EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 15, 2012

Wabunge: Serikali isiwatishe walimu

WABUNGE wameibana serikali, wakiitaka iache ubabe wa kusitisha mgogoro wa walimu kwa kutumia mahakama badala yake itafute ufumbuzi wa kudumu kwa madai yao.
Wakati kambi rasmi ya upinzani bungeni ikisema kuwa hatua ya wabunge kuzuiliwa kujadili mgogoro huo ni kitendo cha kulihujumu Bunge lenye haki ya kikatiba ya kuisimamia na kuishauri serikali, Mbunge wa Kahama, James Lembeli (CCM), alisema Tanzania ni nchi ya wafanyabiashara, matapeli na wahuni kwa kuwa ndio wanaoweza kufanikisha mambo yao.

Akichangia mjadala wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi jana, Lembeli, alisema ametoa kauli hiyo kuwa walimu, madaktari na wakulima kwa miaka mingi wamekuwa wakilalamika bila kutatuliwa matatizo yao.
Alisema kuwa wakati wa kuficha mambo umekwisha na kuhoji iwapo serikali haioni matatizo ya walimu, madaktari na wakulima.

“Nikimaliza Bunge naenda jimboni. Mimi nadai posho kila siku, mbona sijapelekwa mahakahamani? Kama fedha haipo waambiwe na iwe kwa wote si wachache waendelee kuneemeka. Nchi hii ni ya wafanyabiashara, matapeli wahuni kwa sababu ndio wanaweza kufanikisha mambo yao.
“Serikali inasema madaktari wamerudi kazini, lakini hawafanyi kazi. Mimi nimezungumza haya kwa sababu nasema ukweli na msema kweli mpenzi wa Mungu. Ukweli ndio huo na ukweli unauna, walimu tuwahurumie, wao ndio waliotuchagua kuja bungeni. Waziri atakapokuwa akihitimisha nataka nimsikie aseme hii ni ya watu gani,” alisema.

Pamoja na hayo, alilaani kitendo cha serikali kukimbilia mahakamani kuzima mgomo wa walimu na kusema walimu hawahitaji kubezwa.
“Hii ni sawa na baba na mama wanagombana na kisha baba anakimbilia polisi… walimu wamerudi kazini, lakini hawafanyi kazi. Mshahara  wa sh 200,000 mwalimu ataishije? Kama sisi wabunge tunalalamika kwa nini tusiwatetee? Kuna haja ya serikali kuzungumza na walimu, madaktari, wakulima,” alisema.

Naye Susan Lyimo kwa niaba ya Kambi ya Upinzani alisema kuwa kutokuwapo kwa mgomo halisi kusiifanye serikali ifikiri kwamba imemaliza tatizo la madai ya walimu, kwani kuna migomo baridi ambayo athari zake huwa mbaya zaidi ya migomo halisi.
Alibainisha kuwa iwapo walimu wataachwa na kinyongo kama walivyo sasa, na kama wataamua kulipa kisasi kwa kuwafundisha watoto vitu visivyo halisi, kuna hatari kubwa kuwa na kizazi kisicho na elimu kabisa na hatimaye kuwa na taifa lisilojiweza katika nyanja zote.

Kutokana na hali hiyo, kambi hiyo imeishauri serikali kufanya mazungumzo na Chama cha Walimu nchini (CWT), ili kufikia maridhiano na hivyo kusonga mbele katika kuboresha elimu.
Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalumu, Maulida Komu (CHADEMA) akichangia hoja hiyo, alikemea tabia ya serikali kumbilia mahakamani kuzima migomo pamoja na kushindwa kuchukua juhudi za dhati kuboresha sekta ya elimu nchini.
“Tunajenga taifa la aina gani? Watoto wanatoa vibiyongo kwa kukaa chini, halafu ninyi bado mnacheka cheka…ndio nchi hii itachukuliwa. Kwani vita maana yake nini? Yote yatatokana na wananchi kuchoka.

“Tuzingatie elimu, tutafakari ni kitu gani kifanyike kuikomboa elimu yetu na si kuendelea kucheka cheka,” alisema.
Akizungumzia wanafunzi wanaomaliza darasa la saba huku wakiwa hawajui kusoma na kuandika, msemaji wa kambi ya upinzani, alimtaka Waziri wa wizara hiyo, Dk. Shukuru Kawambwa na Naibu wake, Phillipo Mulugo, kuwajibika kutokana na sakata hilo.
Pamoja na hilo, aliitaka serikali kutoa tamko rasmi bungeni kuhusiana na jambo hilo, ili jamii iweze kuelewa kinachochangia hali hiyo.

“Kambi ya upinzani inashangaa mpaka sasa Waziri wa Elimu na Naibu wake bado wapo madarakani wakishangilia ushindi wa kuliongoza taifa kushika nafasi ya kwanza duniani kufaulisha wanafunzi 5,200 wasiojua kusoma na kuandika,” alisema Lyimo.
Mbunge wa Mbozi, Godfrey Zambi, aliitaka serikali kuwachukulia hatua walimu na wasimamizi wa mitihani ambao watabainika kuwapatia mitihani wanafunzi.
Alisema watumishi wa serikali wakiwamo walimu wanagoma kutokana na maslahi duni na kueleza kuwa kuna haja kwa serikali kulizingatia suala hilo.

“Walimu wanafanya kazi kubwa na ngumu… wote tuliomo humu ndani tunatokana na walimu, hivyo kuna ulazima wa serikali kuzingatia matatizo ya walimu. Kuvutana, kupelekana mahakamani hakutatusaidia,” alisema.
Akisoma taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya  Huduma za Jamii, Martha Mlata, alisema kamati imebaini utaratibu unaotumika kutoa mikopo ya elimu ya juu haukidhi mahitaji ya wanafunzi hususan wanaotoka katika familia duni.
Mlata  alisema kamati inasikitishwa na hali ya kukosa masomo kwa baadhi ya wanafunzi wanaojihusishana na vitendo vya migomo katika taasisi mbalimbali nchini ikiwamo Chuo Kikuu cha Dodoma, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na IMTU.

Awali, akiwasilisha bajeti yake, Waziri Kawambwa, alisema katika mwaka huu wa fedha, wizara kupitia Bodi ya Mikopo itatoa mikopo kwa wanafunzi 98,772 wa vyuo vya elimu ya juu.
Alisema pamoja na hilo, itasimamia ukusanyaji wa marejesho ya mikopo ya sh bilioni 18 kwa kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wadaiwa na waaajiri watakaoshindwa kutimiza wajibu wao na kuwatafuta wadaiwa kupitia viongozi wa serikali za mitaa.
Alisema mwaka jana, wizara ilitoa mikopo kwa ajili ya chakula, malazi, vitabu na viandikia kwa wanafunzi 93,176 wakiwamo wahadhiri 256.
Dk. Kawamba aliliomba Bunge kuridhia mapato na matumizi ya sh bilioni 724.471 kwa mwaka wa fedha 2012/2013.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate