EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, November 26, 2013

DK KAWAMBWA AJIBU MAKOMBORA YA NAPE

Bagamoyo. 
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa amejibu madai yaliyotolewa hivi karibuni na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye kwamba ni mmoja wa mawaziri walioshindwa kazi, hivyo kustahili kung’olewa.
 
Katika madai yake, Nape alisema Dk Kawambwa ameshindwa kusimamia vyema madai ya walimu na kwamba akiwa Waziri wa Miundombinu, aliingia mkataba na Kampuni ya ujenzi ya Progressive iliyopewa zabuni ya kujenga Barabara ya Namtumbo hadi Tunduru wakati mkandarasi huyo hana uwezo wa kuijenga.

Nape alikaririwa akisema kwamba umefika wakati kwa waziri huyo na wenzake wa Fedha, Dk William Mgimwa; Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza; na Naibu wake, Adam Malima kuhojiwa na Kamati Kuu (CC) ya chama hicho.
Akijibu madai hayo Mjini Bagamoyo jana, Dk Kawambwa alisema anasubiri kwa hamu kuitwa CC kueleza tuhuma zinazomkabili huku akijigamba kuwa yeye ni mti wenye matunda ndiyo maana unapigwa mawe.

Alisema hayo alipokuwa akikabidhi vifaa vya michezo kwa timu 16 zitakazoshiriki michuano ya Kombe la Kawambwa inayofanyika katika Jimbo la Bagamoyo ambalo yeye ni mbunge wake.

“Kuna maneno yanayoendelea hivi sasa eti na mimi mbunge wenu natajwa kuwa fisadi kwa mkataba wa ukandarasi wa barabara, siyo kweli. Wakati mkataba ule unasainiwa mimi nilishatoka kwenye Wizara ya Miundombinu, sihusiki kabisa na mkataba ule,” alisema na kuongeza:

“Mwaka 2010 mimi ndiye niliyeshawishi Ubalozi wa Japan ukatoa fedha kwa ajili ya mradi ule wa Barabara ya Namtumbo - Tunduru lakini mkataba ukasainiwa Desemba 24, 2012 kati ya Wizara na Kampuni ya Progressive.

“Walipovurunda Wizara ikawatimua, mimi sikuhusika hata kidogo kwani wakati wanasaini mkataba ule mimi nilishahamishiwa wizara nyingine.”

“Mimi nipo baridi, nasubiri kwa hamu kubwa kuitwa kwenye Kamati Kuu, mimi si mtu wa kupiga kelele na tuhuma zote dhidi yangu ninaamini si za kweli... wakati mwingine maadui wanatafuta njia za kunichonganisha na chama changu.”

“Wanasema kila wizara ninayopelekwa ninavurunda, nasema, mimi ni mti wenye matunda. Mti wowote ambao unazaa vizuri lazima utapigwa mawe, nasubiri siku hiyo ya kuitwa CC ambako pumba na mchele vitajulikana.”

Akizungumzia ujenzi wa barabara hiyo, Waziri Kawambwa alisema anamshukuru  Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli aliyemfukuza mkandarasi huyo Progressive kwa kushindwa kazi. Hata hivyo, katika madai yake, Nape alisema kumfukuza mkandarasi huyo pekee hakutoshi, bali aliyehusika kumpa mkataba naye anapaswa kuchukuliwa hatua kwani uchunguzi unaonyesha kuwa alishashindwa kazi wakati anapewa mkataba.

Hata hivyo, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alikaririwa na Gazeti la The Citizen akisema kuwa Chama Cha Mapinduzi hakina mamlaka ya kuingilia utendaji wa Serikali kwani kinatakiwa kuishia katika ngazi za watendaji wa chama.

Kinana
Wakati huohuo, Lauden Mwambona anaripoti kutoka Tukuyu, Mbeya kwamba, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana amewalaumu viongozi wa chama hicho ngazi za mikoa na wilaya kwa kushindwa kuisimamia Serikali na kusababisha Watanzania wengi wakupoteza imani nacho.

Kinana alisema hayo jana alipokuwa akihutubia wakazi wa Halmashauri ya Busokelo wilayani Rungwe katika Mji mdogo wa Kandete katika siku ya pili ya ziara yake  mkoani Mbeya.

Alisema Serikali Kuu inapeleka fedha nyingi kwenye halmashauri na mikoa lakini matokeo yake zinaishia kwenye matumbo ya watu jambo ambalo limewakasirisha Watanzania wengi.

Aliwataka viongozi wa CCM kufuatilia fedha zinazoingia kwenye miradi ya maendeleo na kama Serikali haikutuma fedha hizo, ipo haja ya CCM kufuatilia kwa viongozi wakuu wa nchi.

Kuhusu uchaguzi ndani ya CCM, aliwasihi viongozi hao kuachana na tabia ya kuwapendelea watu wanaotoka mijini au nje ya eneo husika wanaotaka kuwania uongozi badala ya kuwasikiliza kwanza wagombea wanaotokana na wananchi wenyewe.

“Tuachane na tabia ya kuwateua vigogo wenzetu au wenye fedha kugombea nafasi za uongozi ndani ya CCM au Serikali. Tuwasikilize wananchi wanamtaka nani,’’ alisema.
Leo Kinana anatarajia kuendelea kuwahutubia wananchi wa vijiji vya Masoko na Ikuti.
CHANZO CHA HABARI NI MWANANCHI

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate