EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, October 11, 2013

MASOGANGE AJA NA SIRI NZITO.

VIDEO Queen wa Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ alitarajiwa kutua nchini  Jumatano ya wiki hii akitokea Afrika Kusini huku siri nzito ya mzigo aliodakwa nao ikitawala, Amani linakujuza.
Agnes Gerald ‘Masogange’.
Masogange anakuja Bongo baada ya kumaliza kulipa deni lote la randi 30,000 (shilingi milioni 4.8) alizoamriwa kulipa na Mahakama Kuu ya Gauteng iliyopo Kempton Park jijini Johannesburg nchini humo baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kuingiza kemikali haramu, Julai 5, mwaka huu.
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika, Masogange anarejea na Melisa Edward ambaye alikamatwa naye lakini mahakama ikamwona hana hatia.

SIRI NZITO
Ujio wa Masogange bado una siri nzito kwani licha ya mahakama hiyo kumtia hatiani kwa faini au kifungo cha miezi thelathini jela, lakini bado serikali ya Tanzania inahaha kutaka kujua mzigo aliodakwa nao alitumwa na nani!
“Masogange ameahidi kutowataja watu waliompa mzigo akidai kuwa itaendelea kuwa siri yake mpaka anakufa,” kilipasha chanzo chetu.
 
WATOTO WA VIGOGO
Watoto wa vigogo ndiyo wamekuwa wakitajwa zaidi kuhusika na kumtuma Masogange ingawa hakuna jina la moja kwa moja la mtoto yeyote wa kigogo lililowahi kutajwa.
ANAYEMJUA MWAKYEMBE
Mpaka sasa, Serikali ya Tanzania kupitia kwa Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison George Mwakyembe iliwahi kumtaja kijana aitwaye Mangunga ambaye ndiye anadaiwa kuwa na Masogange ndani ya ndege kwenda Afrika Kusini.

Binti Kiziwi.
Mwakyembe aliamuru kijana huyo asakwe na kukamatwa ili kujibu mashitaka ya kusafirisha madawa ya kulevya aina ya Methamphetamine kwa Tanzania huku Afrika Kusini ikisema unga huo ni ephedrine ambao si wa kulevywa bali ni kemikali haramu.
KAMATI YA MAPOKEZI YAMWANDALIA PATI YA MAMILIONI
Habari za kifukunyuku zinadai kuwa, jijini Dar baadhi ya mastaa wameunda kamati ya mapokezi ya Masogange, Jacqueline Wolper Massawe akiwa mwenyekiti wake, katibu na wajumbe hawakupatikana majina.
KAZI YA KAMATI
Kazi ya kamati hiyo inadaiwa ni kukusanya mamilioni kutoka kwa mapedeshee wa mjini ili kuwezesha kufanyika kwa pati ya nguvu ya kumshukuru Mungu kwa kumsaidia staa huyo kutoka jela na kurudi Bongo.
“Kamati iko chini ya uenyekiti wa Wolper, si unajua huyu dada hata hivi karibuni alimfanyia birthday Masogange japo mwenyewe hakuwepo?
“Sherehe itaandialiwa kwenye ukumbi mmoja uliopo ufukweni mwa Bahari ya Hindi lakini kwa sasa sitautaja ili kuepuka wazamiaji,” kilisema chanzo chetu.
Saada.
NZOWA: HIYO PATI ITAFANYIKIA WAPI, SINZA KWA DADA’KE AU?
Kufuatia kuwepo kwa madai kwamba, Masogange akitua tu Bongo atadakwa na Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, juzi Amani lilimsaka kamanda wa kikosi hicho, Godfrey Nzowa na kumuuliza kuhusu madai hayo.
Amani: Afande, naomba unisaidie mawili matatu. Yule msanii Masogange aliyekamatwa na madawa ya kulevya na kuhukumiwa Afrika Kusini anarejea nchini kesho Jumatano (jana) Je, ninyi mna mpango wowote wa kumkamata akitua?
Nzowa: Sisi hatuna shida naye tena. Alishahukumiwa kule, sasa tumkamate huku kwa sheria gani?
Amani: Basi kuna habari kwamba mmepanga kumkamata maana tumeambiwa na chanzo chetu kuwa atafanyiwa pati ya kumshukuru Mungu kwa kumtoa katika mazito.
Nzowa: Hiyo pati ataifanyia wapi, Sinza kwa dada’ke au?
Amani: Bado hawajaweka wazi.
Nzowa: Sisi hatuna shida naye.
WOLPER ASAKWA KUULIZWA
Juzi asubuhi, Amani lilimtafuta Wolper kwa njia ya simu yake ya mkononi na kumuuliza ukweli wa kuwepo kwa kamati ya sherehe ya mapokezi ya Masogange ambapo  alijibu:
“Nipo shooting (narekodi) Arusha, nitawatafuta baadaye kuhusu hilo suala kama lipo au halipo.”
MASOGANGE NAYE
Juzi Jumanne, Amani lilimpigia simu Masogange akiwa Afrika Kusini na kumuuliza kuhusu ujio wake wa jana.
Masogange: Ni kweli narudi huko (Bongo) Jumatano, mipango yote ya safari tayari, namshukuru Mungu kwa yote.
WENGINE WANASOTA!
Wakati Masogange akiwa ameponea tundu la sindano, mrembo mwingine wa Bongo Fleva, Sandra Khan ‘Binti Kiziwi’ anateseka gerezani huko China alipofungwa kwa miaka mitatu kwa msala wa madawa ya kulevywa wakati Saada Kilongo yuko mahabusu Bongo kwa kesi ya aina hiyohiyo.
Chanzo ni GLP.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate