EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, June 3, 2013

GARI LA WEMA NYANG’ANYANG’A.

Na Mwaija Salum
GARI la Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ limepata ajali na kuwa nyang’anyang’a huku dereva aliyekuwa akiliendesha akiumia vibaya.
Gari la Wema kwa ndani baada ya ajali hiyo.
Habari zilisema kuwa ajali hiyo ilitokea maeneo ya Morocco, Kinondoni jijini Dar, wikiendi iliyopita ambapo dereva huyo ambaye inadaiwa ni ‘jamaa wa Wema’ aliyetajwa kwa jina moja la Robby aliumia mguu wa kushoto na taya hivyo kukimbizwa hospitali (jina halikupatikana mara moja).
Gar la Wema baada ya ajali.
Gari la Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006/07 lililopata ajali ni lile dogo aina ya Toyota Mark X lenye namba za usajili T 426 CHM ambalo liliharibika vibaya sehemu ya mbele huku vibaka wakidaiwa kutumia nafasi hiyo ‘kulisafisha’ vitu ndani.

WEMA: SIJAWAHI KUMSALITI DIAMOND

WEMA Sepetu ametengeneza kichwa cha habari akidai hajawahi kumsaliti aliyekuwa mpenzi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond’ enzi zile walipokuwa wamezama kwenye dimbwi la mahabat.
                                   Wema na Diamond enzi hizooo.
“Maisha yangu yote tangia nimeanza mapenzi na Nasibu…sikuwahi kuwa unfaithful (msaliti). I used to be very faithful to him (nilikuwa mwaminifu sana kwake) na tulikuwa tunapendana sana… nilikuwa nimesharidhika na maisha ambayo niko nayo,” alisema Wema.
 
Mara kadhaa Diamond amewahi kukaririwa katika vyombo vya habari akimtuhumu mlimbwende huyo alikuwa akimsaliti pindi walipokuwa wapenzi. Tuwaachie mambo yao! Wasituchoshe.

MASTAA ‘UNGA’ UTAWAMALIZA

 
                                                     Rehema Chalamila ‘Ray C’.
LEO Michano haitaegemea kwa msanii au staa mmoja. Habari mbaya ni kwamba baadhi ya wasanii wetu wamejikita kwenye matumizi, usafirishaji na biashara haramu ya dawa za kulevya.
                                                                             Msafiri Diouf.
Wasanii mna mashabiki wengi. Sibishi katika hilo. Kama mlikuwa hamjui, mashabiki wanawapenda. Hawapendi kuwaona mkipoteza maisha mkiwa wadogo kwa sababu ya madawa ya kulevya.
Kama hamjui, madawa ya kulevya au unga au poda au baga kama mnavyoita limekuwa ni janga la kitaifa sasa.
                                                                 Aisha Madinda.
Mkitaka kuamini ninachokisema katizeni mitaa ya Kinondoni-Manyanya, Dar muone vijana wadogo wanavyovuja udenda wakiwa hawajiwezi kiafya. Hakika nguvu kazi ya taifa langu inapotea, familia nyingi na taifa vinaathirika kisa ni starehe inayopatikana katika kubwia unga, uvutaji bangi, unywaji pombe wa kutupwa, matumizi ya mirungi, shisha na vileo vingine.
 
Sawa, kila mtu anahitaji starehe lakini siyo hiyo ambayo kwa sasa mmetumbukia humo.
Kama mlimsikia Prodyuza wa Bongo Records, Paul Mathyasse ‘P-Funky Majani’ alisema kuwa 
 
Albert Mangwea ‘Ngwea’ aliyefariki wiki iliyopita aliingia kwenye matumizi ya unga kwa sababu ya ‘stress’ tangu mwaka 2006.

Bodi ya Mikopo yataka wanafunzi kuzingatia muda

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa msisitizo kwa wanafunzi waliohitimu kidato cha sita mwaka huu tayari kujiunga na vyuo vya elimu ya juu kuanza mara moja na kuzingatia ratiba.

Mkurugenzi wa mawasiliamo wa bodi hiyo, Cosmas Mwaisobwa, alitoa kauli iyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa wanafunzi hao wanatakiwa kuanza kujaza fomu za maombi na kuwa siku ya mwisho ya kupokea maombi hayo ni Juni 30 mwaka huu.

“Bodi inasisitiza kuanza mchakato wa kuomba mikopo kwa waliomaliza kidato cha sita na kuzingatia muda uliotolewa kujaza fomu za maombi na kuziwasilisha kwenye ofisi za bodi,” alisema.
Akizungumzia kuhusu wanafunzi wanaoendelea na masomo, Mwaisobwa alisema tayari waombaji 62,758 wamekamilisha taratibu za maombi ya mikopo na kujaza fomu stahiki, tangu utaratibu huo ulipozinduliwa rasmi Mei Mosi mwaka huu.

“Hadi sasa mchakato kwa waombaji wa mikopo kwa mara ya kwanza na wanafunzi wanaoendelea na masomo unaendelea vizuri ambapo wengi wamejaza fomu kwa njia ya mtandao,” alifafanua.
Katika mwaka wa masomo wa 2012/13, bodi hiyo iliwapatia mikopo waombaji 94,703, ambao wako katika vyuo na taasisi mbalimbali za elimu ya juu nchini.

Kiini cha mgogoro wa gesi Mtwara.

Chanzo cha vurugu kuhusu gesi zilizotokea hivi karibuni mkoani Mtwara, kinaelezwa kuwa ni vuguvugu la kisiasa lililowaingia wananchi kiasi cha kujenga chuki kubwa dhidi ya Serikali baada ya kupata mahubiri ya wanasiasa.

Inaelezwa kuwa mzozo huo ulianza rasmi mwaka jana baada ya Serikali kuituma kamati ya kuratibu Maoni ya Sera ya Gesi ambayo ilifika mkoani Mtwara, Novemba 16, mwaka jana kukusanya maoni ya wananchi.

Katika mikutano yake mjini Mtwara, inaelezwa kuwa wananchi wengi hawakukubaliana na wazo la kusafirisha gesi kwenda nje ya Mtwara kwa njia ya bomba.

Hali hiyo ndiyo iliyowafanya viongozi wa vyama vya NCCR-Mageuzi, TLP, UDP, ADC, DP, APPT Maendeleo, Sau na Chauma, kuungana na kuhamasisha wananchi kuhusu suala hilo.
Inaelezwa kuwa hilo lilifanyika Desemba 6, mwaka jana.

Katibu Mkuu wa Muungano huo, Selemani Litope ,alisema mikutano kati ya viongozi wa vyama hivyo na wananchi ilianza Desemba 12. Mikutano hiyo iliyopewa vibali na Jeshi la Polisi ilifanyika Desemba 12, 16, 19 na 22 na Desemba 27 yalifanyika maandamano makubwa.

“Tuliona kuna malalamiko mengi ya wananchi kuhusu suala gesi kusafirishwa kwenda Dar es Salaam, tukaona tuungane ili tufikishe kilio cha wananchi serikalini, kwa sababu tunaamini kwamba, kuisafirisha gesi hiyo ni kuwanyima wananchi fursa ya kufaidika,” alisema Litope.

ALICE ASHINDA TAJI LA REDD'S MISS DAR CITY CENTER.


Mshindi wa Redd's Dar City Center, Alice Isack (katikati) akiwa na mshindi wa pili, Clarah Paul (kulia) na mshindi wa tatu, Fatma Hussein (kushoto). (Picha na Habari Mseto Blog)

Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu (kushoto) akiwa na wadau wa urembo.

Warembo walioingia katika hatua ya tano bora.

Jaji Mkuu wa shindano hilo Wema Sepetu akiwa na majaji wenzake wakifuatilia shindano la Redd's Miss Dar City Center.

Hoyce Temu akitoa utaratibu wa kujibu maswali.

SALSHIA ISDORE NDIYE REDD'S MISS GEITA 2013



Mshindi wa taji la Redd’s Miss Geita 2013, Salshia Isidore (katikati) akiwa mwenye furaha wakati wa kupiga picha ya pamoja na warembo wqenzake Stella Magerezi (kulia) aliyeshika nafasi ya pili na Mshindi wa tatu wa shindano hilo, Nurieth Rashid. Salshia aliwashinda warembo wenzake 12 waliokuwa wakiwania taji hilo pamoja nae.

MREMBO Salshia Isidore amechaguliwa kuwa Redd’s Miss Geita 2013 baada ya kuwashinda warembo wenzake 12 katika shindano lililifanyika Jumamosi Juni 1, kwenye ukumbi wa Desire uliopo mjini Geita.

Mwelekeo wa Tanzania mpya kujulikana leo chana Tume ya Mabadiliko ya Katiba itakapozindua rasimu ya Katiba Mpya kwenye tukio la kihistoria litakalofanyika kwenye Viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam.

Dar es Salaam. 
Mwelekeo wa Taifa la Tanzania utaanza kujulikana leo mchana Tume ya Mabadiliko ya Katiba itakapozindua rasimu ya Katiba Mpya kwenye tukio la kihistoria litakalofanyika kwenye Viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam.

Watanzania wanasubiri kwa hamu kuona kama rasimu hiyo itakuja na majibu ya maswali magumu, makubwa ya muundo wa Muungano, madaraka ya Rais, uteuzi wa mawaziri kutokana na wabunge, muundo wa wakuu wa mikoa/wilaya na muundo wa mihimili mingine miwili ya dola; Mahakama na Bunge.


Uzinduzi wa rasimu hiyo unafanyika baada ya Tume hiyo kufanyia kazi ya uchambuzi wa maoni ya wananchi. Maoni hayo yalitolewa na wananchi wapatao 1,015,564 kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na waliohudhuria mikutano ya moja kwa moja, waliotuma ujumbe mfupi wa simu (sms), barua pepe na kutumia mitandao ya kijamii.

Idadi ya makundi yaliyotoa maoni ni 170 zikiwamo asasi 22 za dini, kiraia 72, taasisi za Serikali 71, vyama vya siasa 19, viongozi na watu mashuhuri 43 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.
Rasimu hiyo ndiyo itakayopelekwa kwenye Mabaraza ya Katiba na itajadiliwa miezi mitatu ili kuona kama mapendekezo ya Tume hiyo baada ya kuchambua maoni hayo ya wananchi yanafaa au yanahitaji marekebisho.

Tume ya Pinda yaibua madudu zaidi Elimu.

Dar es Salaam.
Tume ya Kuchunguza Matokeo ya Kidato cha Nne iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda imebaini zaidi ya matatizo 20 yanayozorotesha kiwango cha elimu na hata kusababisha maelfu ya wanafunzi kufeli mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Tume hiyo, Profesa Sifuni Mchome alisema inachunguza mfumo mzima wa elimu na kuwa suala la Matokeo ya Kidato cha Nne mwaka 2012 ni moja kati ya mambo wanayoyafanyia kazi.

Mchome ameeleza hayo siku moja baada ya gazeti dada la ‘The Citizen’ kuchapisha habari za kujiuzulu kwa mmoja wa Wajumbe wa Tume hiyo, Rakesh Rajani aliyefikia uamuzi huo kutokana na kile alichosema ni kutoridhishwa na pendekezo la kufutwa kwa matokeo ya mtihani wa kidato cha nne.

Alisema ripoti ya Tume hiyo itakayowasilishwa kwa Waziri Mkuu, Juni 15 mwaka huu, imebaini mambo mengi ikiwa ni pamoja na mitalaa kupitwa na wakati pia idadi ya wanafunzi kuwa kubwa na kuelemewa kwa mfumo wa elimu nchini.

“Kuna mambo ya kuangalia ubora, kuna suala la ofisi na taasisi mbalimbali zinafanya kazi gani? Vipi uwajibikaji wake, majukumu yake na mgawanyo ukoje, Ofisi ya Kamishna inahusika vipi na mitihani, huku kote tumeona kuna matatizo,” alisema.
Alisema pia morali ya walimu imeshuka, jambo linalofanya wengi kuwa tayari kuachana na kazi hiyo wakipata jambo jingine la kufanya.

BALOZI WA TANZANIA AFRICA KUSINI ALIPOWASILI MSIBANI KWA ALBERT MANGWEA.

LIVE kutoka Mbezi Beach Dar es Salaam - Mh #RadhiaMsuya Balozi wa #Tanzania nchini #AfricaKusini atembelea nyumbani kwa wafiwa wa Albert Mangweha
LIVE kutoka Mbezi Beach Dar es Salaam - Mh #RadhiaMsuya Balozi wa #Tanzania nchini #AfricaKusini atembelea nyumbani kwa wafiwa wa Albert Mangweha
Mh #RadhiaMsuya balozi wa Tanzania Africa Kusini akizungumza na wasanii pamoja na wadau wa mziki mawili machache na baada ya hapo ameweza kuondoka kwenye eneo hili la msiba Mbezi Beach

LADY JD ATANGAZA SIKU YA SHOW YAKE,TAR.13 MAHAKAMANI,14 SHOW YAKE,15 SIKU YA KUZALIWA YEYE

#TEAMANACONDA mpango ndio huu.
DIARY YA LADY JAY DEE (03:00Usiku) Ukurasa wa leo anatokea mkali Proffesa Jay, Unataka kufahamu Lady Jay Dee anakwenda kufanya mchongo gani naye?

Katika ukurasa huu hu pia anatokea Chidi Benz na wengine pia, Fuatilia hapa kila kitu ambacho wanakifanya na Binti Commando na uweke maoni yako hapa.

#TEAMANACONDA mpango ndio huu.
Hatimaye Lady Jay Dee Ataja tarehe ya show yake ya miaka 13. Ni tarehe 14 June 2012.

"Long week end 13th June Mahakamani, 14th June Miaka 13 ya Jide. 15th June Bday ya Jide....it's June, ni mwezi wangu. #Team Gemini/Anaconda"

PICHA 6 ZA MASKANI KWA MAREHEMU MANGWEA SINZA,CHUMBA CHAKE NA MDOGO WA DARK MASTA.

Nilikuwa na Msanii Mirror, Muro na Jordan kwenye Nyumba aliyo kuwa anaishi Rapper Ngwear, Ipo Sinza Jijini Dar es salaam. Kwenye hii nyumba alikuwa anaishi na Manager wake Muro, Mirror na Jordan Da Prince Ambaye ni mdogo wake Dark Master. Jordan aliletwa na kutambulishwa kwa Manager Muro kama msanii na Ngwear, iliaweze kusaidiwa katika kazi zake za mziki.

Sunday, June 2, 2013

Mtikisiko Polisi, vigogo watarajiwa kustaafu.

Moshi/Dar.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Jeshi hilo zimedokeza kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali Said Mwema anatarajiwa kustaafu mwezi ujao na haijafahamika kama ataongezewa mkataba ama la.

Vyanzo mbalimbali vimedai kuwa japokuwa IGP Mwema anasita kukubali kuongezewa muda, lakini Rais Jakaya Kikwete anaonelea aongezewe muda ili wamalize pamoja uongozi wao mwaka 2015.
IGP Mwema ambaye alikuwa Ofisi ya Polisi wa Kimataifa (Interpol) Jijini Nairobi, Kenya, aliteuliwa kushika wadhifa wake huo mwaka 2006 na Rais Kikwete, kumrithi Omar Mahita ambaye alistaafu.

Habari zinasema endapo IGP Mwema hatapewa mkataba wa ama miaka miwili, basi ni dhahiri Rais Kikwete atakuwa na kibarua kigumu cha kuanza mchakato wa kumtafuta mrithi wake.

IGP Mwema anachukuliwa kama mmoja wa viongozi wa juu wa Jeshi hilo aliyelifanyia mapinduzi makubwa aliposhika madaraka hayo, ikiwamo kuja na dhana ya ulinzi shirikishi ama Polisi Jamii.

Tayari mabadiliko hayo yameaanza kufanyika kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni jijini Dar es Salaam, Charles Kenyela kuhamishiwa makao makuu ya jeshi hilo.
Taarifa zaidi zimepasha kuwa nafasi nyingine ya juu ambayo kuna dalili ya kuwepo kwa mabadiliko ni ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), inayoshikiliwa na Robert Manumba.
Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya jeshi hilo aliyekuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa (jina linahifadhiwa), amehamishiwa makao makuu wakati tayari kuna taarifa za yeye kustaafu.

Hata hivyo, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Advera Senso alipotakia kueleza juu ya taarifa hizo za mabadiliko ndani ya jeshi hilo, kutokana na muda wa kustaafu kwa maofisa hao kufika alisema hizo ni taarifa za hisia.

Membe: Tanzania haiwezi kuomba radhi Rwanda

Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe amesema kamwe Tanzania haitaiomba radhi Rwanda, baada ya Rais Jakaya Kikwete kuishauri nchi hiyo kufanya mazungumzo na upinzani ili kumaliza vita katika eneo hilo la Maziwa Makuu.
Serikali ya Rwanda iliitaka Tanzania iombe radhi kwa madai kuwa kauli ya Rais Kikwete ni kama tusi kwao na kwamba wao hawawezi kukaa na kuzungumza wapinzani ambao ni wauaji.

“Kama Rwanda haitaki kufuata ushauri wa Rais Kikwete inatakiwa kuuacha na siyo kumtaka aombe radhi,” alisema.
Membe alitoa ufafanuzi huo bungeni jana wakati akijibu hoja mbalimbali za wabunge katika mjadala wa makadirio ya matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa mwaka 2013/2014.

Tamko hilo la Serikali limekuja ikiwa zimepita takriban siku sita tangu Serikali ya Rwanda kutoa tamko la kupinga ushauri huo uliotolewa na Rais Kikwete wakati akiwa katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU), uliofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate