Akizidi kushusha ‘vesi’ mbele ya kinasa
sauti cha Risasi Jumamosi, Kajala alisema anaamini siku zote bifu
zinarudisha nyuma maendeleo hivyo Wema kupatana na Penny ni jambo la
busara kwani ni moja ya chachu ya kufanya mambo mengine yaendelee kwani
hata yeye hapendezwi na mabifu.
“Hata mimi natamani kupatana na Wema. Mabifu ni mambo ya kitoto sana,
kwa kweli nimefurahi sana kuona Penny na Wema wamepatana kwani ni
marafiki wa siku nyingi sana na wanastahili ifike sehemu vitu viishe na
maisha yaendelee kama kawaida,” alisema Kajala.
Alipoulizwa Kajala kama kweli yupo tayari
kupatana na Wema na uwezekano huo upo, Kajala alisema muda wowote
wanaweza kukaa na kumaliza tofauti zao.“Hata mimi siku si nyingi
tutaweka mambo sawa kwa sababu bifu hazijengi, hazina maana hata kidogo
ni kufanya mambo yasiende mbele tu, inabidi tubadilike,” alisema Kajala.
Wema na Kajala walikuwa mashosti wa damu lakini mwaka jana mwishoni
waligombana huku chanzo kikitajwa kuwa ni kugombea mwanaume ambaye
alifahamika kwa jina la CK.
No comments:
Post a Comment