CHAMA CHA WALIMU TANZANIA (CWT)
(Tanzania Teachers’ Union – TTU)
MKOA WA MBEYA
P.O. Box 3079, MBEYA
E-mail: ttumbeyareg@yahoo.com
Telephone: 2502535, Cell: 0784-830564, 0715-830564, 0764-163234
(Tanzania Teachers’ Union – TTU)
MKOA WA MBEYA
P.O. Box 3079, MBEYA
E-mail: ttumbeyareg@yahoo.com
Telephone: 2502535, Cell: 0784-830564, 0715-830564, 0764-163234
Your
Ref: ............................................
Date: 21/8/2012
Our Ref: CWT/MBY/MW/VOL.II/57
MKUU WA WILAYA,
S.L.P 255,
MBEYA
YAH: Kuwakashifu walimu na CWT wakati wa semina za sensa ya watu na makazi
Tafadhali husika na mada tajwa hapo juu.
Chama cha Walimu Tanzania (CWT) mkoa wa Mbeya kwa masikitiko sana kimepokea toka kwa walimu malalamiko juu yako kuhusiana na jinsi ulivyowakashifu wakati wa zoezi la semina za sensa ya watu na makazi. Kwa nyakati tofauti, ulipita kwenye vituo vya semina hizo ambazo wengi walikuwa walimu na kutoa kashifa dhidi ya walimu na taaluma yao pamoja na CWT. Baadhi ya kashifa ambazo ulitoa ni kama ifuatavyo:-
Kwa mantiki hiyo, walimu wametafakari na kuona kuwa kauli hizo ulizotoa kwao tena wakiwepo washiriki wengine wasio walimu zimewadhalilisha, kuwafadhaisha na kuwafanya wadhaulike kwenye jamii na hivyo kuathirika kisaikolojia. Aidha, CWT kimeona kuwa ulikuwa na lengo la kuvuruga zoezi zima la sensa ya watu na makazi kwani uliondoa utulivu wa
washiriki wa semina na kuwafanya wajadili zaidi juu ya kauli zako zenye kila aina ya maudhi. CWT hakiwezi kuvumilia viongozi wa serikali wa aina hii wasioheshimu na kuthamini walimu waliowafundisha na waliopewa dhamana ya kuelimisha umma wa nchi hii. Aidha, CWT kinajiuliza kama ulipoteuliwa kuwa Mkuu wa wilaya ya Mbeya ulitumwa kuja kuwakashifu walimu? Je, ulitumwa kuja kuwakosanisha walimu na CWT yao? Je, sera unazotekeleza kweli ni za Chama tawala au ni za kwako mwenyewe? CWT kinaamini kuwa hayo ni matumizi mabaya ya madaraka kwani hakuna anayeweza kukutuma hayo. Kutokana na kashifa hizo kwa walimu na chama chao unatakiwa ufanye yafuatayo ili warudishe moyo wa kuendelea kukuamini:-
Nakujulisha kuwa, kama utashidnwa kufanya hayo matatu juu, CWT kitaingia kwenye hatua nyingine zaidi kwani walimu walioathirika na kauli hizo wako tayari kwa hatua yoyote itakayochukuliwa na CWT.
Nakutakia kazi njema.
Mwl. Kasuku Bilago
Katibu CWT Mkoa
Mbeya
Nakala:
1) Waziri Mkuu
S.L.P 980
Dodoma
2) Katibu Mkuu CWT
S.L.P 61110
Dar es Salaam
3) Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma
S.L.P 4865
Dar es Salaam
4) Mkuu wa Mkoa
S.L.P 754,
Mbeya
5) Makatibu CWT (W)
Mkoa wa Mbeya
nakala hii imepatikana via blogu ya Kalulunga
Our Ref: CWT/MBY/MW/VOL.II/57
MKUU WA WILAYA,
S.L.P 255,
MBEYA
YAH: Kuwakashifu walimu na CWT wakati wa semina za sensa ya watu na makazi
Tafadhali husika na mada tajwa hapo juu.
Chama cha Walimu Tanzania (CWT) mkoa wa Mbeya kwa masikitiko sana kimepokea toka kwa walimu malalamiko juu yako kuhusiana na jinsi ulivyowakashifu wakati wa zoezi la semina za sensa ya watu na makazi. Kwa nyakati tofauti, ulipita kwenye vituo vya semina hizo ambazo wengi walikuwa walimu na kutoa kashifa dhidi ya walimu na taaluma yao pamoja na CWT. Baadhi ya kashifa ambazo ulitoa ni kama ifuatavyo:-
- Ulikuwa ukieleza kuwa walimu ni kada ya waliofeli mitihani na hivyo serikali inawashangaa kudai waongezewe mishahara.
- Ulieleza kuwa walimu wamejaa madudu kichwani.
- Ulieleza kuwa walimu ni manjuka yaani watu mbumbumbu wasiojua kitu chochote.
- Ulikuwa ukiwaeleza walimu kuwa Mukoba (Rais wa CWT) anamiliki pesa nyingi toka CWT hivyo hata akigoma na kufukuzwa kazi hatapata shida yoyote ya maisha, hivyo anawadanganya walimu wanaogoma.
- Ulikuwa ukieleza kuwa CWT kinawanufaisha makatibu na viongozi kuliko walimu maana wao wanatembelea magari kwa pesa zenu na hivyo ni kwa nini walimu waigomee serikali badala ya kukigomea chama chao cha CWT.
- Ulikuwa ukieleza kuwa washiriki wa semina hawatakiwi kuugua, kufa wala kufiwa kabla ya zoezi la sensa kuisha ila baada ya sensa wanaruhusiwa kuugua, kufa na kufiwa maana serikali haitakuwa na hasara yoyote.
Kwa mantiki hiyo, walimu wametafakari na kuona kuwa kauli hizo ulizotoa kwao tena wakiwepo washiriki wengine wasio walimu zimewadhalilisha, kuwafadhaisha na kuwafanya wadhaulike kwenye jamii na hivyo kuathirika kisaikolojia. Aidha, CWT kimeona kuwa ulikuwa na lengo la kuvuruga zoezi zima la sensa ya watu na makazi kwani uliondoa utulivu wa
washiriki wa semina na kuwafanya wajadili zaidi juu ya kauli zako zenye kila aina ya maudhi. CWT hakiwezi kuvumilia viongozi wa serikali wa aina hii wasioheshimu na kuthamini walimu waliowafundisha na waliopewa dhamana ya kuelimisha umma wa nchi hii. Aidha, CWT kinajiuliza kama ulipoteuliwa kuwa Mkuu wa wilaya ya Mbeya ulitumwa kuja kuwakashifu walimu? Je, ulitumwa kuja kuwakosanisha walimu na CWT yao? Je, sera unazotekeleza kweli ni za Chama tawala au ni za kwako mwenyewe? CWT kinaamini kuwa hayo ni matumizi mabaya ya madaraka kwani hakuna anayeweza kukutuma hayo. Kutokana na kashifa hizo kwa walimu na chama chao unatakiwa ufanye yafuatayo ili warudishe moyo wa kuendelea kukuamini:-
- Uwaombe radhi walimu ndani ya siku 7 kwa kila kituo cha semina ya sensa na makazi ya watu ulichopita na kutoa kauli hizo.
- Umuombe radhi Rais wa CWT mwl. Gratian Mukoba ndani ya siku 7, uliyedai amejiulimbikizia fedha za CWT.
- Uwaombe radhi makatibu na viongozi wa CWT ndani ya siku 7 uliodai wanajinufaisha na CWT kuliko kuwanufaisha walimu.
Nakujulisha kuwa, kama utashidnwa kufanya hayo matatu juu, CWT kitaingia kwenye hatua nyingine zaidi kwani walimu walioathirika na kauli hizo wako tayari kwa hatua yoyote itakayochukuliwa na CWT.
Nakutakia kazi njema.
Mwl. Kasuku Bilago
Katibu CWT Mkoa
Mbeya
Nakala:
1) Waziri Mkuu
S.L.P 980
Dodoma
2) Katibu Mkuu CWT
S.L.P 61110
Dar es Salaam
3) Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma
S.L.P 4865
Dar es Salaam
4) Mkuu wa Mkoa
S.L.P 754,
Mbeya
5) Makatibu CWT (W)
Mkoa wa Mbeya
nakala hii imepatikana via blogu ya Kalulunga
No comments:
Post a Comment