Hali hiyo ilisababisha mechi hiyo ichelewe kuanza kwa muda wa dakika tano ili kuwasubiri wachezaji ambao walikuwa wameingia mitaani kwa ajili ya kutafuta viatu.
Akizungumza jana, kocha mkuu wa timu hiyo, John Tegete alisema kuwa wachezaji hao walifikia uamuzi huo baada ya kuhofia kushindwa kucheza vizuri katika mechi hiyo, kutokana na viatu vyao wanavyomiliki kutokuwa na uwezo wa kuhimili matope yaliyotokana na mvua kubwa iliyonyesha jijini humo kabla ya kuanza kwa mchezo huo.Alisema hali hiyo yote inachangiwa pia na ukata mkubwa unaoikabili timu hiyo pekee kutoka katika jiji hilo la Mwanza lenye utajiri mkubwa na watu wengi wenye uwezo wa kuisaidia timu hiyo.
“Hakika sikufurahia kabisa hali hiyo, lakini nilishindwa, nifanyeje kwa sababu tunahitaji ushindi ili tuweze kujiweka katika mazingira mazuri ya kuepukana na balaa la kushuka daraja,” alisema Tegete.
Alisema, “Ilibidi niwaruhusu wakaingia mitaani kutafuta viatu, hata hivyo nawashukuru sana vijana wangu waliweza kupambana hadi dakika ya mwisho na bila ya kufungwa na timu ambayo wachezaji wake wanahudumiwa kila kitu na wamekuja Mwanza kwa usafiri wa ndege.”
Katika hatua nyingine, Tegete aliongeza kuwa pamoja na matatizo yote yanayoikabili timu hiyo, hana mpango wowote wa kuachana nayo ispokuwa ataendelea kuiongoza hadi dakika ya mwisho.
Tegete amewataka watu wote wenye mapenzi mema na timu hiyo kujitokeza na kuisaidia ili iweze kukabiliana na changamoto hizo ili kuhakikisha wanapigana na kuendelea kubakia katika Ligi Kuu.
Katika miaka ya hivi karibuni Toto Africans imekuwa ikakabiliwa na ukata mkubwa hali ambayo mara kwa mara imeifanya timu hiyo kuwa na wakati mgumu na kushindwa kutatua matatizo yanayoikabili.
Hivi sasa timu hiyo inashika nafasi ya 12 katika msimo wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 13 baada ya kucheza mechi 16, ambapo imeshinda mechi mbili imetoka sare mechi saba na imepoteza mechi saba.
No comments:
Post a Comment