EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, August 25, 2012

Polisi, wanaopinga Sensa wavutana

WAKATI baadhi ya taasisi za Kiislamu nchini zikitofautiana kuhusu ushiriki katika Sensa ya Watu na Makazi inayoanza kesho, Jeshi la Polisi limesema litawachukulia hatua za kisheria watakaobainika kusababisha kuvurugika kwa shughuli hiyo ya kitaifa.
Kwa nyakati tofauti jana, taasisi hizo na polisi walitoa matamko yao, ikiwa ni siku moja kabla ya kuanza kwa Sensa ya Watu na Makazi iliyopangwa kufanyika kwa wiki nzima kuanzia kesho.

Mkuu wa Mafunzo na Operesheni wa Polisi, Paul Chagonja alisema jeshi hilo limebaini kuwa baadhi ya taasisi na makundi ya watu yanawashawishi wananchi kutoshiriki Sensa kwa manufaa yao binafsi.
Kwa upande wake, Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu Tanzania kupitia kwa Katibu Mkuu wake, Sheikh Ponda Issa Ponda alisema kuwa wataitisha maandamano ili kudhihirisha msimamo wao wa kugoma kushiriki Sensa ya Watu na Mkazi.

Hata hivyo, Jumuiya ya Kuendeleza Quran na Sunna Tanzania (Juqusuta), kupitia kwa Kaimu Mwenyekiti wake, Sheikh Mohamed Said imeitaka Serikali kupuuza wanaopinga Sensa na kutojishughulisha na vipeperushi vinavyosambazwa kuzuia watu wasishiriki.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari jana, Kamishna Chagonja alisema tayari baadhi ya watu wamekamatwa kwa tuhuma za kuvuruga mchakato wa kazi hiyo.
“Hatutawavumilia hata kidogo watu watakaobainika kuwashawishi wananchi wasishiriki Sensa kwa namna yoyote, iwe kwa maneno au kuwarubuni kwa fedha,” alisema.
Alionya kuwa yeyote watakayembaini akijihusisha kwa namna yoyote ile na vitendo vinavyoashiria kuvunjika kwa amani au kuathiri mchakato wa Sensa, atashughulikiwa na vyombo vya dola.

Mkoa wa Dar es Salaam
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki alisema: “Nasikitishwa na makundi haya ya watu ambayo yanahamasisha wengine wasihesabiwe. Nawataarifu kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa sababu kitendo hicho ni kinyume na sheria za takwimu.”
Alisema hadi jana, maandalizi yote yalikuwa yameshakamilika na makarani wote walioteuliwa kwa kazi hiyo wameshalipwa posho zao za semina.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda alisema wenyeviti wa Serikali za Serikali Mitaa watalipwa Sh100,000 kusaidia kufanikisha Sensa.
Mwenda alitoa kauli hiyo baada ya kuwapo kwa tishio la wenyeviti hao kugoma. Alisema Ofisi ya Taifa ya Takwimu imetoa Sh50,000 na nusu nyingine itatolewa na manispaa hiyo.

Msimamo wa Sheikh Ponda
Sheikh Ponda alisema Dar es Salaam jana kuwa maandamano hayo yatafanyika Agosti 29, mwaka huu kupinga pamoja na mambo mengine, Serikali kutumia nguvu ya ziada dhidi ya msimamo wao huo.
Awali, alisoma tamko la Jumuiya hiyo na kuwasisitiza Waislamu kutoshiriki Sensa, huku akiitaka Serikali kuiahirisha ili kuepusha matumizi mabaya ya fedha za umma.
Alitaja sababu nne jumuiya hiyo kugomea Sensa kuwa ni kugubikwa na propaganda na matumizi ya mabavu na Serikali kushindwa kujenga mazingira rafiki yakufanyika kwake.
Kuhusu maandamano, alisema yanatarajiwa kushirikisha wakazi wa mikoa saba nchini ambayo aliitaja kuwa ni Tabora, Mwanza, Arusha, Pwani, Morogoro, Dar es Salaam na Dodoma.
Alisema Dar es Salaam, maandamano hayo yataanzia katika misikiti yote iliyopo Kariakoo kuelekea Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).

Juqusuta wapuuza
Makamu Mwenyekiti wa Juqusuta, Sheikh Hassan Kabeke alisema vipeperushi hivyo vinaonyesha namba za simu hivyo polisi izitumie kuwasaka wahusika akisema hizo ni ushahidi tosha wa kutiwa hatiani kwa wahusika.
Sheikh Kabeke alisema Uislamu ni dini ya amani na kwamba kuna watu wanaoutumia kama mtaji wa kujipatia umaarufu na kuwataka Waislamu kukataa kutumiwa na watu kwa kivuli cha Uislamu kwa masilahi binafsi ya watu.
“Kuna watu wamefikia hatua ya kuwataka Waislamu kufunga siku tatu baada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kumalizika kwa lengo la kuwalaani wenzao atakaoshiriki Sensa. Nakuonyeni kuwa huu ni uzushi mkubwa...” alieleza.

Maalim Seif atoa wito
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad amewataka Waislamu kushiriki Sensa na kuacha kulalamika kwani msingi wa malalamiko yao ni utengano baina yao hivyo kushindwa kufanya mambo ya maendeleo kama ilivyo kwa waumini wa dini nyingine.
Akizungumza baada ya Ibada ya Ijumaa katika Msikiti wa Mtoro, Dar es Salaam jana, Maalim Seif alisema Waislamu walio wengi ni wanafiki na wapo ambao wanaona haya hata kujitambulisha mbele ya hadhira jambo ambalo haliwezi kuwasaidia zaidi ya kuwafanya wabakie walipo.
“Mtanisamehe ila lazima niseme jambo hili. Wengi wetu ni wanafiki, kuna ambao hawawezi hata kutamka hadharani kuwa wao ni Waislamu,” alisema Maalim Seif na kuongeza:
“Nawaomba masheikh mwondoe hali hiyo ili kuleta tija na maendeleo ya Waislamu nchini.”

Mkoa wa Mwanza
Wenyeviti wa Serikali za Mitaa wa Mkoa wa Mwanza jana walitoa tamko la kutokushiriki Sensa kwa madai kuwa hawajashirikishwa kikamilifu.
Aidha, walisema wamesikitishwa na dharau iliyofanywa na waratibu wa Sensa kwa kuwapa posho ya Sh50,000 kwa siku zote tisa ambazo watakuwa wanafanya kazi kwa kushirikiana nao.
Kiongozi wa wenyeviti hao, Hamisi Shindo alisema jana katika ukumbi wa UTPC, Mwanza kwamba walifikisha malalamiko kwa wahusika, lakini hakuna hatua zilizochukuliwa.
“Tuliwaandikia barua Agosti, 22 mwaka huu na kuwapelekea lakini wameshindwa kutujibu na tulipomwuliza mkuu wa mkoa alijibu kuwa Ofisi ya Takwimu imesema haina fedha za kuwalipa wenyeviti wa mitaa,” alisema Shindo.

Mkoa wa Tanga
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa amesema ofisi yake imekamilisha maandalizi Sensa ya Watu na Makazi na akawataka wananchi kutoa ushirikiano kwa makarani wanaoandikisha .
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Gallawa alionya kuwa atakayeivuruga shughuli hiyo atachukuliwa hatua za kisheria.
Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu amekuwa akihamasisha wananchi kujitokeza katika Sensa ya Watu na Makazi kwa kupita nyumba kwa nyumba usiku. Pia amekuwa akipita katika masoko mbalimbali yaliyopo wilayani hapa kuwahamasisha wafanyabiashara ili wajitokeze katika kuhesabiwa.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego amewataka   wakazi wake kutambua kuwa Sensa haina uhusiano na itikadi za kidini.

Akizungumza na wenyeviti wa mtaa na vitongoji wa Wilaya   ya Tanga jana, Dendego alisema lengo la Sensa ni kuwezesha kupatikana kwa takwimu sahihi ambazo  zitatumika kwa ajili ya kupanga maendeleo.
Wilayani Korogwe, madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo, wameazimia kufuata kanuni, sheria na taratibu ili kuhakikisha wanawahamasisha wananchi kuhesabiwa.
Mwenyekiti wa Wajumbe wa Baraza la Madiwani, Sadick Kallaghe alisema madiwani kwa kutumia nafasi zao watashirikiana kikamilifu na wananchi ili kukamilisha mchakato huo unaotarajiwa.

Habari hii imeandikwa na Aidan Mhando, Florence Majani, Joseph Zablon Elizabeth Edward, Fidelis Butahe, Frederick Katulanda, Mashaka Kibaya, Korogwe, Raisa Saidi, Tanga na Sheilla Sezzy, Mwanza.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate