EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, August 13, 2012

RECHO ABANWA SKENDO YA KUVAA NUSU UTUPU, AJITETEA

 
WIKI hii tunaye mwigizaji Rachel Haule ‘Recho’ ambaye anajibu na kufafanua juu ya maswali ambayo mmemuuliza.
Kuhusu rushwa ya ngono
Ulikuwa unapenda sana kuigiza lakini nafasi ulikuwa hupati, kwenye filamu yako ya kwanza kushirikishwa nasikia ulitoa rushwa ya ngono. Ni kweli? Issa Chongono, Tanga, 0714455748
RECHO: Siyo kweli, aliyenitoa ni mwanamke mwenzangu.
Huyu anamjua
Nakufahamu Recho, unaishi Sinza maeneo ya uwanja wa mpira karibu na Shule ya Grace. Msomaji, 0719476653
RECHO: Ni kweli.
Huyu anaomba urafiki
Recho nakuzimia jinsi ulivyo na umbo zuri, naomba uwe rafiki yangu. Salim Liundi, Dar, 0658110395
RECHO: Asante, karibu.
Anajitahidi
Recho unajitahidi kwenye kuigiza lakini umbo lako ndilo linakubeba zaidi, jipange. Cassian, 0655202202
RECHO: Asante.

Kuhusu kuvaa nusu uchi
Recho una kipaji lakini nataka kujua, je, bila kuvaa nguo za kuonesha mwili wako muvi haiuziki? Queen Materu,  0653436603
RECHO: Nimezoea kuvaa nguo fupi tangu nikiwa mtoto.

Kuhusu yeye
Dada Recho nakukubali kwa kazi yako nzuri, nataka kujua wewe ni kabila gani, una miaka mingapi na umezaliwa wapi? Ramadhani Khamisi, Tanga, 0717236195
RECHO: Mimi ni Mngoni, nina miaka 24, nimezaliwa Dar.

ANAIFUNDISHA NINI JAMII?
Wewe kama msanii kioo cha jamii, unafundisha nini jamii ukivaa nguo nusu uchi? Mama Elvis, Dar, 0656334307
RECHO: Sifundishi jamii kuvaa nguo fupi ila ni kwa kile ninachoigiza.

Atulie na Saguda
Ukweli unajitahidi sana, kaza buti na kama upo na Saguda tulia uepuke skendo. Zulphathy, Dar, 0719777492
RECHO: Asante.

Idadi ya wanaume
Recho umetembea na wanaume wangapi na je, umewahi kupima Ukimwi? Baba Sapnah, Katavi, 0718296327
RECHO: Sijatembea na wengi na Ukimwi nimepima, sina.

Ana shepu nzuri
Una shepu nzuri dada, nini matarajio yenu na Saguda? Gloria, 0719603656
RECHO: Kuoana.

Akihongwa gari je?
Recho hebu kuwa muwazi kwa hili, tafakari hali ya kazi, mapenzi na maisha ya kesho, jinsi ulivyo mzuri ukihongwa Rav4 umsaliti mpenzi wako utakataa? John, Dar, 0752535336
RECHO: Mimi siamini kama maisha yangu ni Rav4.

Ana watoto?
Recho nakufagilia wewe mkali halafu huna skendo, je, una watoto wangapi? Clara Ritte, Arusha, 0766665002
RECHO: Sina.

Yeye na Steve
Wewe na Steve Nyerere mna ukaribu gani maana filamu nyingi uko naye? Timilai Shemalamba, Tanga, 0653702100
RECHO: Steve ni bosi wangu.

Eti alitoka na HemedY
Recho nilisikia ulishawahi kutoka kimapenzi na Hemedy (Suleiman). Charles Mhando, Mwanza, 0759022399
RECHO: Siyo kweli.

Ana muda gani kwenye gEmU?
Una muda gani kwenye filamu na umecheza filamu ngapi ambazo ni za kwako mpaka sasa? Emmanuel Bernard, Arusha, 0756377286
RECHO: Nina mwaka mmoja na nimecheza filamu mbili za kwangu.

Aheshimu vyombo vya habari
Rachel wewe ni msanii na usanii siyo kuuza sura bali ni kuelimisha jamii, endelea kuheshimu vyombo vya habari mwisho ndivyo vitakavyokufanya utoke. Juma, Moro, 0716110028
RECHO: Sawa, asante.

Huyu anaomba ushauri
Dada Recho napenda uigizaji wako na mimi napenda niwe kama wewe, nitafanyaje ili niwe kama wewe? Msomaji, 0762 732514
RECHO: Nenda kwenye vikundi vya sanaa.

Yeye na Prof Jay
Recho una undugu na Prof Jay? Je, ni kweli sanaa haihitaji elimu, una mpango gani na elimu ya sanaa? Nakukubali ongeza bidii. Mr. Kucha, Dar, 0752535336
RECHO: Hapana siyo kweli, mpango wangu ni kujiendeleza zaidi na elimu ya sanaa.

Nje ya uigizaji
Dada Recho nakukubali sana, nje ya uigizaji unajishughulisha na kazi gani na nini malengo yako ya baadaye? Godfrey, Korogwe, 0656071565
RECHO: Mfanyabiashara, malengo yangu ya baadaye ni kuwa msanii wa kimataifa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate