EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, July 18, 2013

JIONEE MAAJABU MAZISHI YA BABA'KE JOYCE KIRIA.

MAAJABU yameibuka kwenye mazishi ya baba mzazi wa Mtangazaji wa Kipindi cha Wanawake Live kinachorushwa hewani na  Televisheni ya  East Africa, Joyce Kiria, Michael Francis Iwambo Kiria kufuatia kuchimbwa kwa makaburi mawili, Amani lina mkasa mzima.
Kondoo akichinjwa.
Tukio hilo la ajabu lilitokea kwenye msiba wa mzee huyo, Kata ya Kibosho, Kijiji cha Dakau, mkoani Kilimanjaro wakati wa maandalizi ya kuuhifadhi mwili wa merehemu huyo.
 

Mzee Kiria alifariki dunia Julai 10, mwaka huu jijini Tanga alikokuwa akiishi na mke mwingine (si mama’ke Joyce) baada ya kuugua ghafla.

KWA NINI MAKABURI MAWILI?
Ilielezwa kwamba ndugu wa mzee Kiria waliopo kijijini Dakau walipopata taarifa za kifo cha mzee huyo na kwamba mwili wake utazikwa kijijini hapo walichimba kaburi kwenye eneo la makaburi ya ukoo.


“Maiti ilifika kijijini, taratibu za ibada zilifanyika kanisani, lakini kazi ikawa kwenye kuupeleka mwili kaburini. Mke wa marehemu aliyekuwa akiishi naye Tanga aliuliza eneo lililochimbwa kaburi na kuambiwa ni la ukoo, akasema haiwezekani azikwe hapo.
 

“Mwanamke huyo alisema marahemu wakati wa uhai wake aliagiza akifa azikwe kwenye shamba alilopewa na baba yake mzazi, mzee Francis Kiria na si vinginevyo,” alisema mpashaji wetu aliyekuwa eneo la tukio.

MSIBANI HAPAKALIKI
Vuta nikuvute ilitokea eneo la msiba,  mke wa marehemu aliweka wazi msimamo wake kwamba endapo ndugu watalazimisha marehemu azikwe eneo la familia angeondoka na maiti kurudi nayo Tanga kwa mazishi.


JOYCE KIRIA AMWAGA MACHOZI, APIGA MAGOTI
Ilibidi ndugu waweke kikao cha dharura cha familia ili kumshawishi mwanamke huyo akubaliane na matakwa ya familia kwa sababu ndugu wote walizikwa makaburi ya ukoo, lakini mjane huyo alitia ngumu.
 

“Yule mke wa marehemu alikataa katakata, alisema lazima mume wake azikwe kwenye shamba alilopewa na baba yake kama alivyotaka akiwa hai.
“Ilifika mahali, Joyce Kiria alimpigia magoti mwanamke huyo huku akilia na kumuomba aruhusu baba yake azikwe kwenye kaburi lililokwisha chimbwa kwenye eneo la ukoo, lakini wapi, mwanamke aligoma,” alizidi kusema mpashaji wetu.


KABURI LA PILI LACHIMBWA
Kwa mujibu wa mtoa habari wetu, baada ya msimamo wa mwanamke huyo kusimama kwenye maamuzi, ilibidi ndugu wakubaliane naye kwa kutuma watu kwenda kuchimba kaburi la pili kwenye shamba la marehemu.
 

Cha ajabu, wakati wachimbaji wakiendelea na zoezi hilo, kondoo mmoja mweupe alianza kulia kwa muda mrefu jambo lililowashangaza watu walioshuhudia.
 

Wengi wa watu hao walihoji kilio cha kondoo huyo wakisema huenda aliashiria mambo fulani ambayo wazee wa kimila ndiyo wanatakiwa kufuatilia na kutoa ufafanuzi.
 

Mbali na kilio cha kondoo huyo, baadhi ya watu walisikika wakisema wanaamini  baada ya mazishi hayo, kifo kingine kitajiri kwa sababu haijawahi kutokea kijijini hapo makaburi yakachimbwa mawili kwa ajili ya marehemu mmoja.
 
WAZEE WA KIMILA WAKAA KIKAO
Kufuatia kuwepo kwa makaburi mawili, habari zinasema ilibidi wazee wa kimila kuketi kikao cha ghafla na kuulizana mila na desturi za mababu ni nini inapotokea hali kama hiyo.
Ndipo mzee mmoja alisema lazima kondoo mmoja mweupe achinjwe kisha damu yake kumiminiwa ndani ya kaburi lisilotakiwa halafu mzoga wa kondoo huyo ufukiwe katika kaburi.
Kondoo aliyepata ‘kura nyingi’ ni yuleyule aliyelia baada ya mjane wa marehemu kushinda eneo la kuzikiwa mume wake.


KONDOO AKAMATWA, ASOGEZWA KABURINI, ACHINJWA
Kondoo huo alikamatwa, akasogezwa jirani na kaburi, akachinjwa mpaka kukata roho. Damu yake ilimiminikia kaburini, nyingine ilikingwa kwenye kikombe na kumiminiwa kaburini halafu mzoga wake ukatupwa humo na kufukiwa.


BABA WA JOYCE AZIKWA SASA
Baada ya kufanyika kwa mambo hayo yote, mwili wa marehemu ukiwa ndani ya jeneza la mbao lenye rangi ya damu ya mzee ulipelekwa kuzikwa kwenye kaburi lililochimbwa shambani kwake.
 

Mazishi yalifanyika kwa amani, baadaye waombolezaji walitawanyika kurudi eneo la msiba lakini gumzo kuu likiwa kuchinjwa na kuzikwa kwa kondoo huyo.
Baadhi ya watu kijijini hapo wenye rika la utu uzima, walisikika wakisema hawajahi kuona mnyama akitolewa kafara ya kifo cha binadamu.
Wengi walisema wanachokijua wao ni kwamba, utata wa kaburi humalizwa kwa kuzikwa mgomba au majani yaitwayo isale.


JOYCE KIRIA ANENA 
Baada ya kupata habari hiyo ya kusisimua, juzi Amani lilimtafuta Joyce Kiria ili kuthibitisha kutokea kwa habari hiyo na kumpata nyumbani kwake, Changanyikeni, jijini Dar ambapo alikiri na kusema hata yeye mwenyewe haelewi kitu ambacho kimetokea kwa sababu hajawahi kuona katika maisha yake.
 

“Kwa kweli hayo ni majaabu kwangu, hata mimi nimeshangaa kupita kiasi, sijawahi kuliona jambo hili katika maisha yangu na limeniumiza kupita kiasi,” alisema Joyce huku machozi yakimlengalenga.
Mungu ailaze pema peponi roho ya marehemu Michael Kiria. Amina.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate