EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, July 25, 2012

Huduma za Afya hospitali ya Muhimbili zazidi kuzorota

WAKATI serikali ikiamini Madaktari wamerudi kazini, hali ya matibabu katika Hospital ya Taifa Muhimbili imezidi kudorara. Akizungumza na MTANZANIA katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, mmoja wa madaktari (jina tunalo), alisema licha ya madaktari kurudi kazini hali ya matibabu imezidi kupoteza mwelekeo tofauti na hali halisi.

“Huwezi kusema madaktari wamerudi kazini wanatoa huduma…hii siyo kweli, kwa sababu madaktari bado mahitaji yao ya msingi hayajatatuliwa..huwezi kuwa na daktari mwenye manung’uniko kazini, halafu ukasema anatoa huduma bora kwa mgonjwa,

“Mimi nasema ukweli, hospitalini kuna huduma duni zisizokidhi mahitaji ya wagonjwa,nikizungumza kama mwananchi wa kawaida ni kwamba madaktari wanaingia kazini na kusaini lakini hawatoi huduma vizuri,” alisema

“Nawashangaa Watanzania, sijui kwanini wanashindwa kudai haki zao... ukiingia hospitali hazina vifaa lakini utashangaa watanzania wako kimywa,sisi madaktari tukigoma tunaonekana wabaya,” aliongeza daktari huyo.

Akizungumzia hali ya huduma pamoja na nia ya kufanya maandamano, Katibu Mkuu wa Chama Cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Rodrick Kabangila alisema nia ya maandamano ipo palepale.

“Niseme nia yetu ya mgomo ipo palepale, lakini sasa hivi tunashughurikia suala la ‘Intern’s kwani suala hili limeingiliwa na masuala ya kisisa kidogo..kwahiyo ndiyo tunahangaia nao kwanza halafu tutatoa taarifa lini maandamano yetu yanafanyika hivi karibuni,

“Hili suala la Interns, limeingizwa siasa sana kwasababu huwezi kusema unamfutia leseni wakati yeye hana kosa…Serikali ilitaka huyu interns, afanye kazi na nani wakati madaktari ambao ndiyo wanamsimamia yeye walikuwa kwenye mgomo,” alihoji Dk. Kabangila.

Alisema malalamiko yao bado yapo palepale na Baraza la Madakatri Tanganyika haliwatendei haki kwa sababu lipo chini ya Serikali.

“Lile baraza lipo chini ya Serikali, unafikiri haki itatendeka kwetu kweli... sisi tunataka baraza ambalo mwenyekiti wake asiwe mwajiriwa wa Serikali..,” alisema Dk. Kabangila.

Akizungumzia hali ya Dk.Steven Ulimboka, Katibu wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Edwin Chitage alisema kwa sasa hali yake inaendelea vizuri.

“Dk.Ulimboka anaendelea vizuri kwa sasa na anaendelea kufanya mazoezi ila siwezi kusema atarudi leo wala kesho…hizo taarifa za kwamba atarejea hivi karibuni zitakuwa zimezushwa tu na watu,” alisema Dk. Chitage.

Alitaja baadhi ya hospitali kubwa alizodai kuathiriwa na tukio hilo la kufukuzwa kazi kwa madaktari, kuwa ni Muhimbili, Hospitali ya Rufaa Mbeya, Bugando (Mwanza), KCMC (Moshi) na Hospitali ya Rufaa Dodoma.

via MTANZANIA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate