EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, July 18, 2013

Mtwara kwawaka moto tena •Viongozi wa ushirika wafungiwa ghalani.

MZIMU wa vurugu na hasira za wakulima wa zao la korosho mkoani Mtwara umeibuka tena jana baada ya wananchi wenye hasira kuwavamia na kuwashikilia viongozi wa vyama vya ushirika Wilaya ya Mtwara Vijijini.

Wakulima hao wakiwa na hasira huku wakiapa kukabiliana na nguvu yoyote ya serikali, wamewakamata na kuwafungia viongozi wawili wa Chama cha Ushirika wa Nanyamba katika ghala la korosho kwa zaidi ya saa nane, kabla ya kuokolewa na polisi.

Habari za kuaminika na zilizothibitishwa na uongozi wa polisi wa wilaya, zimesema kuwa wakulima hao wenye hasira walimzuia mwenyekiti wa ushirika huo aliyefahamika kwa jina moja la Nantolela na katibu wake, Lipaike ikiwa ni njia ya kuishinikiza serikali iwalipe malipo yao ya pili ya korosho.

Wakiongea kwa hasira na bila utaratibu, wakulima hao wamesema wamechoshwa na ufisadi wa viongozi wa vyama vya ushirika wanaojinufaisha na pesa za wakulima ambao wanafumbiwa macho na serikali kwa muda mrefu.

“Hatuwaachi hadi kieleweke, tulipwe pesa zetu, utani wa aina hii unaofanywa na serikali kushindwa kufuatilia viongozi hawa wanaojinufaisha na jasho letu umetosha, tunataka haki yetu, tunasomesha, tuna mahitaji yetu.

“Hii ni kejeli kubwa, tuliwakopesha korosho tukalipwa malipo ya awali shilingi 600, wengine sasa wanadai 600 zingine, wengine wanadai 400, wengine wanadai 200 kutegemeana na walivyolipwa, korosho za wakulima wamekopa na wameshauza maghala hayana korosho, na pesa hazionekani,” alisema mmoja wa wakulima hao.

Fujo hizo zilizotokana na hatua ya serikali wilayani humo kutaka kuwalipa wakulima hao sh 15, tu za malipo ya pili kwa kilo ya korosho, badala ya kulipwa kati ya sh 200 na 600 kama ilivyokubaliwa katika kikao cha Juni 27, mwaka huu.

“Kikao kilichofanyika tarehe 27 Juni tulikubaliana kulipwa, tumeambiwa viongozi wetu walienda benki wamekopeshwa pesa na sasa wametuita kutaka kutulipa shilingi 15, tu kwa kilo badala ya 600 au 300 au 200 kadiri tunavyodai,” alisema mkulima mmoja huku akishangiliwa na wenzake.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu kuhusu suala hilo, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Wilman Ndile alisema: “Niko njiani, naelekea Mtwara sina majibu kwa sasa ingawa tayari tulitoa amri kwa viongozi wa vyama vya ushirika kuwalipa wakulima pesa zilizosalia, sasa hilo la Nanyamba sijalisikia vema, nadhani labda bado kuna viongozi wanasumbua wakulima, nitajitahidi nikifika Mtwara nikupe majibu kuhusu suala hilo hapo kesho.”

Mkuu wa Kituo cha Polisi Nanyamba alikiri kufungiwa kwa viongozi hao tangu saa 3 asubuhi hadi saa mbili usiku alipofika huko kuwaokoa na kuamrisha kuwa wakae na diwani ili kuhakikisha wakulima hao wanalipwa.

“Ni kweli walifungiwa na wakulima, nilifika pale kuwaokoa wasidhuriwe ila sasa kuhusu malipo sikufuatilia maana hiyo sio kazi yangu,” alisema.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Linus Sinzumwa alisema hana taarifa kwa kuwa yupo mkoani Mbeya kwa matatizo ya kifamilia.

Hali hiyo inajitokeza ikiwa ni miezi michache tu tangu kundi la wakulima wa Korosho wilayani Liwale mkoani Lindi, walipojaribu kuzuia gari lililokuwa na fedha za malipo ya korosho wakipinga kiasi kidogo cha malipo yao ya pili na kuanza kufanya vurugu na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali.

Kutokana na vurugu hizo zilizotokea Aprili 23 mwaka huu majira ya saa tisa alasiri, nyumba zaidi ya 10 zilichomwa moto zikiwemo za wabunge na viongozi mbalimbali na mali kadhaa kuharibiwa.
                                                        CREDIT: TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate