EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, July 6, 2012

MPAMBANO WA NGUMI UWANJA WA TAIFA: WEMA NIMEKWIVA


MSANII wa filamu, Wema Sepetu ambaye anatarajiwa kuchapana makonde na Jacqueline Wolper katika pambano la utangulizi kesho, amesema sasa amekwiva na yuko fiti kutokana na mazoezi ambayo anapewa na kocha wake Rashidi Matumla.
Akizunguza na gazeti hili jana, Wema alisema ametumia muda mwingi katika mazoezi hivyo kesho ni lazima atampiga Wolper kwa ‘knock out’.
“Kwa kweli nimejifua vilivyo lengo likiwa ni kuhakikisha naweka historia kesho ya kumchakaza Wolper, kwa nilivyo fiti sidhani kama atafikisha raundi ya pili,” alisema Wema.
Wakati Wema akisema hayo, Wolper amejigamba kwa kusema: “Wema ajiandae tu kwa kipigo, ameshasema mengi ila mimi siku hiyo nataka nimfundishe adabu. Nitamvuruga, nitampiga na kwa uzito wa ngumi nitakazomtupia asipotoka manundu labda awe amechanjia.”
Warembo hao wamesema kuwa wanapigana kumaliza ubishi wa muda mrefu, vilevile kuchangia fedha Mamlaka ya Elimu Tanzania ili kuwasaidia wanafunzi wa kike kupata mabweni na kusoma katika mazingira mazuri.
Mratibu wa tamasha hilo, Luqman Maloto amesema kuwa Wolper na Wema kila mmoja anatamba kumpiga mwenzake, hivyo akataka mashabiki wao kuhudhuria Uwanja wa Taifa ili kumuona mbabe kati ya wawili hao.
“Tumekubaliana kwa kufuata misingi yote. Wolper na Wema wameridhia kupambana ili kumaliza ubishi na kuchangia elimu,” alisema Luqman na kuongeza:
“Wolper na Wema wataingia uwanjani kwa helikopta. Tunatambua thamani ya Wema na Wolper kijamii, kwa hiyo hatutaki wapitie njia ambazo zitawafanya watoe kisingizio. Tutawaingiza kwa helikopta, kila mtu na ya kwake ili watakapokuwa wanaingia, uwanja mzima ushuhudie.”
Luqman aliendelea kusema kuwa pambano la Wema na Wolper litakuwa la utangulizi, kabla ya mabondia wakubwa nchini, wenye rekodi nzito, Japhet Kaseba na Francis Cheka kupambana kwenye pambano la kumaliza ubishi.
“Kama nilivyokwishasema kabla, siku ya Tamasha la Usiku wa Matumaini ni nzito. Matukio ni mengi, vilevile kutakuwa na mechi ya wabunge Simba na Yanga, Bongo Fleva dhidi ya Bongo Movie, bila kusahau siku hiyo tutajua mkali wa steji ni nani kati ya Jose Chameleone wa Uganda na Diamond Platnamz wa Tanzania.
“Kutakuwa na shoo nyingine kali kutoka kwa Roma, Chidi Benz, Juma Nature, Pah One, FM Academia, East African Melody na wengine wengi,” alisema.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate