EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, July 25, 2012

Kigogo polisi atoboa siri kipigo cha Dk. Ulimboka

 Alazwa Muhimbili, awaomba madaktari wasimdhuru
MKUU wa Upelelezi wa Kituo cha Polisi Kawe (OC CID), David Mapunda, ametoa siri ya kutekwa, kupigwa na kuteswa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Chama cha Madaktari, Dk. Steven Ulimboka.
OC CID huyo ambaye kwa sasa amelazwa katika Kitengo cha Mifupa cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (Moi) alilazimika kutoboa siri ya kipigo cha Dk. Ulimboka ili aweze kupata matibabu ya majeraha ya ajali ya kugongwa na gari aliyoipata juzi.
Dk. Ulimboka alipookotwa na wasamaria wema katika msitu wa Pande na kufikishwa katika kituo cha polisi Bunju, kilicho chini ya kituo cha Kawe, OC CID huyo anadaiwa kutoa amri ya Dk. Ulimboka kukaa zaidi ya saa tatu ili asipate matibabu ya haraka.

Vyanzo vyetu vya habari vililiambia gazeti hili kuwa mara baada ya kugongwa na gari juzi, kigogo huyo wa polisi alijitahidi sana kukwepa kwenda Muhimbili lakini alijikuta akiishia mikononi mwa madaktari wa taasisi hiyo ya mifupa ya Moi, hivyo aliingiwa hofu ya kutotendewa haki ya matibabu.
Kabla ya kufikishwa Muhimbili, askari huyo alikwenda katika Hospitali ya Rufaa ya Lugalo na Aghakan, lakini alijikuta anatakiwa kufika Kitengo cha Mifupa cha Moi, Muhimbili, ambako hadi sasa bado anaendelea na matibabu.

Kwa mujibu wa habari hizo kutokana na hofu ya kususiwa na madaktari, polisi huyo alilazimika kuwapigia magoti na kueleza mengi kuhusu kipigo cha Dk. Ulimboka na kwamba yeye hahusiki na sakata hilo.
Mtoa habari wetu alisema kuwa OC CID huyo mara baada ya kufikishwa hospitalini hapo akiwa na maumivu makali, alisema hahusiki na kipigo cha Dk. Ulimboka na hata siku ya tukio hakuwepo.
Katika hali isiyo ya kawaida, kigogo huyo alijitetea huku akiwa na maumivu makali ya majereha aliyopata.
“Mimi sijahusika kabisa na kutekwa kwa Ulimboka. Jamani msinidhuru. Tena siku hiyo mimi sikuwepo,’ alikaririwa OC CID akisema.

Habari zaidi zinasema kuwa askari huyo aliendelea kueleza mengi na hata alipotakiwa kuchomwa sindano, alionyesha woga na kuuliza anachomwa sindano gani.
Ili kuhakikisha anatibiwa vizuri, kumekuwa na doria za kila mara ndani na sehemu mbali mbali za wodi za MOI hali iliyowafanya madaktari na wauguzi wa hospitali hiyo kulalamikia hali hiyo.
Mbali ya OC CID huyo kuingiwa na hofu ya kulipiziwa kisasi, hofu hiyo pia imewakumba ndugu zake kwani hawana amani na matibabu ya ndugu yao.
Tanzania Daima Jumatano ilipofika katika hospitali Muhimbili, ilishuhudia kuwapo kwa askari polisi wakilinda doria, huku OC CID akiwa amelazwa chumba cha peke yake akiendelea kutibiwa.

Akizungumza na gazeti hili jana, mmoja wa madaktari wa Muhimbili ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe, alisema Mapunda alifikishwa hospitalini hapo juzi akiwa katika hali mbaya na mara baada ya kufikishwa aliomba msamaha kwamba hakuhusika kumteka Dk. Ulimboka.
“Ni kweli jamaa alipokelewa lakini tulishangaa kwani alikuwa akiongea kwa kuweweseka kwamba hajahusika na tukio la kumteka na kumtesa Dk. Ulimboka na akawa anaomba tusimdhuru,” alisema daktari huyo.

Kwa mujibu wa daktari huyo, kilichowashangaza zaidi ni ulinzi mkali wa polisi aliowekewa mgonjwa huyo huku kukiwa na watu wanaofuatilia kila anayeingia katika wodi namba D aliyolazwa.
Afisa Uhusiano wa Moi, Jumaa Almasi, alisema mgonjwa huyo alifikishwa hospitalini hapo wiki iliyopita akiwa amepata majeraha mwilini baada ya kugongwa na gari.
Kuhusu mgonjwa huyo kumtaja Dk. Ulimboka, Almasi, alisema hawezi kuzungumzia tukio hilo kwani hakuwepo wakati akifikishwa hospitalini hapo.
Kwa Upande wake, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, alithibitisha kupata ajali kwa OC-CID Mapunda na kuongeza kuwa ajali hiyo aliipata wakati akitekeleza majukumu yake.
Alisema hakuna uhusiano wowote wa tukio la kutekwa Ulimboka na ajali hiyo.

Tangu tukio la kutekwa na kuteswa kwa Dk. Ulimboka serikali kupitia maafisa wake wa usalama wamekuwa wakihusishwa kwa namna moja au nyingine.
Kuhusishwa huko kwa serikali hususan jeshi la polisi kunafuatia matukio mbalimbali ikiwa ni pamoja na afisa upelelezi kutoka kituo cha Selanda Bridge katika eneo la Muhimbili, matamshi ya kutatanisha ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova pamoja na kukamatwa kwa mtu aliyedaiwa kuungama kanisani kuwa ndiye aliyemteka na kumtesa Dk. Ulimboka.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate