EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 2, 2012

GARI WOLPER LAKAMATWA


Shakoor Jongo na Erick Evarist
LILE gari la kifahari aina ya BMW X6 lenye namba za usajili T 574 BXF linalomilikiwa na staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper Masawe limedakwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Kwa mujibu wa ofisa mmoja wa TRA ambaye hakutaka jina lake lichorwe gazetini, gari hilo la kisasa lilikamatwa Juni 28, 2012 kupitia Kampuni ya Mnada ya Majembe kutokana na sababu kadha wa kadha.
SABABU ZAANIKWA
Akiendelea kufunguka, afisa huyo alisema kuwa sababu ya kwanza ni kuhisiwa kuwa gari hilo liliingizwa nchini kinyemela kutokana na vielelezo vyake vya kwenye kadi kupitia kwenye vyombo vya habari, ndipo taa nyekundu ikawaka ndani ya vichwa vya maafisa wa TRA na kuanza kulifuatilia.
Alidai kuwa mbali ya kuingia nchini kinyemela, lakini BMW hilo halijalipiwa ushuru zaidi ya miaka mitano iliyopita kwa mujibu wa vielelezo vyake.
MPANGO WA KULIKAMATA ULIVYOSUKWA
Kwa mujibu wa ofisa huyo, ili kufanikisha zoezi la kulikamata gari hilo, vijana kutoka kampuni ya Majembe waliingia mzigoni kulisaka ambapo kuna mtu alipiga kambi jirani na makazi ya Wolper, Mbezi Beach jijini Dar.
Ilisemekana kuwa vijana hao walikuwa na kazi moja tu, kuhakikisha anapotoka Jack wanamfuatilia hatua kwa hatua hadi mahali atakapokwenda kupiga kambi na kulitia mikononi.
“Haikuwa kazi rahisi maana muda mrefu alikuwa haonekani nalo, ndipo mpango huo ulipokuja kukamilishwa kwa njia ya kumfuatilia anapotoka kwake hadi mahali lilipokamatwa maeneo ya katikati ya Jiji la Dar,” alisema.
Akaendelea kudai: “Unajua hawa mastaa wetu kuna vitu wanavifanya bila kujua madhara yake, kitendo cha Wolper kuonesha kadi ya gari kwa waandishi wa habari huku anafahamu ina mapungufu kibao ndiyo sababu kuu ya gari hilo kuanza kufuatiliwa.”
MH! ETI USHURU MILIONI 70?
Taarifa nyingine ya kushtua ni kwamba ilidaiwa kuwa kuwa TRA peke yake inadai Sh. milioni 70 za ushuru.
“Si fedha ndogo zinazodaiwa na TRA, kwa hesabu ya harakaharaka ni zaidi ya Sh. milioni 70 ambazo zinatakiwa kulipwa.”
Baada ya The Biggest IQ Paper, Ijumaa Wikienda kujiridhisha kuwa gari hilo limedakwa, lilimuendea hewani Wolper lakini hakuweza kupokea simu hadi gazeti linakwenda mitamboni.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate