Rais
Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akiagana na Rais John Dramani Mahama wa
Ghana nyumbani kwake jijini Accra jana Agosti 11, 2012 baada ya
kumtembelea na kumpa pole ya msiba wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo
Marehemu John Evans Atta Mills aliyezikwa juzi.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Rais John Dramani
Mahama wa Ghana nyumbani kwake jijini Accra jana Agosti 11, 2012
wakati alipomtembelea kiongozi huyo mpya wa Ghana na kumpa pole ya
msiba wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Marehemu John Evans Atta Mills.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akitazama mananasi yakitayarishwa kwa ajili ya
kusafirishwa na kuuzwa nje ya nchi katika kiwanda cha Bomarts Farms Ltd
katika kitongoji cha Dobro nje kidogo ya jiji la Accra jana Agosti 11,
2012.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitazama ukulima wa kisasa wa mananasi
yanayolimwa kwa ajili ya kuuzwa nje ya nchi katika shamba la Bomarts
Farms Ltd katika kijiji cha Dobro katika eneo la Nsawam nje kidogo ya
jiji la Accra jana Agosti 11, 2012. Kulia kwake ni Mtendaji Mkuu wa
shamba hilo Bw. Anthony Botchway na mwenye suti ya bluu ni Waziri wa
Chakula na Kilimo, Mhe. Kwesi Ahwol.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia upandaji wa miche ya mananasi katika
shamba la Koranco kijiji cha Obotweri nje kidogo ya jiji la Accra. Kulia
kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Koranco Farms Ltd, Bw Emmanuel B. Koranteng
ambaye amekuwa akilima shamba la matunda kwa miaka 27. Mwalimu Nyerere
aliwahi kumtembelea shambani hapo katikati ya miaka ya 1980 kujionea
ukulima huo wa matunda.
(PICHA NA IKULU)
(PICHA NA IKULU)
No comments:
Post a Comment