EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, February 13, 2013

VALENTINE’S DAY HIYOOO! VIPI KUHUSU UHURU WA SIMU YAKO?


ZIMEBAKI siku kadhaa kabla ya kuadhimisha Siku ya Wapendanao Duniani (Valentine’s Day). Siku hii maalum ya ‘ku-show love’ huadhimishwa kila ifikapo Februari 14 ya kila mwaka ikiwa ni mahsusi kabisa kuonesha namna unavyompenda mpenzi wako au watu wengine muhimu maishani mwako.
 
Tunapojiandaa kuelekea siku hiyo, si vibaya tukakumbushana mambo ya msingi ambayo yatakufanya wewe na umpendaye muiadhimishe kwa uhuru. Katika siku za hivi karibuni, marafiki wengi wamekuwa wakinitumia ujumbe mfupi wa maneno na kunilalamikia jinsi wapenzi wao wanavyowanyanyasa kupitia simu zao.
Dada Irene wa Sinza, Dar aliniandikia kuwa mpenzi wake amekuwa na kawaida ya kuweka password kwenye simu yake kiasi kwamba hata akitaka kuigusa simu ya mpenzi wake, hawezi kufanya hivyo kwani hukataa kabisa kumtajia namba ya siri.
Akazidi kufunguka kuwa kibaya zaidi, mpenzi wake anapopigiwa simu wakiwa pamoja, hutoka na kwenda kuzungumza bafuni au nje kabisa huku akitumia sauti ya kunong’ona. Akaomba ushauri juu ya tafsiri ya tabia hiyo ya mpenzi wake.
Kaka Bariki kutoka Sumbawanga yeye alinitumia ujumbe na kunieleza kuwa mpenzi wake huwa anafuta meseji kwenye simu yake kila zinapoingia au anapotuma, wakati mwingine hubakiza zile alizomtumia yeye tu. Kama hiyo haitoshi, pia hufuta hata rekodi za simu zilizoingia au kutoka kwenye simu ya mpenzi wake.

Marafiki, hao ni baadhi tu ya wengi walionitumia ujumbe lakini wanawakilisha jamii yetu tunayoishi. Ni ukweli usiopingika kuwa matumizi ya simu yamerahisisha sana usaliti kwa wapenzi wasiojitambua. Simu zimefanya iwe rahisi mtu kutoka nje ya uhusiano wake na kulisaliti penzi lake.
 
Watoto wa mjini siku hizi wanakwambia ukishapata namba ya simu ya mwanaume au mwanamke ‘unayemtaka’, basi kila kitu kimeisha. Mipango yote hufanyika kwa SMS au wakati mwingine kupigiana, appointment hupangwa na mwisho wawili hukutana na kuvunja amri ya sita.
 
Walioachana kwa sababu ya simu ni wengi lakini pia wale ambao wanatifuana kila kukicha, kila mmoja akimfikiria mwenzake tofauti kuhusiana na matumizi mabaya ya simu idadi ni kubwa kuliko maelezo.
 
Leo nataka kuzungumzia kitu ambacho naweza kutofautiana na wengi lakini ndiyo ukweli hasa katika kipindi hiki, lengo ni kuleta amani na kuwafanya wapenzi na wanandoa kudumu kwa muda mrefu bila migogoro. Ninachotaka kusema ni kwamba mnapokuwa katika uhusiano kisha mkafikia hatua ya kufikiriana ndivyo sivyo kwa sababu tu ya simu zenu za mkononi ni hatari sana.
 
Kwa nini mpenzi wako afikie hatua ya kufikiria kwamba unamsaliti? Inawezekana ni kwa sababu ya namna unavyompa uhuru wa kuishika simu yako na kufanya anachokitaka. Kwa nini uweke password ambayo mpenzi wako haijui? Kwa nini ukazungumze na simu nje? Kuna kipi ambacho hutaki mpenzi wako akifahamu? Hizo ni tabia zilizopitwa na wakati.
 
Wapo wapenzi wachache ambao ni mfano mzuri wa kuigwa, yaani unakuta mtu anamuachia mpenzi wake simu hata kutwa nzima na anakuwa huru kabisa! Anafanya hivi kwa sababu anajiamini kuwa hana nyendo chafu na hamsaliti mpenzi wake. Itapendeza kila mmoja akiwa muaminifu kwa mpenzi wake hasa katika zama hizi zilizojaa maradhi sugu ikiwemo Ukimwi.
Ukimpa mpenzi wako uhuru kwenye simu yako, bila shaka hamtakwaruzana na mtasherehekea Valentine’s Day kwa mahaba ya dhati.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate