UAMUZI wa Pep Guardiola kujiunga na Bayern Munich umekuja kama jambo la kushtua, amesema Alex Ferguson.
Guardiola
alikuwa akihusishwa na vilabu vikubwa duniani vikiwemo Manchester City
na Chelsea alipokuwa anajiandaa kurudi kwenye soka baada ya mapumziko ya
mwaka mmoja.
Lakini
kocha huyo wa zamani wa Barcelona, akawaduwaza watu pale alipoichagua
Bayern Munich atakayoanza kuitumikia mwishoni mwa msimu.
Bosi wa United, Alex Ferguson amesema: “Nimeshangazwa sana kwasababu sikuliona hilo linavyokuja.
“Muda wote gumzo lilikuwa ni kuhusu England”
Hata hivyo Fergie ameona ni kwanini Guardiola ameamua kusaini mkataba wa miaka mitatu Bayern Munich.
Aliongeza:
“Ukiwa kama kocha utagundua kuwa Bayern Munich ni timu ambayo kamwe
huwezi kutema ofa yao kwasababu ni moja kati ya timu bora zinazokimbiza
Ulaya.
“Wana jiji la kuvutia, uwanja wa kuvutia, wachezaji wazuri na historia nzuri.
“Kuna
mtu kama Karl-Heinz Rummenigge, Uli Hoeness, Gerd Muller na Sepp Maier.
Sina uhakika mtu kama Franz Beckenbauer ana nafasi gani kwa sasa.
“Wakiwa na hazina ya watu kama hao, inakuwa ni rahisi kuichagua Bayern Munich”
No comments:
Post a Comment