EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, July 25, 2012

SAJUKI APATA GONJWA


Gladness Mallya na Erick Evarist
PAMOJA na kwamba afya ya staa wa filamu Bongo, Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ inaendelea vizuri, imegundulika kuwa ana ugonjwa mwingine tofauti na ule uliompeleka India kufanyiwa upasuaji, Risasi Mchanganyiko linakuwa la kwanza kukuhabarisha.
Hivi karibuni, Sajuki alirejea kutoka nchini India alipokwenda kwa ajili ya matibabu ambapo alionekana kuwa na mabadiliko makubwa kiafya jambo lililowapa matumaini mashabiki wake.

HABARI MEZANI
Akizungumza na waandishi wetu, juzi, Jumapili nyumbani kwake, Tabata jijini Dar es Salaam, mke wa Sajuki, Wastara Juma alisema mumewe amegundulika kuwa na tatizo lingine walipokuwa nchini India kwa matibabu.
Alisema, hawakutaka kuweka hali hiyo mapema kwa Watanzania kwa kuhofia kusababisha simanzi, lakini sasa wanalazimika kufanya hivyo ili kuwafanya wajue kinachoendelea kwa staa wao.
“Kwa kweli mume wangu bado anaumwa na amegundulika kuwa na tatizo lingine ila tunamshukuru Mungu anaendelea vizuri,” alisema Wastara kwa huzuni nyingi.

NI UGONJWA GANI?
Kwa mujibu wa Wastara, walipokuwa India (katika Hospitali ya Apollo), Sajuki alifanyiwa vipimo mbalimbali ili kubaini matatizo yanayomsumbua ambapo aligundulika kuwa na tatizo kwenye uti wa mgongo na ngozi ya mwili mzima.
“Ana tatizo kwenye mfupa wa uti wa mgongo, lakini pia anasumbuliwa na tatizo jingine kwenye ngozi. Baada ya madaktari kugundua magonjwa hayo walimuanzishia dawa ya kutibu mgongo na mazoezi kwa ajili ya kumuweka sawa.
“Hizo dawa alianza kuzitumia tulipokuja huku, ambapo pia anaendelea na mazoezi. Tatizo lingine ni hilo la ngozi, ambalo pia anaendelea kutumia dawa,” alisema.

KWA NINI MGONGO?
Akifafanua kuhusu ugonjwa unaoshambulia sehemu ya mfupa wa uti wa mgongo, Wastara alisema madaktari walisema, tatizo hilo linasababishwa na kukaa kwa muda mrefu.
“Jambo hilo tulikubaliana nalo, kwa sababu ni kweli Sajuki huwa anakaa muda mrefu kwenye kompyuta kwa ajili ya kazi zake, lakini pia huwa anaendesha gari kwa muda mrefu. Tunaamini ndiyo chanzo cha ugonjwa huo kama madaktari walivyosema,” alisema na kuongeza:
“Lakini baada ya kupata dawa na ushauri  sasa anaendelea vizuri,  kwa sababu pia anafuata masharti aliyopewa vizuri. Huwa nahakikisha anapata muda mrefu wa kupumzika, hakai muda mwingi na haendeshi sana gari.
“Wamemwambia mambo mengi, hata kuinainama kila mara pia wamekataza. Kimsingi mwenzangu anahitaji uangalizi wa karibu sana. Hata hivyo anaweza kuendelea na filamu ila kwa kuzingatia na scene (onesho) yenyewe, ila kwa sasa anapumzika kwanza ili afya yake itengemae.”

KLINIKI KILA WIKI
Akiendelea kuzungumzia afya ya mumewe, Wastara alisema huwa wanalazimika kwenda Kliniki ya kila wiki katika hospitali moja jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuangaliwa maendeleo yake.
Aidha, alisema kila wiki tatu huwa wanatuma vipimo nchini India katika Hospitali ya Apollo aliyokuwa akitibiwa kwa lengo la kuchunguza maendeleo yake.

KUHUSU UGONJWA WA NGOZI
Wastara alisema, tatizo la ngozi alilonalo mumewe bado hajaanza kutumia dozi yake kwa sababu hawajapata fedha ya kutuma India ili waweze kutumiwa dawa zenyewe.
“Tupo kwenye mchakato wa kutafuta hizo fedha, lakini hali bado ni ngumu na anatakiwa kuanza dozi mapema kama madaktari walivyoshauri,” alisema na kuongeza:
“Mwezi Desemba (mwaka huu) anatakiwa kurudi tena ili aangaliwe tena maendeleo yake kwa ujumla. Yote hiyo ni gharama kubwa sana, lakini tunaamini Mungu atatusimamia.”

GHARAMA ZAMTOA CHOZI WASTARA
Alisema kwa namna mahitaji yalivyo mengi na yanayohitaji fedha, wapo kwenye wakati mgumu kuweza kuyakabili.
“Kiukweli bado tunahitaji msaada wa Watanzania wenzetu. Tunashukuru kwa wale waliojaliwa kutusaidia awali hadi kufanikisha safari yetu ya matibabu India lakini watakaoguswa wanaweza kuendelea kutusaidia.
“Mpaka sasa Sajuki hajaanza dozi ya ugonjwa wa ngozi na zipo nyingine anazotakiwa kuzitumia, lakini hazipatikani hapa...ni mpaka India.”

VIDUME VYAMTOKEA WASTARA
 Akizungumzia suala la usumbufu wa kimapenzi, Wastara alisema ni jambo la kawaida na ni kweli kuna baadhi ya wanaume wanatumia udhaifu wa ugonjwa wa mumewe kumshawishi kimapenzi.
“Kutongozwa ni jambo la kawaida kwa mwanamke, lakini mimi kama Wastara msimamo wangu ni kumheshimu mume wangu. Siwezi kushawishika kwa namna yoyote, kwanza hata hamu yenyewe sina.
“Ninachokiangalia kwa sasa ni afya ya mume wangu. Najua nina wajibu mkubwa wa kuhakikisha namhudumia mume wangu kwa mapenzi yote. Akili yangu haipo kwenye mapenzi kabisa, hali aliyonayo mume wangu inaniumiza sana.
“Kamwe sitamsaliti Sajuki wangu. Wema wake kwangu wakati nikiwa kwenye matatizo siwezi kuulipia kwa kumdhalilisha kwa kutoka na mwanaume mwingine eti kwa sababu anaumwa. Anayewaza kufanya hivyo, akajaribu kwingine, siyo kwangu.”

KALAMU YA MHARIRI
Kwa matatizo aliyonayo Sajuki ni wazi yeye na familia yake bado wanahitaji msaada wa hali na mali ili kuweza kukidhi mahitaji ya matibabu yanayomkabili kwa sasa.
Kama Mtanzania mwenzake, guswa na moyo wa utoaji na Mungu wa Mbinguni atakuongezea katika mifuko yako.
Ikiwa umeguswa, tafadhali tuma mchango wako kwenye akaunti namba 050000003047 yenye jina la Wastara Juma Issa iliyopo katika Benki ya Biashara ya Akiba (ACB) au tumia Tigopesa kwenda namba 0713 666113 yenye jina Wastara Juma.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate