo na kila kitu, anaweza hata kuhamia nyumbani kwa mwanamke huyo.
Vincent Kigosi ‘Ray’ akiwa na mpenzi wake Chuchu Hans.
“Ila ni mtu anayechoka haraka na hawezi kudumu kwa muda mrefu kwenye penzi na mwanamke mmoja tu.
“Pia anapenda kuwa na mapenzi ya siri siku zote. Hata akioa ni lazima ataendelea kuwa na mwanamke wa nje ‘nyumba ndogo’.

Saturday, February 22, 2014

CHUCHU, RAY WAMMWAGIA MINOTI CHOKY

WAPENDANAO, Chuchu Hans na Vincent Kigosi ‘Ray’ waligeuka mapedeshee kwa muda baada ya kummwagia fedha za kutosha, Mkuruguenzi wa Bendi ya Extra Bongo, Ally Choky.

Chuchu Hans na Vincent Kigosi ‘Ray’ katika pozi.
Tukio hilo lililoteka hisia za mashabiki wa bendi hiyo lilitokea juzikati katika Ukumbi wa Meeda, Dar ambapo Ray aliyekuwa ameambatana na ubavu wake huo, walionekana ukumbini humo wakipata vinywaji, baadaye muda ulivyozidi kwenda, wakanogewa na rhumba la Choky na kuanza kutunza. “Mh! Leo mtu na mtuwe wamegeuka mapedeshee, wanamwaga minoti ya kufa mtu, hata hazihesabiki…hatari,” alisikika shabiki mmoja aliyeshuhudia tukio hilo.

Saturday, February 15, 2014

RAY, CHUCHU HANS NI PIGO!

Stori: Gladness Mallya na Hamida Hassan
Ni pigo kubwa! Ile ndoa inayodaiwa kukaribia kufungwa kati ya nyota wa filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Miss Tanga 2006 aliye pia msanii wa filamu Bongo, Chuchu Hans imepingwa isifungwe mpaka mambo f’lani yakae  sawa.
Ray na Chuchu wakijiachia.
Kwa mujibu wa mtonyaji wetu, Ray na Chuchu wako mbioni kufunga ndoa wakati wowote kuanzi Mei, mwaka huu, lakini mjadala mzito uliopo mbele yao kwa sasa ni uhalali wake.
“Unajua wanachofahamu wao (Ray na Chuchu) wanaweza kufunga ndoa kwa ulaini kabisa, lakini ukweli ni kwamba kuna ugumu mkubwa.
UGUMU ULIPO
“Kanisa analosali Ray, viongozi wanasema wao si wa dunia hii mpaka wakubali kufunga ndoa ambayo mmoja wa wahusika ana ndoa yake,” kilisema chanzo hicho.
Kikaendelea: “Kwa hiyo kama wako tayari kufunga ndoa hiyo lazima Chuchu akubali kubadili dini yeye ndipo ataruhusiwa kungia kanisani kufungishwa ndoa.”
Mtume na Nabii Onesmo Ndegi.
KANISA LA RAY
Juzi Alhamisi, Risasi Jumamosi lilifunga safari hadi kwenye Kanisa la Living Water-Makuti Kawe, Dar ambako mpaka mwaka uliopita magazeti pendwa yaliandika Ray anaabudu huko.
Lengo la Risasi Jumamosi lilikuwa kuonana na Mtume na Nabii Onesmo Ndegi lakini hakuwepo ofisini, ila msaidizi wake mmoja alipopatikana alikiri kumfahamu Ray.
Msaidizi:  Ray alishasali hapa, lakini sijamwona siku nyingi, sijui ana matatizo gani?
Risasi Jumamosi: “Oke, tukiacha hilo la kutofika kwa siku nyingi. Lililopo sasa hivi ni kwamba anataka kufunga ndoa na dada mmoja anaitwa Chuchu Hans ambaye ana ndoa tayari, hajaachika na mumewe yu hai. Unasemaje kuhusu hilo?
Msaidizi: “Sisi hatuamini katika kuachana. Kama alishafunga ndoa na mume yupo hai, hao wametengana tu, lakini ndoa yao ipo.
“Huyo mwanamke alishajifunga, kifungo chake kitatenguliwa pale tu mumewe atakapoondoka duniani (kifo).
KANISA LA MTAKATIFU MAXIMILIAN KOLBE
Baada ya kuondoka kanisani hapo, mapaparazi wetu walikwenda Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Maximilian Kolbe, Mwenge, Dar es Salaam.
Risasi Jumamosi liliambiwa Baba Paroko hakuwepo kwa wakati huo, lakini muumini mmoja aliyesema yeye ni mwalimu alipoulizwa kuhusu nafasi ya Ray kufunga ndoa na Chuchu Hans alisema:
“Maandiko yako wazi. Sasa kama huyo mwanamke ana mume wake tena mmesema yupo nje ya nchi, siku akija si atamshika ugoni kwa mke wake?
“Huwezi kufunga ndoa kama bado una ndoa. Mungu hajaagiza hivyo. Ndiyo maana sisi (Wakristo) huwa tunatoa siku ishirini na moja za kutangaza ndoa ili kama kuna mwenye pingamizi ajitokeze na kulianika.
“Watu waongo siku hizi. Wapo wachumba wanakuja kuandikisha ndoa kumbe mmoja bado yupo kwenye ndoa halali.”
 
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum.
IMANI YA KIISLAM INASEMAJE?
Mapaparazi wetu hawakuchoka, walimtafuta Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Musa Salum ambaye kuhusu Ray na Chuchu kufunga ndoa alifunguka hivi:
“Kama Chuchu ni Muislam, itabidi Ray abadili dini awe Muislam, si vinginevyo.”
Risasi Jumamosi: Chuchu alifunga ndoa Bomani na mume Mkristo, ila yeye Muislam. Inakuwaje hapo?
Sheke Mkuu: “Itakubalika kama Ray atabadili dini tu, maana hiyo ndiyo ya Bomani, Kiislam siyo.”
Blandina Chagula ‘Johari’.
JOHARI, MAINDA WAPATANA
‘Johari’ ambaye ni Blandina Chagula na ‘Mainda’ mwenye uhalisia wa jina la Ruth Suka (zamani Mwanaid), wawili hao sasa ni mashosti wakubwa baada ya kuwa na bifu la miaka 8 kisa kikitajwa  kuwa ni ‘kaka mkubwa’ huyo (Ray) kuwachanganya kimapenzi.
Kwa mujibu wa chanzo, mastaa hao wanaotamba kwenye filamu za Bongo kwa miaka mingi wameamua kumaliza tofauti zao huku wengi wakitafsiri kuwa, wanashikamana kwa sababu ya  kuumaliza uhusiano wa Chuchu na Ray. Haikufafanuliwa.
Mainda.
MADAI MENGINE
Pia ilidaiwa kuwa, Mainda aliamua kumaliza bifu na Johari kwa sababu mchungaji wake alimtaka  kufanya hivyo.
“Niliwakuta kambini wakishuti filamu, Mainda akaniambia aliitwa kushiriki filamu hiyo kama mpambaji, Johari yeye amecheza baadhi ya  vipande ndipo Mainda akamtaka mwenzake wamalize tofauti zao,” kisema chanzo chetu.
Hivi karibuni, Risasi Jumamosi liliinasa picha iliyotundikwa mtandaoni na Mainda akimwonesha yeye, Johari na Mtangazaji wa StarTV, Sauda Mwilima.
Mainda aliisindikiza picha hiyo na maneno  yaliyosema: “Nimejifunza kitu katika maisha, kusamehe.”
KAKA MKUBWA RAY
Juzi, Risasi Jumamosi lilimpigia simu ya mkononi Ray lakini hakupokea. Akatumiwa meseji, hakujibu!
CHUCHU HANS
Baada ya kusomewa mashitaka yote, alijibu kwa ufupi: “Sina cha kuongea.”
JOHARI
Johari naye hakupokea simu yake ya mkononi licha ya kuita kwa muda mrefu na kukatika kisha kupigwa tena. Akatumiwa meseji, hakujibu!
MAINDA
Na yeye simu yake iliita sana bila kupokelewa, akatumiwa meseji, hakujibu!
CHANZO NI GPL

Saturday, February 1, 2014

MAMA JOHARI AMFUMUA RAY

Makubwa! Kwa mara kwanza mama mzazi wa mwigizaji mkongwe Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ ambaye hakupenda jina lichorwe gazetini ameibuka na kumfumua staa wa filamu ‘mbia’ wa mwanaye, Vincent Kigosi ‘Ray’.
Mwigizaji mkongwe Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’.
Akizungumza na mapaparazi wetu katika mahojiano maalum nyumbani kwake, Ubungo External, Dar, wiki hii, mama Johari alifunguka kuwa hamjui wala hajawahi kumuona Ray ambaye ni mkurugenzi mwenza wa Johari. Ndiyo wamiliki wa kampuni ya kufyatua filamu ya RJ Productions.
Mama Johari ambaye pia ana makazi yake mkoani Shinyanga alisema alitua jijini Dar kwa matibabu ya presha.
Vincent Kigosi ‘Ray’.
Baada ya kumjulia hali, mapaparazi wetu walitaka kujua mama huyo anamzungumziaje Ray ambaye amekuwa akifanya kazi kwa karibu na bintiye na kwamba ilishasemekana ni wapenzi.

Sunday, January 12, 2014

MASTAA WABARIKI RAY, CHUCHU KUOANA

BAADA ya kuzagaa kwa fununu za chini ya kapeti kuwa mastaa wa sinema za Kibongo, Vincent Kigosi na Chuchu Hans kutarajia kufunga ndoa, wenzao wa Bongo Movie wameonesha hadharani kuwa wanaiunga mkono ndoa hiyo na kutoa baraka zao.
Ray na Chuchu Hans wakiwa katika pozi la kimahaba.
Tukio hilo lilijidhihirisha wazi hivi karibuni katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar katika uchaguzi wa viongozi wa Klabu ya Bongo Movie ambapo Ray ambaye alikuwa mwenyekiti mstaafu wa klabu hiyo, aliambatana na ‘bebi’ wake huyo (Chuchu) na kupozi katika staili ya ‘mista na misezi’.

Bila kupepesa macho, kwa nyakati tofauti mastaa hao waliokuwa wakifuatilia uchaguzi huo, wa kiume walimuita Chuchu shemeji huku wa kike wakimuita Chuchu wifi ambapo bibie aliitikia bila hiyana.

Thursday, January 2, 2014

RAY AONA AIBU KUMBUSU LULU

STAA wa filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ amesema alipata wakati mgumu kumpanga mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ kwenye filamu yake ambayo walipaswa kucheza kama wapenzi kwa kuhofia kumbusu.
Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Akizungumza katika kituo kimoja cha runinga cha jijini Dar hivi karibuni, Ray alisema licha ya kuwa Lulu alikuwa anastahili kuigiza katika sinema ya Woman Principle miaka kadhaa iliyopita, aliona Lulu anafaa kutokana na umakini wake lakini akaona bora amchukue Miss Tanzania namba 3, 2003, Nargis Mohammed kwa kuhofia kupata aibu ya kuoneshana malavidavi na Lulu.
 
Vincent Kigosi ‘Ray’.
“Lulu alikuwa na uwezo wa kumudu kipengele hicho, kipindi hicho alikuwa mdogo sana, niliona ni jambo la aibu kidogo kumbusu mdomoni mtoto mdogo kama yeye halafu ni kitu ambacho jamii itakaa ikitazame nikaona bora nimchukue Nagris, Lulu nikampa sini nyingine,” alisema Ray.
Aliongeza kuwa, kikubwa kilichomfanya avutiwe kucheza na Nagris ni kwa sababu ni mwanamke ambaye katulia na hana skendo hivyo itamuongezea heshima na mvuto wa kazi yake katika jamii.

Wednesday, November 20, 2013

MAINDA ATISHIWA KUUAWA


SIKU chache baada ya staa wa filamu za Kibongo, Ruth Suka ‘Mainda’ kufunguka  kuhusu mambo mazito yaliyomo ndani ya tasnia ya filamu, staa huyo ameanza kupokea vitisho vya kukatishwa uhai wake.

Friday, September 6, 2013

BEHIND THE SCENES.RAY AND JACKLINE WOLPER STARS IN A NEW MOVIE

Vicent Kigosi(Ray) and Swahili movies' sexy diva Jackline Wolper will be seen in a new flick. The two megastars in Swahiliwood have already shared screen space together in some movies including Surprise and currently they are shooting their new project by Rj Company. Look behind the scenes of the movie..............

                                    Ray and Wolper on set

Thursday, August 22, 2013

MASTAA HAWA... MAJINA YAO YA ASILI ‘YAMEKUFA’

KWA kawaida binadamu yeyote huzaliwa na kubatizwa jina ambalo hulitumia katika masomo na hata kazi yake.
 

Tofauti na ilivyo katika fani nyingine, wasanii wamekuwa wakijibatiza majina ya ziada (a.k.a). Mbaya zaidi, majina hayo huwa yanaanza kama utani lakini inafika wakati msanii husika analizoea jina hilo jipya na kulifanya kuwa kama rasmi.
Leo Amani linakuletea orodha ya baadhi ya mastaa ambao majina waliyopewa na wazazi wao ‘yamekufa’, hawayatumii kabisa:
LULU
Jina lake halisi ni Elizabeth Michael, Lulu lilizoeleka kupitia tasnia ya uigizaji. Alianza kulitumia wakati alipojiunga na Kundi la Sanaa la Kaole.
Hadi leo hii, siyo rahisi kabisa mtu kutokea na kumuita jina la Elizabeth, wengi wanamfahamu kwa jina la Lulu.

RAY
Ray ndiyo jina ambalo limezoeleka na wengi. Vincent Kigosi alilopewa na wazazi wake ni kama limekufa. Kwa zaidi ya miaka kumi sasa tangu alipokuwa kwenye Kundi la Sanaa la Kaole hadi sasa.
Jina la Ray ndiyo watu wanalolifahamu zaidi ingawa hivi karibuni baadhi ya wasanii wenzake wamekuwa wakijaribu kumuita Vincent ili kurudisha uhai wa jina hilo.

JOHARI
Jina lake halisi ni Blandina Chagula. Johari lilizaliwa kwenye Tamthiliya iliyobeba taito ya jina hilo. Akiwa katika Kundi la Kaole, alianza kujiita Blandy, baadaye alibadilisha jina hilo na kuwa Johari walipoingiza tamthiliya hiyo ambayo pia ilizaa filamu.
“Kuna wakati huwa najuta kutumia jina la a.k.a ambalo limefunika kabisa jina langu la asili,” anasema Johari.

DK. CHENI
Ameanza gemu kitambo, tangu Kundi la Splended.  Jina alilopewa na wazazi wake ni Mahsein Awadhi, kwa sasa limekufa. Hakuna anayelitumia, hata yeye mwenyewe.
Jina hilo lilizaliwa baada ya mazoea yake ya kupenda kuvaa cheni kubwa kwenye michezo iliyokuwa ikirushwa Runingani, kwa sasa wengi wanashindwa hata kulitamka jina lake.

Saturday, July 6, 2013

AUNT, WOLPER: TUTAWAUA WABUNGE WENU

Aunt Ezekiel.
Na Mwandishi Wetu
NI mshikemshike kwa ajili ya Tamasha la Matumaini, Jumapili hii kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar ambapo mastaa wa filamu za Kibongo wanaoshiriki ndondi na wabunge, Aunt Ezekiel na Jacqueline Wolper wametamba kuwamaliza waheshimiwa hao.
 
                                                                   Jacqueline Wolper.
AUNT VS ESTER BULAYA
Aunt ambaye atazichapa na Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Mara (CCM), Ester Bulaya ameapa kuwa lazima siku hiyo ‘amuue’ mheshimiwa huyo kwa madai kuwa kwa sasa yupo fiti baada ya kurejea kutoka kambini, Dubai.
Alisema kuwa amepata mazoezi ya nguvu ya kurusha na kupangua ngumi kutoka kwa mwalimu wake, Abdul Al-Mohd ambaye amempa mbinu zote za kummaliza mbunge huyo katika raundi za mwanzo.
 
                                                                          Ester Bulaya.
“Nipo fiti sana, najua mheshimiwa Ester ni mtu wa Mara kwa wakorofi na ana hasira lakini hilo halinipi shida, cha msingi mashabiki wangu waje kushuhudia nikimmaliza mtu,” alisema Aunt na kuongeza:
“Ester ni mwanasiasa mzuri na ana mazoea na majukwaa ya siasa lakini mimi nataka niwathibitishie watu kuwa naweza kumiliki ulingo vilivyo kama ninavyokuwa stejini.
 
                                                                    Halima Mdee.
“Kazi ni moja tu keshokutwa (Jumapili) kwenye Uwanja wa Taifa, natoa tahadhari kuwa ‘nitamuua’ mbunge wenu. Nawaahidi mashabiki wangu na watu wote ushindi ‘so’ wote tukusanyike tupate burudani na kuchangia elimu yetu.”

Saturday, June 29, 2013

Kitu kipya toka kwa Wolper na Ray - waigiza kama mke na mume.

Vincent Kigosi ama Ray na mrembo Jacqueline Wolper , wapo location wakishoot movie yao mpya ambayo bado hatujaweza kupata jina lake mpaka sasa kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu.
 Kitu kipya toka kwa Wolper na Ray - waigiza kama mke na mume. Angalia picha
Katika picha picha hizo walizoziweka kwenye akaunti zao za mtandao mmoja wa kijamii nchini inaonekana wanaigiza kama mke na mume.

“Siye tena kazini new movie, mke wa mtu me hapa nacheza.me en broo ray mwenyezi mungu kua nasi mwanzo hadi tumalize inshaalah ,” ameandika Wolper kwenye moja picha hizo.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate