EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, September 5, 2012

Kesi ya Rais wa MAT, Dkt. Mkopi: Upelelezi umekamilika, mashitaka kusomwa 27.09.2012

Rehema Mohamed, Majira, Dar es Salaam -- Upande wa mashtaka umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa, upelelezi wa kesi inayomkabili Rais wa Chama cha Madaktari (MAT), Dkt. Namala Mkopi, umekamilika.

Wakili wa Serikali Bi. Wila Ahoga, alidai hayo mahakamani hapo jana wakati kesi hiyo ilipoletwa kwa ajili ya kutajwa mbele ya hakimu Bw. Faisal Kahamba.

Alidai kuwa, kutokana na upelelezi huo kukamilika anaiomba Mahakama hiyo ipange tarehe ya kumsomea mshtakiwa maelezo ya awali ambapo Hakimu Kahamba, alipanga Septemba 27 mwaka huu.

Katika kesi hiyo, Dkt. Mkopi anakabiliwa na mashitaka mawili, likiwemo la kutotii amri ya mahakama ya kuzuia mgomo wa madaktari na uhamasishaji mgomo kinyume cha sheria.

Upande wa mashitaka ukiongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Tumaini Kweka, akisaidiana na Ladslaus Komanya, ulidai kati ya Juni 26 na 28 mwaka huu, jijini Dar es Salaam, mshtakiwa akiwa Rais wa MAT, hakutii amri iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kitengo cha Kazi, Juni 26, mwaka huu.

Ilidaiwa kuwa, amri hiyo ilimtaka Dkt. Mkopi kuwatangazia wanachama wake kwamba wamezuiwa kushiriki mgomo kama amri ya awali iliyotolewa na Mahakama hiyo, Juni 22 mwaka huu.

Shitaka la pili, ilidaiwa Juni 27 mwaka huu, jijini Dar es Salaam, mshitakiwa akiwa mjumbe wa MAT aliwashawishi wajumbe wa chama hicho kufanya mgomo kinyume cha amri iliyotolewa na Mahakama Kuu, Kitengo cha Kazi, Juni 22 mwaka huu.

Mshitakiwa huyo anatetewa na jopo la mawakili wanne, likiongozwa na Isaya Matamba, Dkt. Maulid Kikondo, Dkt. Gaston Kennedy na Dkt. Rugemeleza Nshala.

Dkt. Mkopi yupo nje kwa dhamana baada ya kukamilisha masharti ya kuwa na wadhamini wawili waliosaini hati ya dhamana sh. 500,000.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate