EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, August 14, 2012

MUME: MKE WANGU KANIIBIA NYETI


Na Makongoro Oging’
UNAWEZA usiamini lakini ukweli ni kuwa Juma Ali (48), mkazi wa Mtoni jijini Dar es Salaam amedai kwamba mkewe, Hadija Chande (40) (pichani) amemchezea kishirikina, hivyo kujikuta hana nyeti ya kiume.
Taarifa kutoka katika vyanzo vyetu vya habari zimedai kwamba Ali kwa sasa hana uwezo wa kufanya tendo la ndoa kwa kuwa nyeti yake imetoweka kimiujiza na shutuma zote anambebesha mkewe kwamba ndiye aliyefanya ‘mchezo’ huo.
 
Habari zinadai kuwa kutokana na hilo, kumezuka mgogoro mkubwa kati ya wanandoa hao kwani mume amekuwa akimdai mkewe  arejeshe nyeti yake, jambo ambalo halijawezekana.
Imedaiwa kuwa Hadija, mara baada ya kufunga ndoa na Ali mwaka 1996 alikuwa na wivu wa kupindukia, hivyo kuamua kutafuta dawa na kumfanyia mumewe ili ndoa yao izidi kuimarika lakini mara baada ya kutenda alichoambiwa afanye kama dawa, nyeti ilitoweka na kubaki na ‘kipande’ kidogo cha kusaidia kutoa haja ndogo.
 
“Kutokana na madai ya Ali, mkewe aliamua kufungasha virago na kutoweka nyumbani na kwenda kusikojulikana wakati mumewe yupo kazini,” kilisema chanzo.
Gazeti hili baada ya kusikia habari hizo za kushangaza, lilimtafuta Ali ambaye baada ya kuulizwa kuhusu mkasa huo alititirisha maneno kama ifuatavyo:
 
“Ni kweli hayo uliyoambiwa. Kwa sasa ninachomdai mke wangu aliyetoweka ni nyeti yangu, naomba anirudishie kwani ufumbuzi wa mgogoro wetu hauwezi kupatikana kamwe kama hatazirudisha.
“Hapa unaponiona ndugu mwandishi mimi siyo mwanaume tena. Sina ‘kitu’, hapa kimebaki ‘ kipande’ kama kalamu ambayo haifanyi kazi yoyote. Mke wangu nilipomuoa alinikuta nina watoto sita niliozaa na mke niliyemuacha mwaka 1994, sasa hivi siwezi kufanya tendo la ndoa.
 
“Mgogoro wa kutoweka na nyeti yangu ulianzia mke wangu alipoanza kunilalamikia kuwa natembea nje ya ndoa na akaniahidi kuwa ni lazima atanidhibiti. Madai yake niliyapinga lakini nguo zangu za ndani zikaanza kupotea. Nilipomuuliza alisema angeninunulia nyingine, nilikuwa na mashaka naye, nikamuomba anirudishie lakini hakufanya hivyo.
 
“Mara tu chupi zangu zilipoanza kupotea, nikawa sisikii hamu ya tendo la ndoa. Mwezi uliopita, nyeti yangu ikawa imetoweka, nilipomuuliza akawa mbogo. Ilipofika Julai 28, mwaka huu, saa sita mchana, nilitoka kazini na kurudi nyumbani lakini sikumkuta mke wangu na nguo zangu za ndani na soksi hazikuwepo pia.
“Licha ya nguo, picha zangu nazo alizichukua na nilipomuuliza mtoto wangu Karim akasema mama yao amesema kabeba vitu vyake vyote ndani ya nyumba na hakumuambia anakokwenda.
 
“Nilikaa siku tatu, nikaamua kwenda serikali ya mtaa wetu ya Mtoni na wakanishauri nikaripoti polisi ambako nilipokwenda walifungua jalada namba namba MTG/RB/2054/2012. Polisi waliniambia nitakapomuona popote niwaarifu ili wamkamate.
“Nilisafiri kwenda mikoani na niliporudi nilikuta barua kutoka Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) wilayani Temeke ikinitaka niende katika ofisi zao kwa kuwa mke wangu kafungua shauri la kutaka talaka, jambo nililogundua kuwa alishauriwa na rafiki zake ili nimpe nyumba.
“Najua kilichomtoa mke wangu nyumbani ni kushindwa kunirejeshea nyeti yangu, hapa ameshaniua hivyo siyo rahisi kwake kurudi kwani hatafurahia tendo la ndoa. Ili kesi hii iishe sharti ni moja tu kwamba anirudishie nyeti yangu,” alisema Ali.
Mke wa Ali, Hadija alipohojiwa kuhusu sakata hilo alikuwa na haya ya kusema:
 
“Mbona na mimi sizai na sina hata mtoto wa dawa? Kuhusu kwamba nimetoweka na nyeti yake ni kwamba mimi sijui mambo hayo, asinifuatefuate.”
Mjomba wa Hadija, Abdalah Chande alipoulizwa kuhusu sakata hilo, alikiri kuelezwa na Ali kuhusu mgogoro huo na kudai kuwa alimzushia kuwa yeye ndiye anayemharibu mpwae (Hadija) na akampiga marufuku kukanyaga nyumbani kwake, akaahidi kushirikiana na baba yake mdogo kutatua tatizo hilo.
Baba mdogo wa Hadija  aliyejitambulisha kwa jina moja la Juma alipoulizwa kuhusu mgogoro huo alisema hautambui lakini alimlaumu mwanaye huyo kwa kupeleka shauri hilo Bakwata kabla ya kulifikisha kwake.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate