EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, December 19, 2012

Wafungwa Wawili Waachiwa Huru Na MICT.

Taasisi ya Kimataifa inayorithi Kazi za Mahakama za Umoja wa Mataifa (MICT) imewaachia huru kabla ya muda wao wa adhabu kuisha, watu wawili waliokuwa wanatumikia kifungo baada ya kutiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994.

Watu hao ni pamoja na meya wa zamani wa wilaya ya Gikongoro, mkoa wa Kigali Vijijini, Paul Bisengimana na kiongozi wa zamani wa wanamgambo wa Interahamwe mkoani Gisenyi, Omar Sereshago. Wawili hao walikuwa wanatumikia adhabu zao nchini Mali.
Wakati anaachiwa,Bisengimana alikuwa ameshatumikia theluthi mbili ya kifungo cha miaka 15 alichopewa.Alikuwa kizuizini tangu Desemba 4, 2001.
 Meya huyo alitiwa hatiani Aprili 13, 2006 kwa kusaidia na kuunga mkono kutendeka kwa uhalifu wa kuua na kuteketeza kizazi kama uhalifu dhidi ya binadamu baada ya yeye mwenyewe kukiri makosa hayo.
 Serushago kwa upande wake ameachiwa akiwa ameshatumikia robo tatu ya kifungo cha miaka 15 jela alichopewa Februari 5, 1999 baada ya kutiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari na uhalifu dhidi ya binadamu. Kiongozi huyo wa wanamgambo alikuwa kizuizini tangu Juni 9, 1998. Yeye pia kama alivyo mfungwa mwenzake alikiri kwa hiari yake mashitaka hayo dhidi yake.
 Katika uamuzi uliomhusu Bisengimana, Rais wa MICT, Jaji Theodor Meron alisema, ‘’Baada ya kuchambua kwa makini vipengele vilivyomo katika sheria na pia mazingira maalum ya kesi ya Bisengimana, nimeonelea kwamba anastahili kuachiwa huru mapema na mara moja.’’ Alimwelekeza Msajili kuifahamisha serikali ya Mali juu ya uamuzi huo.
 Uamuzi wa MICT ambayo ilianzishwa rasmi 2010 kurithi kazi za mahakama mbili za Umoja wa Mataifa ikiwa ni pamoja na Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu katika Yogoslavia ya zamani (ICTY) imeonekana kutatua mgogoro wa kisheria wa muda mrefu kati ya mahakama hizo mbili juu ya suala hilo.
 Katika ICTR, mfungwa anatakiwa kutumikia robo tatu ya adhabu aliyopewa kabla ya kufikikiriwa kuachiwa huru mapema wakati ICTY, uamuzi kama huo unaweza kutolewa iwapo mfungwa atakuwa ameshatumikia theluthi mbili ya adhabu yake.
 Lakini katika uamuzi wake, Rais Meron alisema ‘’Nimeonelea kwamba wafungwa wote wanaosimamiwa na MICT wanastahili kutendewa sawa.’

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate