Mkazi wa Dar es Salaam aliyejitambulisha kuwa mmoja wa wamiliki wa shule
ya Mtakatifu Benedict ya Dar es Salaam, amesema suala la mwalimu
aliyehusika na suala la kuvua nguo wanafunzi darasani kama adhabu ni
uhalifu wa kawaida usio na madhara kwa mtoto.
Akijitambulisha kwa jina la Renatus Michael, amesema uhalifu mkubwa ni wa kupiga wanafunzi viboko kama ambavyo imezoeleka kufanywa na baadhi ya walimu katika shule mbalimbali nchini.
Michael, ambaye alizungumza jana na gazeti hili kwa njia ya simu akidai kuwa Dar es Salaam, aliongeza kuwa uongozi wa shule una mpango wa kumchukulia hatua mwalimu aliyehusika na tukio hilo ambaye ni wa jinsi ya kike.
“Mimi nawashangaa sana mlivyoandika habari hiyo, hayo ni mambo ya shule na huo ni uhalifu mdogo usio na madhara kwa mtoto … ndiyo maana hata Polisi waliliweka pembeni, kwani limekaa muda wote huo … mmeandika kwa ukali kama vile lilikuwa suala la kupiga viboko?” Alihoji huku akilalamikia kuandikwa kwa taarifa hizo.
Alisema tukio hilo ambalo liliwakuta wanafunzi wanne wa kiume lilitokea Julai na mara kwa mara amekuwa na mazungumzo na mzazi aliyetoa taarifa hizo Polisi bila maafikiano.
“Ukweli ni kwamba tuliwahi kukaa naye sehemu mbalimbali na mara ya mwisho tulikutana usiku hotelini eneo la Buza ambapo mzazi huyo alikuwa akilalamika kwa nini mtoto wake afanyiwe kitendo hicho ambacho kingeweza kumwathiri kisaikolojia,” alisema Renatus.
Alisema akiwa mmiliki alijitahidi kumwomba radhi mzazi huyo akimhakikishia kuchukuliwa hatua dhidi ya mwalimu huyo, lakini hakutaka yaishe na ndipo alipotoa taarifa Polisi.
Kuhusu kuchukuliwa hatua mwalimu huyo, alisema uongozi wa shule una mpango wa kufanya hivyo na kwamba ulikuwa ukisubiri kuanza kwa likizo ya Septemba.
Kuhusu ni kwa nini uamuzi juu ya mwalimu huyo uchukue muda mrefu kiasi hicho ikilinganishwa na athari iliyowakuta wanafunzi hao, alisema kuna adhabu ya kumpa mwalimu na kuna adhabu ya wanafunzi, hivyo ni lazima uchunguzi wa suala hilo ukamilike.
Hata hivyo, Renatus alihofia kusambaratika kwa shule hiyo ambayo alidai ni changa ikiwa na wanafunzi pungufu ya 120, akisisitiza kuwa hata wao kitendo hicho hakikuwafurahisha.
via HabariLeo
Akijitambulisha kwa jina la Renatus Michael, amesema uhalifu mkubwa ni wa kupiga wanafunzi viboko kama ambavyo imezoeleka kufanywa na baadhi ya walimu katika shule mbalimbali nchini.
Michael, ambaye alizungumza jana na gazeti hili kwa njia ya simu akidai kuwa Dar es Salaam, aliongeza kuwa uongozi wa shule una mpango wa kumchukulia hatua mwalimu aliyehusika na tukio hilo ambaye ni wa jinsi ya kike.
“Mimi nawashangaa sana mlivyoandika habari hiyo, hayo ni mambo ya shule na huo ni uhalifu mdogo usio na madhara kwa mtoto … ndiyo maana hata Polisi waliliweka pembeni, kwani limekaa muda wote huo … mmeandika kwa ukali kama vile lilikuwa suala la kupiga viboko?” Alihoji huku akilalamikia kuandikwa kwa taarifa hizo.
Alisema tukio hilo ambalo liliwakuta wanafunzi wanne wa kiume lilitokea Julai na mara kwa mara amekuwa na mazungumzo na mzazi aliyetoa taarifa hizo Polisi bila maafikiano.
“Ukweli ni kwamba tuliwahi kukaa naye sehemu mbalimbali na mara ya mwisho tulikutana usiku hotelini eneo la Buza ambapo mzazi huyo alikuwa akilalamika kwa nini mtoto wake afanyiwe kitendo hicho ambacho kingeweza kumwathiri kisaikolojia,” alisema Renatus.
Alisema akiwa mmiliki alijitahidi kumwomba radhi mzazi huyo akimhakikishia kuchukuliwa hatua dhidi ya mwalimu huyo, lakini hakutaka yaishe na ndipo alipotoa taarifa Polisi.
Kuhusu kuchukuliwa hatua mwalimu huyo, alisema uongozi wa shule una mpango wa kufanya hivyo na kwamba ulikuwa ukisubiri kuanza kwa likizo ya Septemba.
Kuhusu ni kwa nini uamuzi juu ya mwalimu huyo uchukue muda mrefu kiasi hicho ikilinganishwa na athari iliyowakuta wanafunzi hao, alisema kuna adhabu ya kumpa mwalimu na kuna adhabu ya wanafunzi, hivyo ni lazima uchunguzi wa suala hilo ukamilike.
Hata hivyo, Renatus alihofia kusambaratika kwa shule hiyo ambayo alidai ni changa ikiwa na wanafunzi pungufu ya 120, akisisitiza kuwa hata wao kitendo hicho hakikuwafurahisha.
via HabariLeo
No comments:
Post a Comment