EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, August 19, 2012

Watu zaidi ya milioni 34 wanaishi na VVU Duniani

 
Takwimu zinaonyesha kuwa kwa mwaka 2011 zaidi ya watu milioni 34 ulimwenguni wanaishi na maambukizi  ya Virusi vya ugonjwa wa Ukimwi (VVU) kati ya hao  milioni 30.7  watu wazima, milioni 16.7 wanawake  na milioni 3.4 watoto wenye  umri wa chini ya miaka 15.
Hayo yamesemwa jana na   Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Kupambana na Ugonjwa wa Ukimwi (UNAIDS) Dkt. Raul de Melo Cabral wakati akiongea na wake wa wakuu wa nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) waliohudhuria mkutano wa  kuzuia maambukizi ya virusi vya Ugonjwa wa Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kwa maendeleo ya kanda unaofanyika Maputo nchini Msumbiji.
Dkt. Cabral alisema kuwa  ugonjwa wa Ukimwi utaendelea kuwa changamoto kwa nchi zote na kila mtu anatakiwa kupambana  nao ndiyo maana katika Azimio la  Kisiasa  lililofanyika mjini New York mwaka 2011 wakuu wa nchi zote wanachama wa Umoja wa Mataifa  (UN)  wakiwemo wa SADC walipitisha malengo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua zaidi katika kupambana na ugonjwa huo.
“Walikubaliana kuwa  ifikapo  mwaka 2015 wawe wamepunguza nusu ya maambukizi  ya ugonjwa huo katika nchi zao, kupunguza maambukizi mapya kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto,  kutoa matibabu  kwa watu milioni 15 katika nchi zote wanachama wa umoja huo wanaoishi na VVU  na kuongeza  bajeti  katika masuala yanayohusiana na afya”, Alisema.
Akichangia mada katika mkutano huo Mke wa Rais ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete alisema kuwa ni jambo jema kwa wake wa viongozi wa SADC kuwa na mfumo mzuri wa utendaji kazi ambao  utawawezesha kufanya mambo  yatakayokuwa na tija katika kanda  na kuweza kuwasaidia wanawake  na watoto  ambao kwa kiasi kikubwa wameachwa nyuma kimaendeleo.
“Sisi kama wanachama tunatakiwa kutengeneza  mpango mkakati na kuona jinsi gani unaweza kujitoa  ili kuweza kutimiza  malengo tuliyojiwekea  ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto yanapungua  au kutokuwepo  kabisa katika  jamii inayotuzunguka”, alisema Mama Kikwete.
Aliendelea kusema kuwa pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo kuwasaidia rasilimali ambazo wanazifanyia kazi kila siku wao pia wanajukumu kubwa la kuhakikisha kuwa wanachangia  kwa kiasi kikubwa ili waweze kutimiza malengo waliyojiwekea.
 Kwa upande wake Mke wa Rais wa Zambia ambaye pia ni Mwenyekiti  wa Umoja wa wake wa Marais wa  Afrika wa Kupambana na Ugonjwa wa Ukimwi (OAFLA) Dkt. Christine Kaseba Sata alisema kuwa  hivi sasa nchi za SADC zinafanya jitihada kubwa ya kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (MTCT) baada ya kugundua kuwa ugonjwa huo ni wa hatari si tu kwa watu wanaoishi na ugonjwa huo  bali hata kwa watoto wanaoupata kutoka kwa mama zao.
Dkt. Sata alisema kuwa Ugonjwa wa Ukimwi unatishia maisha ya watu  kwa kizazi kilichopo na kijacho kwani watoto wengi wanaozaliwa kama watakuwa na maambukizi  hawataweza kuishi muda mrefu, ugonjwa huo unaharibu familia, kupunguza uzalishaji na uchumi  katika ngazi ya familia na kutokuwa  na kizazi kisichokuwa na urithi kwa kizazi kijacho.
“Licha ya kupambana na ugonjwa wa Ukimwi changamoto nyingine tunayokabiliana nayo  ni ya kuenea kwa kasi kwa ugonjwa wa shingo ya kansa ya kizazi na matiti kwa wanawake wengi katika nchi wanachama wa Umoja wa SADC, wanawake  hawa wanakufa kwa ugonjwa  ambao unaweza kuzuilika na kutibika kama mgonjwa atapata matibabu mapema” , Dkt.Banda alisema,
Aliendelea kusema kuwa wanawake wengi wanakufa kwa kukosa uelewa kuhusiana na ugonjwa huo , kutofanyiwa uchunguzi na kupata huduma za matibabu mapema  na kuwashauri wake hao wa viongozi kufanya kazi kwa ukaribu na Serikali ya nchi zao  jambo ambalo litawafanya  watu  wengi zaidi kuwa na ufahamu kuhusiana na ugonjwa huo.
Mkutano huo wa siku mbili  wenye kaulimbiu isemayo kuondoa maambukizi ya Ugonjwa wa ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto  inawezekana  unahudhuriwa na wake mbalimbali wa wakuu wa nchi  wanachama wa SADC akiwemo mke wa Rais Mama Salma Kikwete

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate