EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, June 23, 2012

Wanawake Mbeya wajutia vidhibiti mimba

WANAWAKE wengi hasa waishio nchi zinazoendelea wamekuwa wakipanga uzazi kwa kutumia dawa wanazopewa na ushauri wa namna ya kuzitumia.
Lengo la ushauri huo ni kuepuka kuzaa bila mpangilio huku wakiaminishwa kuwa dawa hizo zinawasaidia.

Dawa hizo licha kuwapatia madhara, lakini wengi wao wamekuwa wakikaa kimya na kuugulia madhara wanayoyapata, tena bila kujaza fomu ambazo baadhi ya watumiaji wamedai kuwa hawafahamu lolote kuhusiana nazo.

Mbali na shirika hilo kutetea uhai nchini, pia huwa linazunguka barani Afrika kueleza na kutetea madhara yatokanayo na dawa hizo, utoaji mimba, elimu kwa vijana, usafi wa roho na mambo mengine.
Katika utafiti niliofanya mkoani Mbeya na vitongoji vyake, ukiandaliwa na kudhaminiwa na Shirika la Kutetea Uhai wa Binadamu Tanzania (PROLIFE), niligundua kuwapo kwa wanawake wengi ambao wamepata madhara baada ya matumizi ya dawa hizo.
Kabla sijaendelea na namna utafiti ulivyofanyika na madhara waliyoyapata, nianze kwa kueleza aina ya dawa na vidhibiti mimba vitumiwavyo.

Kuna aina tano ya vidhibiti mimba, nazo ni vidonge vya majira vitumiavyo chachu za bandia za projestorini na estrojeni zilizotengenezwa katika maabara ambapo mwanamke humeza kila siku.
Zipo aina mbalimbali za vidonge, majina ya vidonge hutegemea aina na kiwango cha chachu zilizowekwa.
Vidonge vyenye chachu ya estrojeni pekee huitwa vidonge na vidonge vyenye mchanganyiko wa chachu ya estrojeni na projestini huitwa vidonge mchanganyiko.
Vidonge vyenye chachu aina ya projestini pekee huitwa: Progestorene Only Pills (POP) au Low Dose Pill au Mini Pill.
Leo hii vidhibiti mimba vingi vimetengenezwa kwa chachu hii pekee ambayo ni morning After Pills, RU486, Emmergency Contraceptives.
Aina ya pili ni vipandikizi ambapo mashirika yanayoendeleza njia za kisasa za kupanga uzazi wanasifia vipandikizi, kama ni njia nzuri na salama kwa wanawake wanaotumia.
Mashirika hayo yanadai kuwa, njia hii ni rahisi kwani inaondoa ile adha ya kumeza vidonge kila siku, zoezi ambalo baadhi ya watumiaji husahau.
Hii ni chachu au homoni iitwayo ‘levonorgestrel’ inayowekwa katika vifuko 6. Baada ya kuwekwa, huanza kufanya kazi saa 24 hadi miaka 5.
Kila kifuko huwekwa mg 36 za chachu ya ‘crystalline levonorgestrel’ na kila kimoja kina urefu wa mm 34 na upana wa mm 2.4. Kiasi cha mg 30 ya projestini husambazwa katika damu kila siku.

Aina ya tatu ni kondomu inayotumika kwa mwanaume na mwanamke pia. Kwa kawaida kifaa hiki hubana kufuatana na umbile la mtu.
Kondomu zimegawanyika katika aina tatu; ya kwanza ni zile zilizotengenezwa kwa utumbo wa kondoo zinazosemekana kuwa hazina uwezo mkubwa zikitumika kama kidhibiti mimba.
Aina ya pili ni zile zilizotengenezwa kutokana na mpira wa latex. Watengenezaji wanazisifia kuwa na ubora mkubwa zinapotumika au kama kidhibiti mimba au kwa lengo la kudhibiti kuenea kwa maambukizo ya magonjwa ya zinaa ikiwemi virusi vya ukimwi (VVU).

Aina ya tatu ni kondomu zilizotengenezwa kutokana na mchanganyiko wa mpira na vitu vingine ziitwazo “polyurethane.”
Soko la kondomu limepata umaarufu zaidi kuanzia miaka ya 1980 kufuatia kuzuka na kuenea kwa janga la ukimwi.
Aina ya nne ya vidhibiti mimba ni kitanzi. Hiki ni kifaa kidogo cha plastiki chenye vinyuzi mwishoni, ambacho huwekwa kwenye mji wa mimba kupitia uke.
Mtumiaji anaweza kugusa nyuzi hizo kama anataka kujua kitanzi alichoweka bado kipo.
Baadhi ya wanawake ambao nilipata kuzungumza nao baada ya Mkurugenzi wa Prolife, Emil Hagamu kutoa mafundisho, walieleza madhara na kusema kuwa mwanzo hawakujua wanaumwa nini, na matatizo yao yanatokana na nini.
Scola Yusuph alieleza: “Mimi nilitumia vidonge, lakini nikawa natoa harufu mbaya katika sehemu zangu za siri na nilipimwa nikaambiwa nina fangasi.”
Naye Agness Raphaely anasema baada ya kutumia sindano aina ya depo provera akawa hajisikii hamu ya tendo la ndoa japo kabla ya kutumia alikuwa akifurahia.
Zawadi Kilembe ameeleza kuwa, alichoma sindano Januari 13 mwaka huu na akaanza kupata siku zake mfululizo hadi Aprili 17.
Anasema alikuwa anaumwa sana kila siku hadi kufikia kulazwa, na kusema madhara mengine aliyopata ni kukonda, kichefuchefu, kichwa kuuma, kuumwa tumbo na chembe moyo.
Katika tafiti ya kwanza iliyoshirikisha zaidi ya wanawake 350, wanawake 150 kati yao walieleza madhara waliyoyapata kutokana na dawa hizo.

Tafiti hii pia iliendelea hadi Mbeya vijijini ambako nilibahatika kukutana na wanawake wa Kanisa la Moravian katika Kijiji cha Igoma, ambao wanaeleza matatizo wanayoyapata baada ya kutumia dawa za uzazi wa mpango.
Elizabeth Brayson anasema baada ya kutumia vidonge alipata matatizo ya kuumwa kichwa na kutoka damu mfululizo.

Anasema baada ya kupata shida hiyo, aliamua kwenda hospitali na kushauriwa abadilishe na kuweka vipandikizi maarufu vya vijiti.
Imelda Mwakilasa anasema baada ya kuchoma sindano moja alikosa hamu ya tendo la ndoa hali iliyosababisha kuwa na mgogoro wa mara kwa mara na mumewe, na ilimchukua miaka minne na alipata kizunguzungu na kichwa kuuma, kiasi kwamba hata alipokunywa dawa kilikuwa hakiponi.
Hao ni baadhi tu ya wanawake ambao wameumizwa na matumizi ya dawa hizo.

Mkurugenzi wa Prolife, Hagamu, anaeleza dhima nzima ya shirika hilo na kusema kuwa ni kulinda, kutetea na kudumisha uhai wa binadamu, kutetea hadhi na heshima yao kwani vidhibiti mimba vinaharibu hekalu la Mungu.
Dhima nyingine ni kufundisha njia za uzazi wa mpango kupitia maumbile ya mwanamke, elimu ya usafi wa moyo, na kutengeneza taifa la mtetezi wa uhai.
                                      Habari na  Happiness Mnale wa Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate