NDIYO habari ya ‘mujini’ kwa sasa, kwamba
staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul Juma ‘Diamond Platnumz’ na mwandani
wake, mtangazaji wa kituo cha runinga cha DTV, Penniel Mungilwa ‘Penny’
wamemwagana, Risasi Jumamosi limemwagiwa upupu.
Penniel Mungilwa ‘Penny’ na Nasibu Abdul Juma ‘Diamond Platnumz’ wakiwa pamoja katika pozi.
KAMA UTANI, WEMA ATAJWA
Kwa sharti la kutotajwa mahali popote, ‘mtonyaji’ wetu ambaye ni mtu wa
karibu wa wawili hao aliliambia gazeti hili kuwa chanzo cha Diamond na
Penny kuingia kwenye listi ya ‘zilipendwa’ kilianza kama utani.
Awali ilidaiwa kuwa kila mmoja amekuwa akijiona mwenye thamani mbele ya mwenzake huku Wema Sepetu naye akidaiwa kuwa chanzo.
Nasibu Abdul Juma ‘Diamond Platnumz’ akiwa na Wema Sepetu.
“Hakuna penzi tena kati yao, wameachana na kila mmoja yuko kivyake.
“Walianza kama utani, unajua wale kila mmoja anajiona yuko juu kuliko
mwenzake, lakini kitendo cha Diamond kuripotiwa kutoka na wanawake
tofauti mara kwa mara hasa Wema, kimemchosha Penny ndiyo maana ameamua
kujiweka pembeni kuepuka msongamano.
“Kupangwa kama mafungu ya nyanya inahusu?” alihoji ‘kikulacho’ huyo ambaye ni rafiki wa Diamond.
RISASI MZIGONI
Baada ya kutojiridhisha moja kwa moja na taarifa za awali kutoka kwa
rafiki huyo, timu ya gazeti hili kwa kuwatumia ‘wahangaikaji’ wake
maalum, iliingia mzigoni kupeleleza ukweli juu ya tetesi hizo.
Watu
kadhaa walio chini ya Wasafi Classic Baby (WCB) ambayo rais wake ni
Diamond walihojiwa ambapo majibu yalikuwa yaleyale kwamba, kwa sasa
Diamond na Penny imebaki stori!
SHAKA ILIPOANZIA
Wakati timu yetu ikiendelea na uchunguzi wake makini juu ya uvumi huo,
hivi karibuni Diamond alionekana ‘singo’ kwenye pati ya kusherehekea
siku ya kuzaliwa ya ‘dada wa mjini’, Halima Haroun ‘ Halima Kimwana’
ambayo aliiandaa Diamond.
Minong’ono ya kuhoji kutoonekana kwa Penny
ilisikika ndani ya Ukumbi wa Business Park, Kijitonyama jijini Dar
ilikofanyikia pati hiyo iliyojaa vitendo vya ufuska.
“Haiwezekani leo rais (Diamond) akajiachia peke yake bila Penny. Si kawaida ya Diamond.
“Kwa vyovyote watakuwa wameshamwagana kwa sababu kwenye pati zote huwa
wanakuwa pamoja tangu walipoanza uhusiano wa kimapenzi,” alisikika mmoja
wa waalikwa katika sherehe hiyo.
Katika tukio hilo, Penny alipigiwa simu na
paparazi wetu na kujibu kwa kifupi: “Naumwa. Halafu si lazima nije kwani
kila mtu ana ratiba zake.”
Penniel Mungilwa ‘Penny’.
PENNY KIZIMBANI TENA Baada ya kukamilisha
udadisi huo kupitia kwa watu wao wa karibu, gazeti hili lilianza na
Penny kwa kumuuliza undani juu ya habari hiyo lakini alionekana kuwa
‘mzito’ kwa kutoingia ndani kulizungumzia sakata hilo huku akiahidi
kulifungukia muda wowote kuanzia sasa.
“Kwa sasa sina cha kuzungumza
juu ya hilo, nitalizungumzia muda wowote tena si siku nyingi zijazo,
lakini si leo, tafadhali sana,” alijibu Penny kwa kifupi na sauti ya
chini iliyojaa uchovu.
Paparazi: “Hebu nisaidie, mko wote au hamko wote?”
Penny: “Nimesema sitoweza kusema lolote kwa leo, subirini.”
Nasibu Abdul Juma ‘Diamond Platnumz’. DIAMOND KIMYA
Alipotafutwa Diamond kwa njia ya simu yake ya kiganjani, hakupokea
licha ya kupigiwa mara kadhaa kwa namba zake zote. Akatumiwa meseji
yenye maelezo yote, hakujibu.