EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, July 20, 2012

Ushindani CCM, Chadema sasa umevuka mipaka

KWAMBA mwishoni mwa wiki iliyopita vurugu kubwa zilitokea  kwenye mkutano wa hadhara zikiwahusisha wafuasi wa Chadema na CCM zimesababisha kifo cha mtu mmoja katika Kata ya Ndago, wilayani Iramba, mkoani Singida hakika ni habari za kusikitisha sana.
 
Tunaambiwa kwamba katika vurugu hizo, wafuasi wa vyama hivyo vikuu vya siasa nchini walishambuliana kwa kutumia silaha za jadi, ikiwamo mawe wakati wa mkutano wa hadhara uliokuwa ukihutubiwa na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika na kusababisha kifo cha Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (UV-CCM) wa kata hiyo ya Ndago, Yohana Mpinga.
 
Jeshi la Polisi mkoani Singida limethibitisha kutokea kwa vurugu hizo na kifo cha mwenyekiti huyo wa UV-CCM na kusema kwamba linawashikilia watu 18 wa kata hiyo kwa mahojiano na watakaobainika kuhusika na ghasia hizo watafikishwa mahakamani, huku likiendelea na msako wa kuwatafuta watu wengine waliohusika katika tukio hilo.
 
Mpaka sasa wafuasi wa vyama hivyo bado wanatupiana lawama ambazo hazijaweza kuthibitishwa na mamlaka husika, lakini polisi wanadai kwamba baadhi ya wafuasi wa CCM waliokuwapo katika mkutano huo  waliwarushia mawe wafuasi wa Chadema kwa madai kwamba viongozi wao waliokuwa wakihutubia mkutano huo walikuwa wakitoa kauli za kumkashifu Mbunge wao wa jimbo hilo la Iramba Magharibi, Mwingulu Nchemba (CCM).
 
Pamoja na kwamba hatuna mamlaka ya kutoa hukumu kuhusu upande unaopaswa kulaumiwa kwa kusababisha vurugu hizo, kwa ujumla wetu tunalazimika kulaani vurugu hizo kwa nguvu zetu zote. Vyama hivyo viwili vimekuwa na uadui na mvutano mkubwa kati yao kwa muda mrefu sasa, hivyo kusababisha uvunjifu wa amani kutokana na vitendo vya kuhujumiana na kudhoofishana kisiasa ambavyo vimezaa ushindani kati yao tunaoweza kusema umevuka mipaka kwa kiwango chochote kile.
 
Hali inakuwa mbaya zaidi uhasama huo unapovuka mipaka kutoka uhasama wa kisiasa kati ya vyama hivyo hadi uhasama kati ya mbunge na mbunge. Sote ni mashuhuda wa uhasama kati ya wabunge hao wawili ambao ulikolezwa hivi karibuni na mbunge huyo wa Ubungo baada ya kumtuhumu bungeni mwenzake wa Iramba Magharibi kwamba ni mmoja wa watuhumiwa waliokwapua fedha za EPA.
 
Pamoja na kukosa ushahidi wa kutosha kuthibitisha madai hayo kama alivyoamuriwa na Bunge, mbunge huyo wa Ubungo aliamua kupeleka mashtaka kwa wapigakura wa hasimu wake huyo mwishoni mwa wiki iliyopita kwa kuhutubia mkutano wa hadhara ambao ulipigwa mawe na wafuasi wa mshindani wake huyo katika Jimbo la Iramba Magharibi. Wakosoaji wa mbunge huyo walisema haikuwa wakati mwafaka wala busara kwake kumkandia hasimu wake kwenye jimbo lake hilo la Iramba Magharibi, lakini Mbunge Mnyika anadai kwamba mbunge huyo ndiye aliyeanzisha uchokozi kwa kumwaga fitina kwa wapigakura wake katika jimbo lake la Ubungo hivi karibuni na kusema hatua yake hiyo ililenga kulipiza kisasi.
 
Wapo watu wanaodai kwamba waliovurumisha mawe katika mkutano wa mbunge huyo wa Ubungo walitumwa na Mbunge Mwingulu Nchemba. Lakini kama tulivyosema hapo awali, hakuna tuhuma ambazo zimethibitishwa hadi hivi sasa, licha ya ukweli kwamba siyo sisi wala watu wanaotoa tuhuma kwa pande hizo mbili walio na mamlaka ya kisheria kutoa hukumu. Kwa maneno mengine, tuziachie mamlaka husika siyo tu zifanye uchunguzi  ulio huru, bali pia zitoe uamuzi wa haki na usioacha shaka yoyote.
 
Hata hivyo, tukio hilo la Singida lazima lizifumbue macho mamlaka zote zinazohusika katika kusimamia na kuratibu shughuli za vyama vya siasa. Ndiyo maana moja ya maswali magumu yanayoulizwa kuhusu vurugu hizo za Singida ni hili: Ilikuwaje mkutano huo wa hadhara wa Chadema uliokuwa na kibali cha Jeshi la Polisi haukupewa ulinzi wa kutosha?

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate