EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA
Showing posts with label AGNESS MASOGANGE. Show all posts
Showing posts with label AGNESS MASOGANGE. Show all posts

Monday, March 16, 2015

MASOGANGE ASHTUSHWA NA USHINDI WA MAKALIO YAKE

MODO maarufu Bongo, Agness Gerad ‘Masogange’ ameshtushwa na ushindi wa makalio yake baada ya kutojua kama ametajwa kuwa ni mwanamke mwenye makalio mazuri Afrika Mashariki.
Modo maarufu Bongo, Agness Gerad ‘Masogange’.
Masogange alishinda nafasi hiyo kupitia utafiti uliofanywa na mtandao wa Media Take Out ambapo kwa kutumia vigezo vyao, walimwanika Masogange kuwa ndiye mwanamke pekee mwenye makalio bomba wakidai amejengeka vizuri zaidi.
“Daah! Mimi mwenyewe nilikuwa sijui, nashukuru kama wao wameona mimi ndiyo mwenye kiungo hicho muhimu cha kuvutia na bora kwa wanawake wengine wote,” alisema Masogange ambaye kwa sasa amehamishia makazi yake nchini Afrika Kusini.   

Friday, March 13, 2015

MAKALIO YAMPAISHA MASOGANGE MAREKANI


Staa  aliyejipatia umaarufu mkubwa kutokana na makalio yake, Agnes Gerald ‘Masogange’ sasa amepaa kimataifa zaidi na kuwa  gumzo hadi Marekani baada ya hivi karibuni mtandao mmoja wa watu maarufu nchini humo kumpa shavu.
Staa  aliyejipatia umaarufu mkubwa kutokana na makalio yake, Agnes Gerald ‘Masogange’.
Masogange aliripotiwa na mtandao wa Media Take Out na kumuelezea kuwa ni staa mwenye makalio makubwa barani Afrika akitokea Tanzania.Mbali na maelezo kibao ya kusifia wowowo lake, mtandao huo uliposti picha kibao za mwanadada huyo ambaye sasa anaishi Afrika Kusini akiweka mapozi tofauti ya kimitego.
Hata hivyo, baadhi waliponda maelezo hayo kwa kusema kuwa, Afrika ina mabinti wenye maumbo tata kuliko Masogange hivyo mtandao huo ungefanya uchunguzi kabla ya kuripoti habari hiyo.

Friday, January 23, 2015

MASOGANGE AIBU TUPU SAUZ

Na Erick Evarist/Ijumaa
MIEZI michache tangu ahamishie makazi yake nchini Afrika Kusini, modo aliyetikisa Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ ametia aibu kutokana na kudaiwa ‘kujiuza’ kwa njia ya mtandao nchini humo.
Modo anayetikisa Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’.
Chanzo makini kilicho karibu na staa huyo kimepenyeza ubuyu kuwa, Masogange yupoyupo tu, kazi kujipiga picha za utupu na kuzitupia mtandaoni kana kwamba anatafuta wanaume.“Kimsingi hana kazi huku Sauz zaidi ya kuposti picha kwenye mtandao wa Instagram na anachanganya sana wanaume wenye pesa zao, si unajua tena mtoto kajaliwa shepu la maana.
“Ukitaka kuthibitisha hilo ninalokwambia, ingia katika akaunti yake utaona picha kibao za kihasara akiwa hotelini, kama siyo kutuaibisha na kujiaibisha mwenyewe ni nini?” kilihoji chanzo chetu.Agnes Gerald ‘Masogange’ akipozi.
Baada ya chanzo hicho kuvujisha ubuyu huo, paparazi wetu aliingia kwenye akaunti ya mrembo huyo na kujionea picha kibao zenye mapozi ya kihasara. Jitihada za kumpata ili azungumzie madai hayo hazikuzaa matunda kwani simu yake haikuwa hewani lakini katika maelezo yake kwenye mitandao ya kijamii amewahi kudai anasoma chuo ingawa haijajulikana ni chuo gani.

Saturday, December 20, 2014

MASOGANGE NA SKENDO YA UTAPELI

VIDEO Queen matata Bongo, Agnes Jerald ‘Masogange’ amefungua mdomo wake na kuwaka kuwa anachukizwa na tabia ya baadhi ya watu ambao wanatumia jina lake kutapeli kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook.Akizungumza na mwanahabari wetu,  Masogange alisema kuwa watu wanaotumia jina lake wakome
Video Queen matata Bongo, Agnes Jerald ‘Masogange’.
kwa sababu wanamjengea hisia tofauti kwa watu wakati yeye hanufaiki na chochote.
“Kwa kweli inauma sana mtu kutumia jina langu kwenye mitandao halafu halitumii kwa uzuri, kazi ni kuomba pesa kwa watu mbalimbali, jamani mimi situmii mtandao wa Facebook kabisa kwa hiyo watu wawe makini,” alisema Masogange.

Saturday, August 30, 2014

UCHUMBA WA MASOGANGE WATIBULIWA


Stori: Mwandishi Wetu
SIKU chache baada ya kupata uraia wa Afrika Kusini, uchumba wa Video Queen, Agnes Gerald ‘Masogange’ na mpenzi wake, Louis Dolnard umetibuliwa.
Video Queen, Agnes Gerald ‘Masogange’
Hali hiyo ilijiri kutokana na madai kuwa kuna wanaume wamepeleka maneno ya kimbeya kwa mpenzi wake huyo yakiashiria kuwa mrembo huyo hajatulia.
Hata hivyo, Agnes amefunguka kuwa kamwe hawezi kuachana na mchumba wake huyo.
“Wanaume wengine sijui wapoje, wanapeleka maneno ya kimbeya kwa mchumba wangu sijui wanataka nini? Kwa taarifa yao siachiki ng’o,” alisema Masogange.

Wednesday, August 20, 2014

MNIGERIA AMPATIA MASOGANGE PASIPOTI YA SAUZI


Stori: Sifael Paul na Imelda Mtema
Habari ya mjini kwenye ulimwengu wa mastaa Bongo ni taarifa kuwa video queen maarufu, Agness Gerald ‘Masogange’ amepatiwa passport (pasipoti) ya kuishi nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’ na mwanaume anayedaiwa kuwa ni mfanyabiashara raia wa Nigeria.
Video queen maarufu, Agness Gerald ‘Masogange’.
MWANAUME KAMWINGIZA MKENGE?
Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika, ishu hiyo ambayo imekuja miezi kadhaa baada ya ule msala wa Masogange wa madawa ya kulevya ‘unga’ inadaiwa ‘imeinjiniwa’ na mwanaume huyo ambaye haijajulikana kama naye amechukua uraia wa Sauzi au la.

KWA NINI MKENGE?
Ilisemekana kwamba ni mkenge kwa sababu ili Masogange apate pasipoti hiyo, ilibidi aikane nchi yake ya kuzaliwa ya Tanzania. Sheria za uraia wa Bongo kwa sasa zinakataza mtu kuwa na uraia wa nchi mbili.

Agness Gerald ‘Masogange’ akipopzi na Louis Dolnard.
KIKAZI ZAIDI!
Awali, miezi kadhaa iliyopita ilielezwa kuwa Masogange alitimka Sauzi kwa mwanaume huyo ambaye anadaiwa kufanya naye ‘kazi’ (haikutajwa aina ya kazi) nchini humo.

Thursday, February 13, 2014

MASOGANGE: SITAKI KUTONGOZWA

VIDEO Queen matata Bongo, Agnes Gerald Waya ‘Masogange’ amewajia juu kundi kubwa la wanaume linalomtaka kimapenzi wakati wanatambua vyema kuwa ana mtu wake.
Agnes Gerald Waya ‘Masogange’.
Akipiga stori na paparazi wetu hivi karibuni, Masogange alisema tangu atoke Sauz aliponaswa kwa msala wa kusafirisha malighafi haramu, wanaume wakware wamekuwa wakimsaka kama fisi aliyeona mfupa kitu ambacho hakubaliani nacho.
“Sitaki kutongozwa kabisa, waniache. Kinachonikera zaidi wanaonitongoza wengi wanatambua kabisa nina mchumba wangu (Evance), watu wengine sijui wapoje!” alisema Masogange.



Friday, January 10, 2014

MASOGANGE ANASWA NA BWANA WA JACK

VIDEO Queen, Agnes Jerald ‘Masogange’ hivi karibuni alibambwa maeneo ya Sinza Kamanyola jijini Dar akijiachia na anayetajwa kuwa ni mpenzi wa Jack Patrick, Juma Khalid ‘Jux’.
Masogange akipozi na Jux.
Wawili hao walibambwa kwenye duka moja lililopo maeneo hayo baada ya Jux kutua kutoka China huku Agnes akionekana kama anayemfariji kwa tukio la Jack kunaswa na madawa ya kulevya.
http://api.ning.com/files/Iht4Psekqy0wttdXe*EsPRkqo*eRW*Qp69gUzbFS7smv8PTpbqof801LuB2JiAsnEHN0DmKCmtkMNQ9uNA-PB4Cq4PCBRIbh/jacknajux.jpg%3Fwidth%3D650Jux akiwa na mpenzi wake Jack Patrick.
Akiuzungumzia ukaribu wake na Jux, Masogange alisema: “Wala hakuna lolote kati yangu na yeye. Mimi na wale akina Jux pamoja na dada yake ni watu wangu wa karibu sana tunaojuana muda mrefu hivyo tulikuwa  tunabadilishana mawazo tu.”
Masogange akiwa na Jack.
Jux na Jack wamekuwa wakionekana katika mitaa ya China wakila bata huku kukiwa na madai kuwa ni wapenzi na kuonekana kwa Jux na Masogange wakijiachia kumeibua maswali mengi.
CHANZO NI GPL

Friday, December 13, 2013

MUONEKANO MPYA WA AGNES MASOGANGE


Pichani juu ni taswira za mpya za Video Queen wa Bongo, Agness Gerald 'Masogange' alizotupia kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Saturday, November 2, 2013

HUKUMU YA MASOGANGE YAPINGWA..MASOGANGE AJIFICHA



 Agness Gerald ‘Masogange’.
MAKAMANDA wa vitengo vya kudhibiti madawa ya kulevya kwa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wamemaliza kikao chao jana kujadili mustakabali wa uhalifu ikiwemo hukumu iliyotolewa kwa Mtanzania Agness Gerald ‘Masogange’ aliyekamatwa na malighafi haramu aina ya Ephedrine, Julai 5, 2013 nchini Afrika Kusini kwamba ni ndogo.
 
Taarifa za ndani kutoka Jeshi la Polisi Tanzania zimeeleza kuwa makamanda wa nchi hizo 15 walikutana jijini Arusha kuanzia Jumatatu iliyopita lengo kubwa likiwa kutokubaliana na adhabu zinazotolewa na baadhi ya nchi wanachama kwa wanaokutwa na hatia ya kukamatwa na madawa ya kulevya ‘unga’.

WALICHOJADILI
Kwa mujibu wa chanzo kilicho ndani ambacho kiliomba hifadhi ya jina kwa kuwa si msemaji, makamanda wa nchi hizo walikuwa na kibarua kizito cha kujadili mbinu mbalimbali za kukabiliana na uhalifu pamoja na hukumu inayotolewa kwa watu wanaokutwa na hatia ya kukamatwa na unga.
“Walijadili matukio mengi ya uhalifu likiwemo suala la madawa ya kulevya, wakajadili mbinu za kukomesha biashara hiyo haramu ili waweze kupata suluhisho la kudumu,” kilisema chanzo hicho.
                                                                           
WATAKA HUKUMU KWA NCHI WANACHAMA IWE MOJA
Ilidaiwa kuwa, malighafi aliyokamatwa nayo Masogange na mwenzake kwa nchi nyingine kifungo chake kinafanana na kile cha mtu aliyekamawa na madawa ya kulevya, lakini kwa Afrika Kusini ni cha chini sana.
Chanzo hicho kilizidi kumwaga data kuwa, miongoni mwa masuala yaliyokuwepo kwenye ajenda ni pamoja na umoja katika suala zima la hukumu hususan kwa watuhumiwa wa madawa ya kulevya kwani kumekuwa hakuna uwiano baina ya nchi moja na nyingine ndani ya Jumuiya hiyo.
“Tumeona ilivyokuwa kwa Masogange, nchi nyingi zimepinga kabisa ile hukumu kwani ilikuwa haifanani na kosa husika. Mtu anatozwa faini ya shilingi milioni nne na laki nane (Sh. milioni 4.8) kitu ambacho hakiingii akilini kabisa, makamanda wengi wameonesha kupinga hukumu ile,” kilisema chanzo hicho.

MASOGANGE AJIFICHA
Wakati makamanda wa nchi hizo wakimaliza kikao chao, habari zenye utata zimesambaa kwamba, Masogange alitua Bongo katikati ya mwezi uliopita lakini anaishi Dar au Mbeya kwao kwa kujificha.

Baadhi ya watu, wakiwemo marafiki zake wamekuwa wakisema kwa mkato staa huyo yupo Dar huku wengine wakisema baada ya kutua Dar alikwenda kwao Mbeya kwa sababu hataki kujulikana kuwa amesharudi Bongo.
Mwenyewe anapopatikana kwenye simu na kuulizwa amekuwa akijibu bado yupo Afrika Kusini lakini siku yoyote atatua Dar.

NZOWA ATOA UFAFANUZI
Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa alipoulizwa kwa njia ya simu juzi kuhusu mkutano huo alijibu kuwa yupo safarini kikazi akiwa katika mazingira mazuri atatoa ufafanuzi.
“Nipo safarini kikazi, naomba unitafute siku nyingine nitakupa ufafanuzi mzuri sana,” alisema Kamanda Nzowa ambaye naye ilidaiwa alikuwepo kwenye kikao hicho.

KUMBUKUMBU
Masogange na Mellisa Edward walikamatwa Julai 5, mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo uliopo Kempton Park jijini Johannesburg  nchini humo wakidaiwa kuingiza madawa ya kulevya aina ya Crystal Methamphetamine yenye thamani ya shilingi bilioni 6.8.
Hata hivyo, mahakama kuu nchini humo ilidai madawa hayo si ya kulevya bali ni malighafi haramu iitwayo Ephedrine ambapo kwa sheria za Afrika Kusini mtu akipatikana na hatia ya kuyaingiza nchini humo ni kifungo cha miezi 32 jela au faini ya shilingi milioni 4.8 kama alivyohukumiwa Masogange ambayo ni ndogo.
Pata habari kama hii kwa ufupi kwenye simu yako ya mkononi ya Vodacom kwa kutuma neno GLOBAL kwenda 15778.
CHANZO  NI GPL

Friday, October 11, 2013

MASOGANGE AJA NA SIRI NZITO.

VIDEO Queen wa Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ alitarajiwa kutua nchini  Jumatano ya wiki hii akitokea Afrika Kusini huku siri nzito ya mzigo aliodakwa nao ikitawala, Amani linakujuza.
Agnes Gerald ‘Masogange’.
Masogange anakuja Bongo baada ya kumaliza kulipa deni lote la randi 30,000 (shilingi milioni 4.8) alizoamriwa kulipa na Mahakama Kuu ya Gauteng iliyopo Kempton Park jijini Johannesburg nchini humo baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kuingiza kemikali haramu, Julai 5, mwaka huu.
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika, Masogange anarejea na Melisa Edward ambaye alikamatwa naye lakini mahakama ikamwona hana hatia.

SIRI NZITO
Ujio wa Masogange bado una siri nzito kwani licha ya mahakama hiyo kumtia hatiani kwa faini au kifungo cha miezi thelathini jela, lakini bado serikali ya Tanzania inahaha kutaka kujua mzigo aliodakwa nao alitumwa na nani!
“Masogange ameahidi kutowataja watu waliompa mzigo akidai kuwa itaendelea kuwa siri yake mpaka anakufa,” kilipasha chanzo chetu.
 
WATOTO WA VIGOGO
Watoto wa vigogo ndiyo wamekuwa wakitajwa zaidi kuhusika na kumtuma Masogange ingawa hakuna jina la moja kwa moja la mtoto yeyote wa kigogo lililowahi kutajwa.
ANAYEMJUA MWAKYEMBE
Mpaka sasa, Serikali ya Tanzania kupitia kwa Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison George Mwakyembe iliwahi kumtaja kijana aitwaye Mangunga ambaye ndiye anadaiwa kuwa na Masogange ndani ya ndege kwenda Afrika Kusini.

Sunday, September 22, 2013

Polisi kufuatilia nyendo za Masogange, Melissa.

Johannesburg. 
Kitengo cha Kupambana na Dawa za Kulevya Nchini, kimewataja Agnes Gerald, maarufu Masogange, na Melissa Edward kuwa watafuatiliwa nyendo zao kwa umakini.
 
Hatua hiyo iliyotangazwa na Kamishna Mkuu wa kitengo hicho, Geofrey Nzowa, imekuja siku moja baada ya Watanzania hao, Masogange na Melissa kuachiwa huru na Mahakama ya Kempton Park ya Afrika Kusini.

Nzowa alizungumza jana na mwandishi wa habari hii kwa njia ya simu, kuwa watu hao wataangaliwa kwa umakini watakapokuwa wakisafiri nje ya nchi.

Vilevile, alisema wataimarisha ukaguzi kwa Watanzania wengine, wenye historia ya kubeba dawa za kulevya wanaposafiri kwenda nje ya nchi.

“Masogange na Melissa tutawaangalia kwa jicho la umakini zaidi watu hawa,lakini siyo hao tu hata Watanzania wengine kwa sababu umdhaniaye siye kumbe ndiye,” alisema Nzowa.
Nzowa alisema Watanzania watakaokamatwa na dawa za kulevya nchini au nje na wataadhibiwa kulingana na sheria kama Masogange alivyoadhibiwa.

Hata hivyo, juzi Nzowa alionyesha kushangazwa na hukumu waliyopewa Masogange na Melissa akisema kuwa ni ndogo ukilinganisha na kiasi kikubwa cha kemikali walizobeba.

Hapa jijini Johannesburg, Masogange na Melissa jana walionekana wakitembelea maeneo mbalimbali ya jiji hilo ikiwamo madukani wakifanya ununuzi na katika saluni za urembo.
Mtu wa karibu na watu hao alisema, Watanzania hao hawana hofu ya kufanya chochote kwa sababu mahakama imegundua kuwa hawana hatia.

“Waogope kutembea barabarani kwa sababu gani wakati wameachiwa huru? Mahakama imefanya kazi yake na wao wana haki,” alisema mtu huyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

Saturday, September 21, 2013

Msanii Masogange, mwenzake wapata dhamana Afrika Kusini

Johannesburg. 
Watanzania Agness Masogange na Melisa Edward waliokamatwa kwa kutuhumiwa kubeba dawa za kulevya huko Afrika Kusini wameachiwa kwa dhamana.
 
 Mkuu wa Kitengo cha Polisi cha Kuzuia na Kudhibiti Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa

Mkuu wa Kitengo cha Dawa za Kulevya Afrika Kusini, Kamishna Toto Mangaleni aliithibitishia Mwananchi jana kuwa watuhumiwa hao wameachiwa kwa dhamana,lakini wataendelea kubaki Afrika Kusini wakati kesi yao ikiendelea.

Mangaleni alisema wanawake hao ambao juzi pia walipanda kizimbani, walipata dhamana hiyo jana kutoka Mahakama Kuu ya Gauteng iliyoko eneo la Kempton Park jijini Johannesburg.
 
Hata hivyo, Kamishna Mangaleni alisema hawezi kuzungumzia zaidi kuhusu kesi hiyo kwa sababu hataki kuharibu uchunguzi ambao unaendelea dhidi ya Watanzania hao, ambao ni wasanii.

Marafiki wa karibu wa Masogange wanaoishi maeneo ya Midland Johannesburg ambao walikataa kunukuliwa majina yao, walithibitisha kuwa wanawake hao wameachiwa kwa dhamana.

“Ni kweli wameachiwa leo asubuhi. Lakini hatuwezi kuongelea kwa kina habari hizi kwa sababu hatutaki matatizo na polisi. Hii kesi bado inaendelea na wataendelea kubaki hapa hadi kesi yao itakapomalizika,” alisema mmoja wa marafiki zake.
Naye Masogange aliandika kwenye mtandao wa ‘Facebook’.

Thursday, September 19, 2013

UJUMBE UNAOSAMBAA KWA KASI KUTOKA KWA AGNES MASOGANGE MUDA HUU,HUU HAPA

Hii ni post aliyoiweka Agnes Masogange kwenye ukurasa wake wa FB na imeanza kusambaa kwa kasi kupitia wasanii mbalimbali.
Je yawezekana wametoka?Au ndio zile fununu kuwa wanapiganiwa kesi yao irejee nchini?
Tungoje kama ni kweli ama uzushi

Monday, July 15, 2013

BINTI KIZIWI AHUKUMIWA MIAKA MITANO JELA BAADA YA KUKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA

MTANDAO wa wauza madawa ya kulevya unazidi kupukutika Bongo kufuatia madai ya kukamatwa kwa watu wanaodaiwa kujishughulisha na ubebaji ‘punda’ wa biashara hiyo haramu, Ijumaa Wikienda lina mtiririko wote.

Mrembo aliyehukumiwa miaka mitano Sandra Khan 'Binti Kiziwi'.

Hivi karibuni, Video Queen wa Wimbo wa Masogange, Agnes Gerald ‘Masogange’ amedaiwa kunaswa nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’ akiwa na kilo mia moja na hamsini za unga unaoaminika ni sehemu ya madawa ya kulevya. Ameshapanda kortini mara moja Ijumaa iliyopita.
Wakati Masogange akisota Sauzi kwa madai hayo mazito, habari ya mjini kwa sasa ni ya mtalaka wa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Ally Mohammed ’Z-Anto’, Sandra Khan au Binti Kiziwi kudaiwa kutupwa jela miaka mitano kwa sakata la ‘unga’.

HABARI YA MJINI KWA SASA NI BINTI KIZIWI 
Kuanzia Alhamisi iliyopita, habari zilizoligubika Jiji la Dar ni kuwa Binti Kiziwi amenyongwa nchini China baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na madawa ya kulevya.
Kwa mujibu wa mitandao, Binti Kiziwi alinyongwa wiki mbili zilizopita.
Hata hivyo, mitandao hiyo haikusema kama mrembo huyo alinyongwa hadi kufa au la! Sheria za hukumu hiyo, mwenye hatia anatakiwa kunyongwa hadi kufa.

Saturday, July 13, 2013

JESHI LA POLISI LATEUA ASKARI WA KUMFUATA AGNESS MASOGANGE AFRIKA KUSINI

Jeshi la Polisi litapeleka askari wake Afrika Kusini kuwahoji washiriki wa video za wasanii wa muziki wa Bongo fleva, Agnes Gerald ‘Masogange’ na mwenzake Melisa Edward waliokamatwa nchini humo na dawa za kulevya. 
 
Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa aliiambia Mwananchi kwa simu jana kuwa watawapeleka polisi kuwahoji na wanaamini wahusika watawaeleza wahusika wa mzigo huo.
 
Wasichana hao walikamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Oliver Tambo nchini Afrika Kusini wakitokea Tanzania wakiwa na kilo 150 za dawa za kulevya aina ya Crystal Methamphetamine.
 “Tutawapeleka askari wetu kuwahoji, tumekwishaanza uchunguzi wa hili...wote watakaohusika katika hili tutawakamata, lakini tunakwenda polepole hatua kwa hatua kuhakikisha tunawanasa wahusika sahihi,” alisema Nzowa.
 
Naye Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, (JNIA), Moses Malaki alieleza kushangazwa na kiasi kikubwa kupitishwa kwenye uwanja huo licha ya kuwa wapo watu wenye dhamana ya kuangalia usalama.
 
“Sitaki kusema tutafanya nini, lakini ninachotaka kukwambia ni kwamba uchunguzi umeanza na suala zima tumewaachia polisi na sisi tutatoa ushirikiano kwa kila hatua watakayotutaka, lazima kukomesha hili.
 
“Tutaangalia nani walikuwa zamu siku hiyo,” alisema Malaki

Wednesday, July 10, 2013

HUYO NDIO "MELLIS EDWARD" ALIYEKAMTWA NA MADAWA YA KULEVYA AKIWA NA "AGNESS MASOGANGE.

Picha  ya  Mrembo Mellis Edward  aliyedakwa  na  madawa  ya  kulevya  Afrika  kusini  akiwa  na  Agness Masogange

Mellis Edward
Inahisiwa kuwa  huyu mwanamke wa pili aliyetajwa na Kamanda Nzowa kwa jina la “Melisa Edward”  ni mdogo wake na Agnes ambaye katika akaunti ya facebook anayo tumia jina la (MELLIS EDWARD) , Agnes amemuweka katika orodha ya family kama ‘sister’ katika akaunti yake ya Facebook.
 Kamanda  Gofrey  Nzowa - Kitengo  cha  Madawa ya Kulevya


 Agness Masogange  akiyahesabu  "MAPESA" yake.Picha  hii aliiweka  siku  chache  zilizopita

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate