EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 2, 2012

Siri ya Benki ya Twiga Bancorp kufanikiwa kupata tuzo Geneva yaanikwa

 Afisa Mtendaji Mkuu wa Twiga Bancorp Limited, Hussein Mbululo (kulia) akifafanua jambo juu ya Tuzo ya Dhahabu waliyo ipata kutoka Geneva Uswis kwa Ubora wa huduma zao, kwa waandishi wa Habari waliotembelea banda la Benki hiyo katika maonesho ya kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam yanayoendelea katika viwanja vya JK Nyerere maarufu Saba Saba barabara ya Kilwa. Pamoja ni wafanyakazi wa Benki hiyo waliopo viwanjanani hapo.
SIKU chache baada ya kupokea Tuzo ya dhahabu ya Kimataifa ya utoaji bora wa huduma, Benki inayomilikiwa na Serikali ya Twiga Bancorp, imeweka hadharani siri ya kupewa tuzo hiyo inayojulikana kama Century International Gold Quality ERA.


Benki ya Twiga Bancorp ilikabidhiwa tuzo hiyo karibuni na Kampuni ya Kimataifa ya Business Initiative Directions jijini Geneva Uswis.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo, Hussein Mbululo, alisema huduma ya moneygram inayowezesha Watanzania na watu wa mataifa mengine kutuma fedha nje kwa dakika chache imechangia kuiwezesha benki hiyo kushinda tuzo hiyo.


Tuzo hiyo kwa Benki ya Twiga Bancorp imekuja siku chache baada ya Serikali kupitia kwa Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk. William Mgimwa kuliambia Bunge kwamba Serikali ipo mbioni kuziongezea mtaji benki zake ikiwemo Benki ya Twiga ili kuziwezesha kuboresha huduma zake. Benki nyingine ni Benki ya Wanawake (TWB), Benki ya Posta (TPB) na Benki ya Rasilimali (TIB).


Mbululo alisema huduma nyingine iliyoiwezesha benki hiyo kushinda tuzo hiyo ni utoaji wa mikopo kwa wafanyakazi bila kuwalazimu wafanyakazi hao kuwa na akaunti katika Benki ya Twiga hatua ambayo imewezesha wafanyakazi nchi nzima hata mahali kusiko na benki hiyo kunufaika na mikopo hiyo.
“Walieleza kuridhishwa na huduma zetu kufikia kiwango cha ubora wa juu lakini pia walieleza kuridhishwa na ubunifu tunaoendelea kuufanya katika kuboresha huduma za kibenki nchini ukilinganisha na benki nyingine.


Kupitia huduma za Money gram mtu anaweza kumtumia fedha za ada au dawa kwa mwenzake aliyepo Uingereza au Marekani na akaweza kuzipata ndani ya dakika tano tu jambo ambalo limewavuta watu wengi kutumia benki yetu,” alisema Mbululo.


Alisema benki hiyo pia imetoa mchango mkubwa katika maendeleo ya Benki Kata za Jamii (VICOBA) katika maeneo mbalimbali hapa nchini hatua ambayo imewezesha kupewa nishani ya kuwa mlezi bora wa VICOBA nchini na kupewa tuzo.Hadi sasa Benki hiyo inahudumia vikundi zaidi ya 150 vya VICOBA.
Alisema benki hiyo inayoendelea kujitanua kwa kufungua tawi moja mkoani kila mwaka, hivi karibuni itafungua tawi jipya mkoani Dodoma na hivyo kuifanya kuwa na matawi Dar es Salaam, Arusha, Mwanza na Dodoma, huku tawi la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam, likiendelea kuvunja rekodi ya kufunguliwa kwa saa 24 kwa siku zote saba za wiki.


Alisema mtandao wa huduma kwa benki hiyo umeimarika kutokana na kadi zake za ATM kuweza kuunganishwa na Mtandao wa Umoja wenye kuzihusisha benki zaidi ya 24, zikiwa na mtandao wa zaidi ya ATM 160 nchi nzima.


Kuhusu mtaji utakaongezwa na serikali kwa benki hiyo, Mbululo alisema fedha hizo zitasaidia kuboresha huduma za benki hiyo kwa kuwezesha kujenga matawi mapya, kununua mashine na kununua kompyuta na vifaa vyake ili kutanua zaidi huduma zake na kuwezesha kuwafikia wananchi wengi.


 Afisa Mwandamizi, Mwendeshaji, Lydia Matembele akitoa maelezo kwa vijana waliotembelea banda lao katika maonesho ya Kimaifa ya Biashara maarufu saba saba .
 Banda la Twiga Bank lipo kando ya lango kuu la Kuingilia Karume Hall.
 Benki ya Twiga Bancorp inatoa huduma ya kuweka na kuchukua fedha dirishanai au katika ATM yake iliyopo viwanja vya Sabasaba kama mmoja wa wateja wa Umoja Switch anavyofanya.
 Mkuu wa Uendeshaji Richard Kombole (kulia)akizungumza na mteja nje ya Banda lao
Afisa Mwandamizi, Mwendeshaji, Lydia Matembele akimsikiliza Mfanya Biashara, Yahia Idriss wa Kampuni ya Giad Sewedy Cables ya Nchini Sudan alipofika kupata huduma ya kubadilishiwa fedha katika Banda hilo la Maonesho linalofanya huduma kamili za Kibenki.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate