Hata hivyo, baadhi ya majirani walisema huwa wanawaona watu wakiingia katika nyumba hiyo lakini ajabu kunakuwa hakuna kelele zozote.
Chanzo chetu cha habari kimesema kuwa waumini wa kanisa hilo hula nyasi na baadaye kutapika, hali inayowafanya waamini kuwa kwa kufanya hivyo, wametakasika kiroho kwa kujazwa Roho Mtakatifu.
Habari zinasema huduma hiyo ilianzishwa Afrika Kusini na Mchungaji na Nabii Daniel Lesego mwaka 2002.
Imedaiwa kuwa kwa sasa waumini hao wapo kwenye mfungo ambao watu hufika kanisani na baadaye kula majani yaliyopo nje ya kanisa hilo wakisema kwamba Roho Mtakatifu huongoza mtu kula chochote huku ikidaiwa kuwa manyasi hayo ni chakula kutoka mbinguni.
Gazeti hili linaendele kufuatilia habari hii.
No comments:
Post a Comment