EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, August 18, 2012

Dk Ulimboka avunja ukimya

KIONGOZI wa madaktari, Dk Stephen Ulimboka amewataka watanzania wasiwe na hofu na wasubiri siku maalum ambayo ataweka wazi ukweli wote kuhusu namna alivyotekwa na kuteswa, pia hali yake ya kiafya kwa sasa.

Dk Ulimboka ambaye amerejea nchini hivi karibuni kutoka Afrika Kusini alikokuwa amepelekwa kwa ajili ya matibabu alisema jana kuwa hawezi kuzungumza lolote kwa sasa  na aachwe apumzike kwani ameugua na ametengana na familia yake kwa muda mrefu, hivyo anahitaji muda wa kuwa peke yake.

“Niacheni nipumzike kwa sasa. Wakati muafaka ukifika, nitasema yote. Sitaacha kusema, muda muafaka ukiwadia nitayasema yaliyonitokea na taratibu maalum zitaandaliwa ili nizungumze na watanzania,” alisema Dk Ulimboka.

Alisema hawezi kuzungumza bila utaratibu maalum bali atazingatia taratibu zitakazoandaliwa na uongozi wa Jumuiya ya Madaktari (MAT) ndipo ataueleza umma na kusema  yaliyo moyoni kuhusu kutekwa na kupigwa kwake.

“Haya mambo yatawekwa hadharani lakini ni kwa utarartibu maalum, si kama hivi mnavyotaka ninyi. Kila mtu ananiuliza halafu mnakwenda kuandika ya kwenu, naona hii imekuwa kama biashara sasa,” alisema.

Aidha Dk Ulimboka alivilaumu baadhi ya vyombo vya habari kwa  kuandika habari ambazo si za kweli kuhusu suala la kutekwa na kuteswa kwake na kusema kuwa wamekuwa wakipotosha ukweli wa tukio lenyewe.

“Wengine wananipigia simu na kunijulia hali, nikiwaambia basi wanaenda kuandika tofauti, kwa mfano juzi wameandika kuwa nimeonekana nikipanda boti, jambo ambalo si la kweli,” alisema.
Akizungumzia hilo, makamu wa rais wa MAT, Prinus Saidia alisema Dk Ulimboka kwa sasa yupo mapumzikoni na atazungumza kwa kina baada ya muda mfupi.

Alisema madaktari wamekubaliana kuwa Dk Ulimboka aachwe apumzike baada ya kipindi kigumu cha muda mrefu lakini atazungumza kwa undani wakati ambao utakubaliwa na jumuiya hiyo.

Wakati huo huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Haki za Raia, Siasa na Mwenendo wa Bunge, Marcossy Albanie amesema  ataitisha mkutano wa waandishi wa habari siku ya Jumatatu ambapo pamoja na mambo mengine atazungumzia suala la kutekwa na kuteswa kwa Dk Ulimboka.

Albanie hakutaka kuweka wazi ni nini hasa ambacho atakwenda kuzungumzia kuhusu Dk Ulimboka bali alisisitiza kuwa taasisi yake itazungumzia suala hilo la kutekwa na kipigo cha daktari huyo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate