EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA
Showing posts with label JENNIFER KYAKA (ODAMA). Show all posts
Showing posts with label JENNIFER KYAKA (ODAMA). Show all posts

Saturday, February 21, 2015

ODAMA AFUNGUKA KUCHANGIA WANAUME!

Laurent Samatta
MAMBO yanazidi kunoga ndani ya safu hii ya Sindano 5 za moto, kutokana na maombi yenu, leo tumemleta kwenu mwigizaji Jeniffer Kyaka ‘Odama’, tiririka naye:
Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Jeniffer Kyaka ‘Odama’.
Paparazi: Mambo vipi Odama! Tuanze moja kwa moja na swali la kwanza, hivi kwa sasa una mpenzi? Mbona hatumjui?Odama: Mambo poa! Mpenzi ninaye, nampenda muda bado wa kumuanika.Paparazi: Ulishawahi kuchangia bwana na mwanamke mwingine katika maisha yako?
Odama: Hapana, sina kumbukumbu hiyo.

Monday, August 18, 2014

ODAMA AMKANA PEDESHEE

Stori: Mayasa Mariwata
Si kweli! Mtoto mzuri Bongo Movies, Jennifer Kyaka ‘Odama’ amekanusha vikali madai ya kutembea na pedeshee mmoja anayedaiwa kuwa ni mmiliki wa baa moja iliyopo maeneo ya River-Side, Ubungo jijini Dar.
Mtoto mzuri Bongo Movies, Jennifer Kyaka ‘Odama'.
Baada ya kusomewa madai hayo ambayo yamesambaa kwenye mitandao ya kijamii, Odama alikanusha vilivyo na kusema wanamsingizia tu.“Hee! Mbona huyo mtu wala simjui, ndiyo kwanza nazisikia hizo habari wakizikuza kwenye mitandao,” alisema Odama.

Monday, March 24, 2014

ODAMA APIGA MZIGO KITUMBO NDII

MTOTO mzuri Bongo Movies, Jennifer Kyaka ‘Odama’ amesema japokuwa ni mjamzito lakini bado ana kasi zaidi katika kufanya kazi zake za filamu.
Jennifer Kyaka ‘Odama’.
Akipiga stori na paparazi wetu, Odama alisema watu wengi wanaamini unapokuwa mjamzito unaacha shughuli zako lakini kwake mambo ni tofauti, kazi kama kawaida.
“Mimi mzigo hapa naendelea kama kawaida wala mimba siyo kigezo cha kusubirisha  mambo yangu, kwanza naona ndiyo imenipa nguvu ya kufanya kazi zangu, nimekamilisha tayari kazi mpya, naiachia March 28 inaitwa Jicho Langu,” alisema Odama.

Saturday, January 25, 2014

KUMBE MIMBA YA ODAMA NI YA KIGOGO SERIKALINI!

Jennifer Kyaka ‘Odama’.
Stori: Musa Mateja
Imevuja! Kumbe kile ‘kibendi’ cha staa wa sinema za Kibongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’ ni cha kigogo mmoja serikalini na ndiyo sababu kubwa ya mwigizaji huyo kufanya siri nzito juu ya ujauzito huo.
Kama mbu aenezavyo ugonjwa wa malaria, ndivyo rafiki wa karibu na msanii huyo alivyotunyetishia juu ya usiri huo huku akisisitiza hifadhi ya jina.
Akizungumza kwa njia ya simu na mwandishi wetu mwanzoni mwa wiki hii, rafiki huyo alisema kwa sauti tulivu kuwa mimba ya Odama ni ya bosi mkubwa wa moja ya wizara nyeti hapa nchini (jina na wizara vinavunda kwenye droo zetu) na kwamba moja kati ya masharti magumu aliyompa ni kuhakikisha jambo hilo linabaki kuwa siri hadi Yesu atakaporudi.
 
Ilisemekana kuwa usiri huo unatokana na madai kwamba kigogo huyo ni mume wa mtu.
Akiendelea kumwaga mchele kwenye kuku wengi, ‘kikulacho’ huyo alisema licha ya Odama kupata huduma zote bora anazostahili mjamzito lakini hana raha kwani furaha ya mjamzito ni pamoja na kumnadi mhusika wa ‘mzigo’ jambo ambalo limekuwa likimnyima raha.

Saturday, November 16, 2013

MCHANGO WA SEND OFF WAWAGOMBANISHA SHAMSA, ODAMA


KATIKA hali ya kushangaza, waigizaji wa filamu Bongo, Shamsa Ford na Jennifer Kyaka ‘Odama’ wamedaiwa kugombana kwa sababu ya michango ya send off.
Jennifer Kyaka ‘Odama’.
Chanzo makini kilicho karibu na wasanii hao kilisema kuwa, Odama alikuwa na shughuli ya sendoff ya mdogo wake ambapo wasanii mbalimbali waliombwa michango lakini Shamsa hakutuma kwa wakati na kusababisha bifu kati yao.

Saturday, September 21, 2013

Odama: Sijahongwa vifaa vya kisasa kwa ajili ya utengenezaji filamu.

Dar es Salaam. 
Miezi kadhaa ikiwa imepita tangu mtayarishaji na mwigizaji wa filamu nchini Jennifer Kyaka ‘Odama’ kuanza kumiliki vifaa vya kisasa kwa ajili ya utengenezaji filamu, amesema kitu kinachomuumiza zaidi ni kwa baadhi ya watayarishaji kuamini kwamba fedha wanazotumia waigizaji wa kike kuandalia filamu wamehongwa.

 
Akizungumza Odama alisema hata maendeleo yake hayajatokana na kuhongwa.


Anaongeza kuwa watayarishaji wa kike wamekuwa na changamoto nyingi sana katika uandaaji wa filamu nchini, lakini yeye ni mwanamke wa shoka kwani anajiamini kwa kile anachokifanya.


“Kinachoniumiza ni hawa wenzetu kuamini kuwa watayarishaji wa kike fedha zao za kupewa na hawana uchungu nazo, hata wakipatana na wasanii kucheza katika filamu zao gharama huwa kubwa tofauti na waandaaji wa kiume wanaonekana wahangaikaji,” alisema.


Thursday, August 22, 2013

MASTAA HAWA... MAJINA YAO YA ASILI ‘YAMEKUFA’

KWA kawaida binadamu yeyote huzaliwa na kubatizwa jina ambalo hulitumia katika masomo na hata kazi yake.
 

Tofauti na ilivyo katika fani nyingine, wasanii wamekuwa wakijibatiza majina ya ziada (a.k.a). Mbaya zaidi, majina hayo huwa yanaanza kama utani lakini inafika wakati msanii husika analizoea jina hilo jipya na kulifanya kuwa kama rasmi.
Leo Amani linakuletea orodha ya baadhi ya mastaa ambao majina waliyopewa na wazazi wao ‘yamekufa’, hawayatumii kabisa:
LULU
Jina lake halisi ni Elizabeth Michael, Lulu lilizoeleka kupitia tasnia ya uigizaji. Alianza kulitumia wakati alipojiunga na Kundi la Sanaa la Kaole.
Hadi leo hii, siyo rahisi kabisa mtu kutokea na kumuita jina la Elizabeth, wengi wanamfahamu kwa jina la Lulu.

RAY
Ray ndiyo jina ambalo limezoeleka na wengi. Vincent Kigosi alilopewa na wazazi wake ni kama limekufa. Kwa zaidi ya miaka kumi sasa tangu alipokuwa kwenye Kundi la Sanaa la Kaole hadi sasa.
Jina la Ray ndiyo watu wanalolifahamu zaidi ingawa hivi karibuni baadhi ya wasanii wenzake wamekuwa wakijaribu kumuita Vincent ili kurudisha uhai wa jina hilo.

JOHARI
Jina lake halisi ni Blandina Chagula. Johari lilizaliwa kwenye Tamthiliya iliyobeba taito ya jina hilo. Akiwa katika Kundi la Kaole, alianza kujiita Blandy, baadaye alibadilisha jina hilo na kuwa Johari walipoingiza tamthiliya hiyo ambayo pia ilizaa filamu.
“Kuna wakati huwa najuta kutumia jina la a.k.a ambalo limefunika kabisa jina langu la asili,” anasema Johari.

DK. CHENI
Ameanza gemu kitambo, tangu Kundi la Splended.  Jina alilopewa na wazazi wake ni Mahsein Awadhi, kwa sasa limekufa. Hakuna anayelitumia, hata yeye mwenyewe.
Jina hilo lilizaliwa baada ya mazoea yake ya kupenda kuvaa cheni kubwa kwenye michezo iliyokuwa ikirushwa Runingani, kwa sasa wengi wanashindwa hata kulitamka jina lake.

Friday, July 26, 2013

Baada ya kusakamwa kuwa huwa anajisingizia kwenda Ulaya, Odama aamua kutoa ushahidi wa picha, Zitazame hapa

Baada ya wadau mbalimbali kuanza kuhoji kuhusu uhalisia wa safari za mwigizaji Jennifer Kyaka (Odama) kwenda ulaya ambaye picha zake kadhaa zilizotolewa mtandaoni wiki chache zilizopita zikimtuhumu kuwa huwa haendi nje ya nchi bali anakuwepo nchini kwa lengo la kutafuta “kiki” na kutengezeza picha hizo kwa program maalumu ya kompyuta, hatimaye jana kupitia mtandao mmoja wa kijamii aliweka picha zake mpya zinazomuonesha nchini Qatar katika maduka mbalimbali na kwenye uwanja wa ndege wa nchi hiyo.

Picha hizi zimekuja kama ushahidi na majibu ya mwaswali yaliyokuwa yakiulizwa na wadau wengi kuhusu mwanadada huyu. Tazama picha hizi hapo

Thursday, July 11, 2013

HUU NDO USHAHIDI IKIONYESHA KUWA ODAMA WA BONGO MOVIE HUTOA PICHA ZA UONGO KUA YUPO NJE YA NCHI. TAZAMA PICHA HIZI UJIONEE MWENYEWE.

Habari na Bongo Movies.com

EDITOR WA PICHA HII ALISAHAU KUKATA VIZURI NA KUONDOA BACKGROUND NYEUPE KWENYE ENEO LA NYWELE LILILOZUNGUSHIWA DUARA
Kuna habari tumeletewa na msomaji wa tovuti yetu ya bongo movies kumhusu mwanadada wetu muigizaji wa Filamu aliyepata tuzo hivi karibuni, Jennifer Kyaka al-maarufu kama Odama kuhusu safari zake za kwenda nje ya nchi.

Habari au tuhuma hizi tuziite, zinasema kuwa mwanadada huyo huwa haendi nje ya nchi kama anavyowaambia fans wake kupitia blog yake ya odama1.blogspot.com kuwa anasafiri kwenda nje kikazi zaidi, na badala yake inasememekana eti huwa anabaki hapa hapa nchini akizuga yupo nje ya nchi lengo ni kutafuta “KIKI” ama umaarufu kama watoto wa mjini wanavyosema.

Mdau aliyetutumia habari hizi amesema kuwa ana ushahidi wa kutosha na katutumia picha mbalimbali toka kwenye mtandao mmoja wa kijamii ambako staa huyo yupo zikimuonesha akiwa maeneo mbalimbali ya “duniani huko” ambayo kwa kuangalia picha hizo anasema kuwa ni feki na zimetengenezwa kwa kutumia teknolojia tuu ya ku-“edit” picha maarufu kama “PHOTOSHOP
Swali ni je, hili suala ni la kweli? Tunaomba wadau wenye majibu na utaalamu wa picha watusaidie kwa kutazama picha hizi na kutuambia kama habari hii ina ukweli wowote.




KATIKA PICHA HII EDITOR KAKOSEA KULETA UHALISIA HAPO ODAMA KAWA MREFU SANA

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate