EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, June 23, 2012

MAMA KANUMBA ANUNUA JUMBA

 
Imelda Mtema na Erick Evarist
ZIMEKATIKA siku 75 tangu kufariki dunia kwa supastaa wa filamu za Bongo, Steven Charles Kanumba, Aprili 7, 2012. Mama mzazi wa marehemu huyo, Flora Mtegoa mambo yamemnyookea ambapo amenunua jumba kubwa la kifahari, Risasi Jumamosi linakuwa la kwanza kuripoti.
CHANZO CHATEMA NYETI
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika, mjengo huo upo Kimara Temboni jijini Dar es Salaam ambapo mama huyo na familia yake (akiwemo Seth Bosco) wamehamia.
Sanjari na wao, pia magari matatu ya marehemu, Toyota Hiace, Toyota Lexus na Toyota GX 110 yamepiga kambi huko, kila moja likiwa na sehemu yake ya kuegesha.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, kwa sasa mama Kanumba hana makazi tena pale Sinza Kijiweni ambako ndiko palipofanyikia msiba wa mwanaye hadi kuhitimisha na arobaini yake.
KUNA USIRI
Chanzo kikadai kuwa kuhama kwa mama huyo na familia yake kutoka Sinza kwenda Temboni kumegubikwa na usiri bila kufafanua siri hiyo inatokana na nini!
MAPAPARAZI WAINGIA MZIGONI KUCHUNGUZA
Baada ya gazeti hili kuzidaka nyeti hizo, Alhamisi ya Juni 21, 2012 lilituma timu ya waandishi wake kwenda kupata uhakika wa madai hayo na kujiridhisha kabla ya gazeti halijakwenda mitamboni.
NJE YA NYUMBA
Ndani ya geti kuu la nyumba hiyo yenye bati la kijani, alikutwa mdogo wa marehemu Kanumba, Seth Bosco akipata chai huku upepo mwanana ukimpuliza. Mama Kanumba alikuwa akiendelea na shughuli zake za kawaida.
Mbali na kuwaona wawili hao, mapaparazi wetu waliendelea na uchunguzi wao ambapo waliipiga raundi nyumba hiyo na kujionea magari yote matatu ya marehemu  yakiwa yamepaki huku jamaa mmoja akiwa juu ya bati kuweka dishi la televisheni la ‘kuangalizia’ Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya ‘Euro’ yanayoendelea kwa sasa nchini Poland na Ukraine.
Makachero wetu walipojiridhisha kuwa mama Kanumba ndiyo kaweka makazi yake mapya, lilipiga picha za kumwaga kisha lilimwendea hewani Seth na kuzungumza naye ili kupata ukweli mwingine.

SAUTI YA SETH KUTOKEA TEMBONI
Paparazi: Mambo Seth?
Seth: Poa tu, nani mwenzangu?
Paparazi: Unaongea na Risasi Jumamosi hapa.
Seth: Enhe, lete habari.

Paparazi: Inasemekana mmehama pale Vatican, mmehamia wapi?
Seth: Aaa, tumehamia Temboni huku.
Paparazi: Ni kweli huko mmenunua nyumba?
Seth: Ni kweli.
Paparazi: Shilingi ngapi?
Seth: Mh! Hilo swali anayeweza kujibu ni mama kwamba ni shilingi ngapi na mambo mengine yote.
Risasi Jumamosi lilipomsaka mama Kanumba kwa kutumia simu yake ya mkononi, hakupatikana hewani siku hiyo.
MJENGO WA BEI MBAYA
Hata hivyo, Risasi Jumamosi lilifanya uchunguzi na kunyaka baadhi ya nyaraka zinazoonesha kuwa mjengo huo umenunuliwa kwa shilingi milioni themanini (80,000,000) za Kibongo.
MASTAA HAWAJUI
Gazeti hili lilijaribu kufanya mawasiliano na baadhi ya mastaa wa filamu Bongo kama wanajua mama yao huyo amehama Sinza lakini kila aliyeulizwa hakuwa anafahamu na kuwa ‘sapraizi’ kwake.
Mwanyekiti wa Klabu ya Bongo Movie, Jacob Steve ‘JB’ alipovutiwa uzi na kuulizwa alisema hajui kama mama Kanumba amehama Sinza.

HII HAPA SAUTI YAKE
“Amehama pale? Duu! Mimi sijui kaka.”
MWAKIFAMBA AKIWA NJIANI KWENDA SINZA
Naye Mwenyekiti wa Shirikisho la Filamu Bongo, Simon Mwakifamba alipopigiwa simu kuulizwa, akajibu anaamini mama huyo bado yupo Sinza, na yeye mwenyewe alipanga kwenda siku hiyo ya Alhamisi jioni ili akamjulie hali.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate