EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, February 12, 2013

Waislamu, Wakristo wamwaga damu na kusababisha kifo cha Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste Assemblies of God, Mathayo Kachila

VURUGU kubwa za kidini kati ya Waislamu na Wakristo, zimezuka katika kijiji cha Buseresere, wilaya ya Chato, mkoani Geita, na kusababisha kifo cha Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste Assemblies of God, Mathayo Kachila (45), huku watu wengine 10 wakijeruhiwa vibaya kwa mapanga.

Mchungaji huyo alichinjwa na watu wanaodaiwa ni kuwa waumini wa Kiislamu kisha mwili wake kutelekezwa kwenye vibanda vya maduka ambavyo viko jirani na eneo hilo jana.
Taarifa kutoka eneo la tukio hilo zilisema kuwa tukio hilo lilitokea asubuhi ambapo chanzo chake kinatajwa kuwa ni watu wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Kiislamu kuvamia bucha iliyokuwa ikiwauzia nyama Wakristo wa kijiji hicho waliokuwa wamepanga foleni kwa wingi kusubiri huduma hiyo.
Wakiristo hao walikuwa wamechinja ng’ombe mmoja na mbuzi wawili eneo la kanisani kabla ya kuipeleka nyama hiyo katika bucha hiyo iliyoko eneo la Buseresere Sokoni na ndipo walipokumbana na kadhia.

Mashuhuda walisema kuwa tukio hilo lilianza saa 2:00 asubuhi muda mfupi baada ya nyama kuwasili katika bucha hiyo ya Wakristo kwa ajili ya kuuzwa, jambo linalodaiwa kuwakera Waislamu ambao waliivamia bucha hiyo kwa lengo la kuifunga.
Taarifa ziliongeza kuwa wakati Wakristo wakitafakari uwepo wa Waislamu kwenye bucha yao, ghafla walishtukia wenzao hao waliokuwa wametapakaa kwa wingi wakiimwagia nyama hiyo vitu vinavyodaiwa kuwa sumu.
Kutokana na hali hiyo, Wakiristo walioonekana kukerwa na kitendo hicho na ndipo mapambano yalipoanza kati ya pande hizo mbili huku Wakristo wakitumia mawe na 


Waislamu wakitumia mapanga na majambia.
Ilidaiwa kuwa wakati mapambano hayo yakiendelea, mchungaji huyo ambaye kwa sasa ni marehemu alifika eneo la tukio ili kujua kulikoni na ndipo alipojikuta akishambuliwa kwa mapanga sehemu mbalimbali za kichwani na kupoteza maisha akikimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Geita kwa matibabu.

“Yaani ilikuwa kama mzaha tu...baada ya Wakristo kuleta ng’ombe mmoja na mbuzi wawili kwenye bucha yao, tulishangaa kuona Waislamu wamevamia hiyo bucha wakati tayari nyama ikiwa inauzwa na Wakristo wakiwa wamepanga foleni wakisubiri kuhudumiwa,” alisema shuhuda mmoja.
Aliongeza kuwa Waislamu walipofika walitaka kuifunga ile bucha lakini Wakristo waligoma na ndipo wengine walifika na kuimwagia ile nyama vitu kama sumu na huo ukawa mwanzo wa machafuko.

“Kwa vile wenzetu walifika eneo hilo wakiwa na silaha tayari walianza kuwakata Wakristo na kuivunjavunja ile bucha huku Wakristo wakijihami kwa kutumia mawe lakini walizidiwa nguvu,” alisema shuhuda mwingine.
Waliojeruhiwa ni Saidi Ntahompagaze (45), Sadick Yahaya (40),Yasin Rajab (56),Vicent Damon (22), wote wakazi wa Buseresere na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Ramadhan ambaye yuko mahututi katika wodi namba nane katika hospitali ya wilaya ya Geita.

Hata hivyo watu wengine watano ambao majina yao hayakuweza kupatikana mara moja walitibiwa na kuruhusiwa kutokana na hali zao kuwa nzuri.
Polisi kutoka wilaya za Chato na Geita walifika eneo la tukio hilo saa 4:30 na kukuta uharibifu mkubwa umekwishafanyika ikiwa ni pamoja na duka la Mwenyekiti wa BAKWATA Wilaya ya Chato, Yusuph Idd, linalotumika kwa biashara ya M-Pesa na vinywaji baridi likiwa linateketea kwa moto.

Mkuu wa Wilaya ya Chato, Ludorick Mpogolo, aliyefika eneo la tukio muda mfupi baada ya polisi kuwasili, mbali na kusikitishwa na kitendo hicho aliwataka wananchi kuwa watulivu wakati serikali ikiangalia njia sahihi za kutatua mgogoro huo ambao unakua kwa kasi kila kukicha.
Hivi karibuni mgogoro huo wa kidini umezidi kukua wilayani humo kwa pande hizo mbili kila upande ukidai ndiyo wenye haki ya kuchinja nyama inayouzwa buchani.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate