EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, July 1, 2012

Madaktari 146 watimuliwa kwa mgomo

MADAKTARI 146 wamefukuzwa katika hospitali mbalimbali nchini kutokana na kushiriki mgomo unaoendelea nchi nzima kwa lengo la kuishinikiza Serikali kutekeleza madai yao.

Uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa, madaktari hao walitimuliwa katika Hospitali za Bugando na Sekou Toure mkoani Mwanza na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya na ile ya Rufaa Dodoma.

Wakati Serikali ikichukua hatua hiyo, mgomo huo jana uliendelea katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Ocean Road, Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) za jijini Dar es Salaam, Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na Hospitali ya Rufaa ya KCMC mkoani Kilimanjaro.

Katika kile kinachoonekana kuwaunga mkono wenzao, madaktari bingwa wa MOI, MNH na Ocean Road jijini Dar es Salaam, jana walitangaza rasmi kuingia kwenye mgomo huo hadi madai hayo yatekelezwe.

Madai ya madaktari ni hali bora ya mazingira ya utoaji huduma nchini, ongezeko la mishahara, posho za kufanya kazi katika mazingira magumu, posho za kufanya kazi katika mazingira hatarishi na posho za kuitwa kazini.

Tamko la madaktari hao bingwa, lilitolewa jana na msemaji wao, Dk Catherine Mng'ong'o muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao chao kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

Tamko hilo limekuja siku moja baada ya baadhi yao kuanza kushiriki mgomo huo juzi, kushinikiza pamoja na mambo mengine, Serikali itoe tamko juu ya tukio la kutekwa na kujeruhiwa kwa Dk Ulimboka.

Hata hivyo, wakati madaktari hao wakitoa tamko hilo, uongozi wa Moi jana ulitoa tangazo kuwataka madaktari wote walioshiriki mgomo huo kurejea kazini ifikapo Julai 2, mwaka huu, vinginevyo watafukuzwa kazi.

Jana jengo la MOI lilikuwa limefungwa kwa makufuli, huku wagonjwa wakielezwa kuwa huduma zote hazitolewi zikiwamo za dharura ambazo awali ziliendelea kutolewa.
Mmoja wa walinzi aliwambia waandishi wa habari kuwa, amefunga mageti kutokana na amri ya mkuu wake wa kazi.
“Mimi ninatekeleza amri ya bosi wangu, amenitaka kufunga geti na hakuna mtu kuingia, awe mgonjwa au ninyi waandishi wa habari kwa kuwa hakuna huduma zinazotolewa humu,” alisema.
Mkoani Mwanza
Madaktari 63 walio katika mafunzo ya vitendo kazini wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Hospitali ya Mkoa Sekou Toure wametimuliwa na kurejeshwa wizarani kutokana na mgomo huo.

Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Dk Charles Majinge alisema kuwa, juzi aliwataka madaktari waliokuwa katika mgomo kurejea kazini, lakini hawakufanya hivyo na jana akaamua kuwarejesha 47 wizarani.

Katika Hospitali hiyo ya Mkoa wa Mwanza Sekou Toure, Mganga Mkuu wa Mkoa, Dk Valentino Bangi alisema, madaktari 16 wamesimamishwa kufanya kazi kutokana na agizo la wizara.

Kilimanjaro

Madaktari walioko kwenye mgomo katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC, Moshi mkoani Kilimanjaro walisema jana kuwa, kinachofanywa na Serikali kuwafukuza kazi waliogoma, ni njia mojawapo ya vitisho, lakini wakasema kuwa kamwe hawataogopa.

Madaktari hao ambao hawakutaka majina yao yaandikwe gazetini walisema, wao wanaendelea na mgomo mpaka pale Serikali itakapotekeleza madai yao.

“Tumesikia wenzetu wa Dodoma na Mbeya wamefukuzwa ….Hiyo haitufanyi turudi kazini na kama Serikali inaona hiyo ndiyo njia ya kumaliza mgogoro huu waendelee sisi tutarudi kazini pale itakapotimiza tunayotaka,” alisema mmoja wa madaktari hao.

Mbeya

Juzi Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, ilitoa tangazo la kuwataka madaktari waliopo mafunzoni waliogoma kurejea kazini jana, na endapo wangekiuka agizo hilo wangekuwa wamejifukuzisha kazi. Na hadi jana jioni hospitali hiyo ilikuwa imewafukuza madaktari 72.

Ocean Road

Katika Taasisi ya Taifa ya Saratani, (Ocean Road), kutokana na madaktari sita kusitisha kutoa huduma tangu Dk Ulimboka alipojeruhiwa kwa kipigo, waligoma na jana Mkurugenzi wa Tiba na Huduma Diwani Musemo alionekana akitembelea wagonjwa.

Dodoma
Madaktari 11 wa mafunzo kwa vitendo katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma nao wamefukuzwa, tukio ambalo jana lilileta usumbufu mkubwa katika upatikanaji wa tiba hospitalini hapo.
“Kwa hakika matibabu yanaendelea ingawa ni katika hali ya kusuasua. Hatuna uhakika kama kweli kuna mgomo wa chinichini au la, maana mimi nimefika mapema, lakini bado sijahudumiwa," alisema mmoja wa wagonjwa waliozungumza na mwandishi wa habari.
Arusha
Katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, huduma zimedorora lakini Mganga Mkuu, Dk Omar Chande alisema jana kuwa, imekuwa ni vigumu kuchukua hatua kuwabana madaktari ambao wanatuhumiwa kufanya mgomo baridi, kwani wote wanaripoti kazini.

"Ni kweli kuna taarifa hizi za kuwapo mgomo baridi, lakini madaktari wote wapo kazini, ila kama kuna kufanya kazi chini ya kiwango, tumeanza uchunguzi," alisema Dk Chande.
Amana

Katika Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam utoaji wa huduma ulisuasua kutokana na mgomo huo jambo lililofanya uongozi kuweka tangazo kwenye Ofisi ya Mganga Mkuu kuwataka watumishi wote ambao hawakuwapo kazini kuanzia Juni 25, 2012 waandike barua za kurejea kazini.

Tangazo hilo pia linawataka madaktari walioko mafunzoni kuandike barua kwenda kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia kwa mganga mkuu wa hospitali hiyo.


Habari hii imeandaliwa na Frederick Katulanda, Mwanza, Rehema Matowo, Moshi, Zakhia Abdallah (SJMC), Editha Majura, Israel Mgussi, Dodoma), Victoria Mhagama na Daniel Mwingira, Sam Jacob na Issa lazaro (SJMC, Godfrey Kahango, Mbeya, na Mussa Juma, Arusha.
Via www.mwananchi.co.tz

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate