EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, September 27, 2014

RAY, JB WAMPIGIA SALUTI KAJALA

Waigizaji wakongwe kwenye tasnia ya filamu Bongo, Jacob Steven ’JB’ na Vincent Kigosi ‘Ray’ wamempigia saluti muigizaji mwenzao,  Kajala Masanja kutokana na filamu fupi aliyotengeneza ya Mbwa Mwitu.
Staa wa Filamu Bongo, Kajala Masanja akihojiwa na waandishi wakati wa uzinduzi wa filamu yake ya Mbwa Mwitu.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye uzinduzi wa filamu hiyo uliofanyika Mlimani City juzi, JB alisema kuwa  Kajala amebuni kitu cha tofauti kabisa ambacho jamii nzima mpaka watoto wanafahamu kuhusu Mbwa Mwitu.

BABY MADAHA ATAMANI PENZI LA WEMA, DIAMOND


Stori: Imelda Mtema
MWANAMUZIKI mwenye vituko kila kukicha Bongo,  Baby Joseph Madaha, ametoa dukuduku lake la moyoni na kusema kuwa kila kukicha anayatamani mapenzi ya Wema Sepetu na Nasibu Abdul ‘Diamond’ kama angekuwa yeye.

MCHUNGAJI ASHTUA KUMUOA DOGODOGO!

Stori: Haruni Sanchawa MCHUNGAJI Peter Rashid Abubakari wa Kanisa la RGC lililoko Mbezi ya Shamba jijini Dar, amedaiwa kuoa mke wa pili aitwaye Pamela Didas Asenga akiwa na umri wa miaka 20 tu ‘dogodogo’, Risasi Jumamosi limetonywa.

SHUHUDA ALBINO ATAKA WAUAJI WANYONGWE HADHARANI‏

DSC_0519
Shuhuda aliyenusurika kwenye mauaji ya Albino ambaye amekatwa mikono yote miwili, Mariam Stanford akitoa ushuhuda wake na killio chake mbele ya meza na wageni waalikwa waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya siku ya kimataifa ya amani iliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam kwenye viwanja vya Mnazi mmoja.
DSC_0534
Mke wa Balozi wa Uturuki nchini Yesim Davutoglu, akilia kwa uchungu baada ya kusikia shuhuda kutoka kwa mhanga wa mauaji ya Albino aliyekatwa mikono yote miwili, Mariam Stanford (hayupo pichani) ambaye hadi sasa anapewa matunzo na Shirika la Under The Same Sun.
DSC_05401
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la UNDER THE SAME SUN, Vicky Ntetema akimfariji mke wa Balozi wa Uturuki nchini Yesim Davutoglu, wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya amani duniani iliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi mmoja hivi karibuni jijini Dar.

Friday, September 26, 2014

MAMA SALMA AHUTUBIA MKUTANO WA WAKE WA MARAIS WA UN WA KUWAJENGEA UWEZO WANAWAKE NA WASICHANA KIFEDHA

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mama Kim Simplis Barrow, Mke wa Waziri Mkuu wa Belize na Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia masuala ya Wanawake na Watoto. Mama Barrow kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa ndio walioandaa mkutano wa Wake wa Marais na Wakuu wa Nchi kuzungumzia masuala ya kuwawezesha wanawake na wasichana kifedha.na “First Ladies Global Call to Action Conference on Women and Girls’ Financial Health.” Tarehe 25 Septemba,2014.PICHA NA JOHN  LUKUWI
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mama Joyce Banda, Rais Mstaafu  wa Malawi muda mfupi kabla ya kuanza mkutano wa Wake wa Marais na Wakuu wa Nchi ulizungumzia namna ya kuwawezesha wanawake na wasichana kifedha huko New York tarehe 25.9.2014.

MENINA, MENINA, MENINA........

 
Menina
Daah sijui nianzie wapi? maana ni msanii unayekuja juu, kitu kinachoniuma zaidi ni kwamba utaingia katika matatizo, kwani hujui?? nakuwasa mdogo wangu kama ni kweli acha kwani hizo ni anga za wakubwa, umeona kilichotokea kwa dada zako waliopita, sasa usitake kuchekwa na jamii, ongeza bidii katika sanaa ili ufike pale ulipotaka kufika, mengine waachie wenyewe, there is no smoke without fire....... usije ukasema hatukukwambia.

Mgosi: Jaja akizoea Bongo atakuwa hatari

Straika wa Yanga, Mbrazili, Geilson Santana ‘Jaja’.
Na Alpha Amos STRAIKA wa Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro, Mussa Hassan Mgosi, amemtabiria makubwa straika wa Yanga, Mbrazili, Geilson Santana ‘Jaja’ kwa kusema atakuwa mchezaji mzuri pindi atakapozoea mazingira ya Tanzania na viwanja nyake.
Jumamosi iliyopita, Mgosi aliifungia timu yake bao moja katika ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Yanga, huku Jaja akishindwa kufunga na kukosa penalti.

Mhh! Ndanda wanafanya mazoezi ‘masaa 7’

TIMU ya Ndanda FC ya mkoani Mtwara, imelazimika kufanya mazoezi kwa saa saba kwa siku ili kujiweka fiti kuelekea mchezo wa ligi dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa kesho Jumamosi kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro.
 

Timu zote mbili ziliweza kuibuka na ushindi kwenye michezo yao ya kwanza ambapo Ndanda iliifunga Stand United mabao 4-1 huku Mtibwa ikiifunga Yanga mabao 2-0.
 

Kocha wa Ndanda, Denis Kitambi, ameliambia gazeti hili kuwa, wanafanya mazoezi asubuhi kuanzia saa moja mpaka saa tatu na kisha wanaanza saa tisa alasiri mpaka 12 jioni.
 

“Tunafanya mazoezi kwa muda mrefu, lengo likiwa ni kujiweka fiti katika michezo yetu ya ligi ambapo mchezo ujao tunacheza na Mtibwa na tunataka kuibuka na ushindi kwani malengo yetu ni kufanya vizuri kila mchezo,” alisema Kitambi.

Beki Simba awapigia magoti mashabiki

Na Sweetbert Lukonge
WAKATI kikosi cha Simba kikitarajia kushuka uwanjani kesho Jumamosi kupambana na Polisi Moro katika mechi ya Ligi Kuu Bara, beki wa kati wa timu hiyo, Hassan Isihaka amewaomba msamaha mashabiki wa timu hiyo kutokana na makosa aliyoyafanya uwanjani Jumapili iliyopita dhidi ya Coastal Union ya Tanga.
Katika mechi hiyo iliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Isihaka alifanya makosa kadhaa likiwemo lile la kuunawa mpira nje kidogo ya eneo la 18 ambalo lilikuwa na faida kwa Coastal, kwani ilijipatia bao kupitia kwa Rama Salim na kufanya matokeo kuwa 2-2.
“Naomba wanisamehe kwa yote yaliotokea katika mechi hiyo na wasinielewe vibaya kwani sikukusudia kufanya hivyo ila hali hiyo ilitokea kwa bahati mbaya wakati nikijaribu kuondoa mpira kwenye eneo hilo la hatari,” alisema Isihaka.

YONDANI: NGOJA NIKUTANE NA OKWI UONE UBORA WANGU

YONDANI.
Beki wa kati wa Yanga, Kelvin Yondani, ametamba kuwa yeye ni bora na anataka kulithibitisha hilo atakapokutana na Emmanuel Okwi wa Simba katika mechi baina ya timu hizo, Oktoba 12, mwaka huu.

Yondani amesema hakuna ubishi yeye ndiye beki bora kwa hivi sasa, hivyo anaamini hakuna mshambuliaji yeyote atakayemsumbua ndani ya uwanja, akiwemo Okwi ambaye anazungumzwa zaidi katika kikosi cha Simba.

TBL YATOA MSAADA WA VISIMA VYA MAJI ZANZIBAR NA MBAGALA‏

Mwakilishi wa Kampuchea ya Bia Tanzania (TBL) Zanzibar Samir Manji ( wa tatu kushoto),  akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh. mil 51 wananchi wa majimbo ya Chumbuni na Mpendae ikiwa ni msaada wa kampuni hiyo kwa ajili ya mradi wa uchimbaji wa visima vya maji safi na salama katika majimbo hayo juzi. Wa pili kushoto ni Ofisa Uhusiano wa TBL, Dorris Malulu.
Mwakilishi wa Mauzo ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Kanda ya Temeke, Bw. Alen Mwebuga (kushoto), akimkabidhi Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya cha Mbagala Round Table Maternity Home, Dkt. Baturi Luhanda, mfano wa Hundi ya sh. Milioni 20, kwa ajili ya kusaidia kuchimba kisima cha maji. Wengine katika picha ni Afisa Uhusiano wa TBL, Bi. Doris Malulu (wa pili kulia), Mhandisi wa mradi huo, Bw. Onesmo Zakaria na Rais wa Rotary Klab Agnes Batenga.
(Na Mpigapicha Wetu)

BILIONEA AMPANGISHIA LULU JUMBA LA KIFAHARI

Stori: Hamida Hassan, Gladness Mallya na Musa Mateja.
Madai mazito ya kushtua mtaani yanasema kwamba staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, mambo yake kwa sasa yapo juu ya mstari baada ya bilionea kutoka jijini Arusha (jina tunalihifadhi kwa sasa) kudaiwa kujitosa kumlea akianza kwa kumpangishia jumba kubwa la kifahari.
Staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, akiwa na begi la fedha.
TWENDENI USHUANI
Habari hizo za mitaani zilidai kwamba bilionea huyo amempangishia Lulu mjengo huo wa maana uliopo ushuani maeneo ya Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.
Kimuonekano, nyumba hiyo iliyoshuhudiwa na wanahabari wetu mwanzoni mwa wiki hii haina tofauti na ile mijengo iliyozoeleka ya mastaa wakubwa wa Marekani kwa maana ya kujitosheleza kwa kila kitu ndani yake.

Mtandao wa Wanawake na Katiba Wawapongeza Wajumbe wa Bunge la Katiba...!‏


Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanawake na Katiba, Prof. Ruth Meena akizungumza na waandishi wa habari. Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanawake na Katiba Tanzania, Prof. Ruth Meena (wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Lilian Liundi na wajumbe wengine wa mtandao wa wanawake na Katiba.Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanawake na Katiba, Prof. Ruth Meena akizungumza na waandishi wa habari. Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanawake na Katiba, Prof. Ruth Meena akizungumza na waandishi wa habari.

SKYLIGHT BAND WAZIDI KUTIKISA JIJI LA DAR KWA BURUDANI NZITO


Skylight Band Divas Mary Lukos(Wa kwanza Kushoto) Aneth Kushaba(katikati) Na Digna Mpera (Wa kwanza Kulia) wakitoa burudani ya nguvu Kwa Mashabiki Wao Ndani ya Kijiji cha Maraha Thai Village Ijumaa Iliyopita.Kila Ijumaa ya mwisho wa wiki Band Ya Skylight Wanapiga show Ndani ya Thai Village.Karibu Leo Upate burrudani ya nguvu yenye kukonga Roho yako na kutakuwa na Supriseeeeeee kibaoooo ndani ya Thai Village
          Hashimu Donode Akiimba kwa raha zake ndani ya Thai Village 
Shabiki huyu hakuweza kujizuia hisia zake pale alipoguswa na muziki mzuri uliokuwa ukiimbwa na Hashimu Donode
Donode Akiendelea kuimba na shabiki wake kwa Raha zaooooo
Digna Mpera akizipiga zile voca; kali za kumtoa nyoka pangoni
Mary Lukos Akifurahi na kucheza ala nzuriiii toka kwa wapiga vyombo wa Skylight Band Hawapo Pichani

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate