KWENU mashosti wa miaka !٪chungu mbovu,!&waigizaji Aunt Ezekiel na Wema Sepetu !٪Madam.!&Vipi mko poa? Mambo yanakwendaje lakini?
Salamu sana ama baada ya salamu, mimi ni mzima wa afya. Namshukuru Mungu. Naendelea na michakato yangu ya kila siku si mnajua tena mjini mipango, tutalala uzeeni!
Madhumuni ya barua hii ni kutaka kuwapongeza kwani sikufurahishwa na ugomvi wenu uliokuwa umefika pabaya.
Sikufurahishwa kwa sababu sikuona hoja ya msingi ambayo iliwafanya nyinyi mfikie hatua ya kutoleana maneno mazito utadhani hamkuwahi kuwa marafiki wakubwa.
Hivi hoja ile tu ya Aunt kudaiwa kuipigia promo shoo ya Diamond ambaye kwa sasa haziivi na Wema ndiyo ilisababisha mtoleane kauli nzito kiasi kile? Mlifikia hatua ya kusema hamzikani, kweli kabisa? Inasikitisha.
Chanzo cha ugomvi wenu kilikuwa dhaifu. Kwanza taarifa nilizonazo, Aunt mwenyewe hakuipigia promo shoo hiyo kwa hiari yake bali mtandao ndiyo ulitumia jina lake pasipo kuwa na ridhaa yake. Nyinyi hata hakuwaza kwa umakini, mkajazwa maneno na wapambe, mkagombana.
Hata hivyo, hata kama ingekuwa ameposti kwa ridhaa yake, tatizo liko wapi? Kwani ugomvi wa Wema na Diamond unamhusu nini Aunt? Hata kama unamhusu, huoni huyo Diamond anayemchumkia Wema, mfanyakazi wake, Moze Iyobo ni mpenzi wa Aunt, je hakuwa na sababu ya kumuunga mkono bosi wa mpenzi wake ili apate fedha nyingi amlipe vizuri Iyobo?
Ndugu zangu, hata iweje, mtu huwezi kuwazuia maadui wako wote wasiongee na rafiki yako. Kuna baadhi ya vitu vinawaunganisha maadui zako na rafiki yako na vinaweza kuwa ni vya muhimu, huwezi kuvizuia hata siku moja.
Mfano mdogo ni huo, Moze aliye chini ya Diamond ndiye baba mtarajiwa wa mtoto wa Aunt.
Kwa vyovyote vile, kuna wakati lazima Aunt atajikuta amekutana na Iyobo akiwa na Diamond. Hawezi kuacha kumsalimia. Hawezi kumuwekea bifu Diamond halafu akabaki salama na Iyobo ambaye ni muajiriwa wa Diamond.
Yote kwa yote bado niwasisitizie tu, chanzo cha ugomvi wenu hakikuwa na mashiko, mlinisababisha hadi nifikirie kwamba huenda kuna kitu kilikuwa kimejificha nyuma ya pazia.
Kabla hamjapatana, akili yangu ilifika mbali kimawazo hadi nikasema isije ikawa ni yale yaliyotokea kwa Kajala Masanja na Wema ya kukwapuliana bwana au mengine yanayofanana na hayo. Mungu awaepushie yasitokee.
Niwashauri kama kaka yenu kwa uzito wa kushibana mliokuwa nao hampaswi kuwa mnagombana bila sababu za msingi. Mabifu hayana maana. Ni matumaini yangu kupatana kwenu ni jambo jema kama walilofanya Ally Chocky na Asha Baraka.
Warembo kama nyinyi mnapendeza mkikaa pamoja, mkijenga tasnia ya filamu pamoja.
Hakuna sababu ya kugombana hadi ugomvi wenu kuwafikia wazazi, si busara hata kidogo.
Bila shaka mtakuwa mmenielewa. Nawatakia ushosti mwema.
Mimi ni swahiba wenu,
.........
Erick Evarist
No comments:
Post a Comment