EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, March 13, 2013

Makundi yaibuka mchakato wa Papa

Vatican City. 
Dirisha limefunguliwa tayari kwa hewa safi kuingia Vatican City. Hivi ndivyo unavyoweza kuuelezea mchakato wa kumpata Papa wa 226 wa Kanisa Katoliki, unaoanza leo.
 
Mchakato huo unaanza rasmi saa 10.45 jioni kwa saa za Vatican (Saa 12.45 kwa saa za Afrika Mashariki) na utatanguliwa na ibada maalumu ya misa ya makadinali 115 wanaoshiriki katika uchaguzi huo.

Tayari, vumbi limeanza kutimka huku makundi makubwa matatu yakiibuka katika uchaguzi huo, unaofuatiliwa kwa karibu kote duniani na ambao unaweza kudumu hadi wiki mbili.
Makundi hayo ni pamoja na lile la makadinali wa Italia, wapatao 28 dhidi ya Wamarekani 11, wote wakiwa na malengo tofauti katika nia yao ya kuchukua wadhifa huo wa juu katika Kanisa Katoliki.

Hata hivyo, Italia ina mgawanyiko mkubwa wa vikundi vya kiitikadi miongoni mwa waumini wake, kama ilivyo kwa makadinali hao, jambo ambalo linapunguza umoja wao.

Wataliano kwa upande mwingine, wangependa kumaliza miaka 35 ya utawala wa wageni katika Vatican tangu alipoingia Papa Yohane Paul II mwaka 1978 (sasa mwenyeheri) na mfuasi wake, Benedict XVI na hivyo kurejesha miaka zaidi ya 450 ya utawala wao katika kiti hicho cha Mtakatifu Petro, wakipenda pia kudumisha mazoea ya utawala wa kirasimu katika uongozi huo.


Tofauti na miaka ya nyuma, wachambuzi wa masuala ya dini na imani, wanaona kuwa uchaguzi wa mwaka huu ni mwepesi zaidi kwani hakuna kadinali mwenye nyota zaidi ya wengine miongoni mwa washiriki hao 115, ambao angepewa nafasi kubwa kuibuka mshindi.
Hata hivyo, Wamarekani, taifa kubwa na tajiri duniani wanaowakilishwa na makadinali 11, imani yao ni kutaka kuupeleka nchini mwao, uongozi wa Vatican. Dhamira yao, pia inapingwa.

Hao wanadhani kuwa Marekani haiwezi kutoa kiongozi mkuu wa kanisa hilo, ambaye ataweza kukabiliana na wapinzani wa Ukristo na kuaminika kwa ulimwengu wa Kiislamu.
Kundi lingine na ambalo linaweza kubadili matokeo, ni la wateule 67 wa Papa Benedict ambao ni zaidi ya nusu ya wapigakura wote.
Wao wanaelezwa kuwa mchango wao katika uchaguzi huo utakuwa mkubwa na hata kuathiri matokeo, kama watapenda kuendeleza misingi ya uongozi wake.
Pamoja na makundi hayo, kuna baadhi ya makadinali ambao kura ya maoni, imeendelea kuwabeba zaidi kabla ya uchaguzi wenyewe kuanzia leo.
 Watu wa kundi hilo wanaongozwa na raia wa Brazil, Odilo Scherer, ambaye anasemekana kuwa karibu na mfumo wa kanisa hilo, Curia, anapigiwa upatu na Wataliano.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate