EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 2, 2012

Gari la Mhe. Fenella Mukangara lililopata ajali na kujeruhi

Picture: Gari la Fenella Mukangara ajalini
Hili ndilo gari ambalo alilokuwa akitumia Waziri  wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara, na kupata nalo ajali  juzi akiwa safarini kutoka Dodoma kuelekea jijini Mwanza kikazi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Antony Luta, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo majira ya saa 3:30 asubuhi katika Kata ya Nyandekwa wilayani Igunga mkoani hapo, ikihusisha gari lenye namba za usajiri STK 8780.

Luta alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva wa basi la Green Star lenye namba za usajili T939 TRA ambalo lilikuwa likitokea Kahama kuelekea Dar es Salaam, alipokuwa akijaribu kulipita lori katika mlima huku gari la Waziri huyo likitokea upande wa pili.

Dereva wa Waziri aliyetambulika kwa jina la Saidi Komando, alijaribu kulikwepa basi hilo, lakini akashindwa na hivyo gari likapinduka mara tatu na kusababisha watu watatu akiwemo Waziri Fenella, kujeruhiwa.

Kamanda Luta alisema mara baada ya ajali hiyo, Waziri huyo na majeruhi wengine walikimbizwa katika hospitali ya Wilaya ya Nzega kwa matibabu na kwamba mipango ya kuwahamishia katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma zinafanywa.

Dereva wa basi la Green Star, Daniel Chawa (32), alikamatwa baadaye na polisi wilayani Igunga, baada ya kuwa amekimbia awali na hivyo atafikishwa mahakamani.

Hali ya Dkt. Mukangara inaendelea vizuri.

Akiongea na Globu ya Jamii sasa hivi yupo Dar es salaam alikorejea jana jioni na kupata matibabu zaidi katika kitengo cha mifupa cha MOI hospitali ya Muhimbili. Amesema baada ya kuchukuliwa vipimo vyote, ameonakana hana madhara mwilini zaidi ya michubuko na  majeraha mengine madogo. Anashukuru kwamba wote walikuwa wamefunga mikanda na kwamba air-bags za gari hilo zimeokoa maisha yao.

Amewashukuru sana madaktari wa Nzega na wa kitengo cha dharura cha Muhimbili ambao walimhudumia pamoja na wa hospitali ya Regency alikopatiwa vipimo vya CT-Scan. Pia anawashukuru Watanzania wote waliomuombea apate nafuu, wakiongozwa na Rais Jakaya Kikwete.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate