EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, December 7, 2012

SAKATA LA NGASSA: Simba yaishtaki Azam kwa TFF.

BAADA ya klabu ya Simba kulaani kitendo cha Azam FC kumuuza mchezaji Mrisho Ngassa kwa El Mereikh ya Sudan, klabu hiyo sasa umeamua kushtaki suala hilo kwa Shirikisho la soka Tanzania (TFF).

Juzi, Azam FC ilitangaza kumuuza Ngassa kwa dola 75,000 huku ikipanga kumpatia dola 50,000 kama dau la kusaini mkataba wa miaka miwili.Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, Azam wamefanya uhuni katika mazingira ya kumuuza Ngassa kwani nyota huyo ana mkataba na Simba utakaokwisha Mei 31, 2013.

Alisema kwa mujibu wa makubaliano yaliyopo kwenye mkataba wa Ngassa, Simba na Azam zote zina mamlaka na mchezaji huyo, hivyo hakuna mmojawapo kufanya maamuzi bila kumshirikisha mwingine.
 
“Mkumbuke mbali ya dola 25,000 tulizotoa kwa Azam FC, tuliingia gharama nyingine za kumshawishi zaidi kama gari, donge nono, pia tulimpa kazi ya ziada kocha wetu kuhakikisha anapandisha kiwango cha Ngassa,” alisema.
Kamwaga alisema Azam wanajichanganya juu ya suala hilo kwani awali waliandika barua kuwa Ngassa amepata timu, hivyo anataka kuondoka Simba kabla ya kuandika barua nyingine kuwa wameamua kumuuza kwa sababu Simba imemsainisha mkataba mwingine.

“Kwa hali hii inaonesha jinsi gani Azam wanavyotapatapa…sisi hatujamsainisha mkataba mpya na kama wana uhakika huo waulete, ukweli ni kwamba mkataba wetu na Ngassa ni kuichezea Simba hadi Mei 31 na baada ya hapo kama atataka rurejea Azam, kubaki Simba au kwenda timu nyingine ataamua,” alisema.

Kamwaga aliongeza kuwa hawatakuwa tayari kumpoteza nyota huyo kirahisi na tayari wamendika barua TFF kuitaka kutotoa hati ya uhamisho wa kimataifa (ITC) kwa El Mereikh.
“Pia tumeishtaki Azam TFF kwa kukiuka sheria 17 za soka kwani kitendo hicho si cha kiungwana na kinapaswa kukemewa kwa nguvu zote,” alisema.
Naye mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage, na mwenyekiti wa kamati ya usajili, Zakaria Hanspope, wamewasili nchini Uganda kufuatilia baadhi ya mambo ikiwemo kuteta na Ngassa juu ya suala hilo.

Kamwaga alisema viongozi hao pia watafuatilia suala la kocha hivyo wakiwa huko, watazungumza na Kocha Kinnah Phiri wa timu ya taifa ya Malawi.
“Wamekwenda huko wakiwa wamekamilika kwani hata masuala ya Okwi yatamalizwa hukohuko na mengineyo mengi,” aliongeza Kamwaga.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate